Bodi ya mikopo imeoza

Chimunguru

JF-Expert Member
May 3, 2009
10,678
4,349
Leo nilikwenda pale tirdo msasani kufuatilia mkopo wa mdogo wangu anasoma pale muccobis. jina lilitoka lkn hawajampa mkopo eti hakupeleka results slip za frm 4. nimekaa pale km 2hrs nasubiri jina la mgo wangu liitwe, hatimaye km saa sita na nusu likaitwa nikaingia ndani nikaongea na mhusika akaniambia nijaze frm upyaa nikajaza ile namaliza tu natoka nje costa mbili zikaingia wanafunzi wa Ardhi institute hao si mchezo, wakadai wamekuja kuchukua cheki zao, wakafunga mlango hakuna mtu kuingia wakawa wanaimba nyimbo pale, walianza na wimbo ya taifa halafu wakaimbo wimbo wa solidarity forever. Baadaye km 45min hivi polisi wakaja na defender lao na kamanda wao wakapaki pale nje kamanda akazama ndani ya ofisi after a while mwakilishi wa wanafunzi akaitwa aliporudi akaja na orodha nzima ya wanafunzi wa ardhi walioomba mikopo. nimeondoka nikawaacha hapo wanaendelea cheki status yao ya mikopo. kwa kweli pale bodi pameoza bila msukumo hawafanyi kazi ni magari ya thamani tu wamepaki nje pale.
 
nilichukua na clip kabisaaa ya madai yao, tatizo ni ku upload kwenye mobile hakuna option. ntaiingiza kwenye pc then mtaiona.
 
Back
Top Bottom