Bob Marley vs Lucky Dube

Nampenda sana Luck Dube, msiba wake uliniuma zaidi ya Misiba yote Duniani lla Bob ni namba nyingine, nimepata kuona ducumentaly ya Bob kiukweli jamaa alizaliwa kwa sababu maalum.

Ukianza tu alivyo zaliwa baba mzungu mama mswahili, baba kumtosa mama akapambana. Hakika Bob ni mpango maalumu wa Mungu, kuonyesha binadamu wote ni sawa.

Tazama hata brand yake mpaka leo hipo sokoni Duniani kote, na ipo juu kiheshima zaidi kuliko brand yoyote ile Africa na Dunia. Japo waafrika hatuipi thamani kama wazungu.

Kutoa wanasiasa mashuhuli wa Afrika walio taka kuleta umoja wa Afrika Kama Mwl Nyerere, Mungu amlaze mahali pema baba wa Taifa huyu. Bob pia ni mtu aliyekuwa na mziki wa kuifanya Afrika kuwa moja.

Namu heshimu sana mtu mwenye ndoto za Afrika iwe moja, kwa vijana wasasa ni mtu kama Masud Kipanya, anafanya kazi nzuri sana sana. Hongera sana kaka Masud kupitia crew nzima ya Maisha plus. Endeleza ndoto zako maana kitendo cha kuwa kusanya vile vijana mataifa mbali mbali ni jambo zuri sana. Kazi imebaki kwa viongozi tulionao kuamua tuu kuhiunganisha Afrika kwa faida ya umoja wa vizazi vijavyo.
 
Mwezi huu Jumamosi iliyopita, tar 15, taasisi ya Robin Hood Foundation iliyoanzishwa na Jay Z pamoja na mkewe, waliandaa onyesho la ma-star wakubwa. Nick Minaj alikuwepo. Nick Minaj ni story nyingine kwa rappers wa kike, next to none. Majority tunasema hivyo na inaaminika hivyo. Lakini wakati Minaj akiwa back stage, mara hamad 'L Boogy' a.k.a Laurin Hill, Fugees first lady anaingia. Minaj alienda chini mojakwamoja, akasujudu. Akamshika miguu 'L Boogy', akimwambia "asante dada kwa kutufungulia milango" (paving the way). Wazaramo wanaita 'kutotola'. Uzi wako ndo umenikumbusha hii story. Ni juzi tu.


'
 

Attachments

  • L2.jpg
    7.1 KB · Views: 73
Lucky dube ni Noma zaidi. Tafuta wimbo wake unaitwa let jah be praised na Good girl utaleta mrejesho hapa binafs bob naona reggae yake ilikaza sana haikuwa na radha ukilinganisha na Dube japokuwa yeye ndiye muasis wa reggae music lkn bado leo nyimbo za Lucky dube ndo zinaongoza kwa kupigwa
 
Asante mkuu nimekuelewa saana mkuu
 
Nimekusoma ndugu yangu kuna kitu pia nimejifunza. Asante saana
 
Sikutegemea kama angepatikana mtu akaandika mawazo kama yako... Uzi umekaa kama unataka kushindanisha lakini sasa nimeongeza vitu fulan fulani katika uelewa wa muziki wa regae
 
Aseee hii sikuwahi kuipataa asante mkuu
 
Luck dube ni.mzurii Latino bob...nyie hyu Jamaal alikuwa real genius. ..ebu cklza who the cap fit. ..real situation. ..nk.....utaona urofautiii...mkubwa ..sna Wada...
 
Aseee hii sikuwahi kuipataa asante mkuu
Unamjua vizuri L'boogy Lauryn Hill? Lauryn aliolewa na Rohan Marley mtoto wa Bob na kupata watoto.....5 nafikiri. Lauryn Hill ni Goddess......anaheshimika mno, anajielewa mno. Kiufupi nikama vile ameendeleza spirit ya Bob kwa namna yake.

Ni sawa kabisa Nicki kushow respect yakiwango cha juu kabisa kwa Lauryn......heshima tele kwa Ms Lauryn Hill
 
Kingine kuhusu Tuff Gong na Lucky Dube

Lucky Dube is nowhere near Bob Marley and Bob Marley couldnt do it without Rastafarai because it's Rastafari teachings and consciousness that eleveted Jamaica and the world at large

Bob is the man......real man.

Bob si wahivivivi.....nyimbo zake ni kama vile Jah alikuwa anaandika.....Neil Garrick anasimulia Bob never struggled to write lyrics.

Skippa alikuwa na nyimbo nyingi si mchezo na zote noma sana.

Nimeshangaa unamfananisha Honorable Bob Marley na Luck Dube.

Mkuu wewe inaonyesha haujui sana kuhusu Reggae music.....unafuatilia juujuu tu.
 
Pamoja na kwamba Bob anaonekana ni legend zaidi, lakini personally nakoshwa zaidi na nyimbo za Dube, inawezekana kutokana na wakati ambao mimi nimeanza kufuatilia na kuelewa kinachoimbwa, beats pamoja na melody. Ujumbe wake unatouch mazingira ya Kiafrica Kuliko Bob.
Political Game, Mr, Taxman, The way it is,
Rip what you sow, Slave , Together as one, Its not easy, usizi (huu sielewi kinachoimbwa, bali napenda melody)
 
Majina yaliyosumbua hapa duniani ni matatu mpaka sasa.
1.YESU
2.MUHAMAD
3.BOB MARLEY
uwe na siku njema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…