komedi
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 204
- 17
Wakati marais mbalimbali wakiwa kwenye kikao huko Geneva nchini Uswisi kulitokea majigambo ya walinzi wa marais kati ya wale wa nchi zilizoendelea na wa nchi zetu hizi.....
Mlinzi wa Rais wa china alinyoosha mkono wake akagusa miwani yake na kuurudisha, ghafla gari lililombeba Rais wake likatokea na Rais wa China akashuka. Yule mlinzi akajisikia fahari sana kwa wenzake.
Kuona hivyo mlinzi wa Rais wa marekani akaamua kuonyesha kuwa wao ni namba moja akakohoa kidogo na mara hiyo gari la Rais wa marekani likatokea na Rais wa marekani akashuka. Yule mlinzi akajisikia fahari mno kwa teknolojia yao ya mawasiliano.
Walinzi wa Afrika wakajisikia vibaya sana mbele ya wenzao.
Ghafla mlinzi wa Rais wa Tanzania ambaye ni kijana wa kifipa akapigiwa simu na walinzi wengine na kumuuliza kama Rais anaweza kuletwa mahala hapo.
Huku walinzi wa kizungu wakiwa wanacheka sana kuona teknolojia inayotumika ilivyo ya kizamani, Mlinzi wa kifipa akajibu '' subiri kwanza nataka nitoe somo hapa''
Akatulia kimya huku marais wakiwa eneo la wazi nje wakisalimiana na wajumbe wa mkutano, ghafla akaingiza mkono mfukoni akatoa hirizi na kuitupa chini kisha akaiokota na kutoa mwamvuli na kujikinga. Ghafla ikaanguka mvua kubwa sana na kuwalowesha marais wote waliokuwepo. Baada ya dakika moja mvua ikakatika kabisa.
Akapiga simu na kuwaambia wenzake ''sasa Rais anaweza kuja''
Wale walinzi wa marekani wakabaki wanakodoa macho huku wakiuliza.
''what kind of intercom is that?''
Mlinzi wa Rais wa china alinyoosha mkono wake akagusa miwani yake na kuurudisha, ghafla gari lililombeba Rais wake likatokea na Rais wa China akashuka. Yule mlinzi akajisikia fahari sana kwa wenzake.
Kuona hivyo mlinzi wa Rais wa marekani akaamua kuonyesha kuwa wao ni namba moja akakohoa kidogo na mara hiyo gari la Rais wa marekani likatokea na Rais wa marekani akashuka. Yule mlinzi akajisikia fahari mno kwa teknolojia yao ya mawasiliano.
Walinzi wa Afrika wakajisikia vibaya sana mbele ya wenzao.
Ghafla mlinzi wa Rais wa Tanzania ambaye ni kijana wa kifipa akapigiwa simu na walinzi wengine na kumuuliza kama Rais anaweza kuletwa mahala hapo.
Huku walinzi wa kizungu wakiwa wanacheka sana kuona teknolojia inayotumika ilivyo ya kizamani, Mlinzi wa kifipa akajibu '' subiri kwanza nataka nitoe somo hapa''
Akatulia kimya huku marais wakiwa eneo la wazi nje wakisalimiana na wajumbe wa mkutano, ghafla akaingiza mkono mfukoni akatoa hirizi na kuitupa chini kisha akaiokota na kutoa mwamvuli na kujikinga. Ghafla ikaanguka mvua kubwa sana na kuwalowesha marais wote waliokuwepo. Baada ya dakika moja mvua ikakatika kabisa.
Akapiga simu na kuwaambia wenzake ''sasa Rais anaweza kuja''
Wale walinzi wa marekani wakabaki wanakodoa macho huku wakiuliza.
''what kind of intercom is that?''