Blandina Nyoni ni NANI!


Kama hizi habari ni za kweli basi tena nchi hii inaangamia kwa viongozi wake kukosa maarifa!! Yaani wizara ambayo inatakiwa iwe na ambulance za kubeba wajwazito ndio inaendekeza ufahari huo? Yaani wazazi wanalala mizungu ya nne lakini inaonyesha ufarahi kwenye maonyesho yasiyokuwa na tija!! Ila sishangai kwa maana kuna siku moja nilikuwa naongea na RAS mmoja wa mikoa ya kusini akaniambia kuwa walikuwa na shughuli ya kuwahamasisha watu kunawa mikono ikabidi wakodi matenki ya maji kwa zaidi ya Tshs. million 10 wakaenda kuwafundisha kunawa mikono kisha wakaondoka na matenki yao na kuwacha wanakijiji hawana maji ya kuendelea kunawia mikono!!! Kule kijijini kulikuwa hakuna maji badala ya kutumia mamilion hayo kuchimba visima wao wakakodi matenki kifisadi. Na hao wa afya wanavaa kitanashati kwenye maonesho wakati hakuna vitanda mahospitalini wana maana gani? Kuna siku watu tutachapana viboko hadharani. Nimechoka ngoja nili fresh kwa kuangalia mpira wa Arsenal na Man U huenda nikasahau kama naishi Tanzania !!
 
Kweli zile suti kiboko kuna jamaa mwaka jana alivaa akasema hata kwenye harusi yake hakuvaa suti kali hivyo
 

Mkuu hapa umenena.
Naamini huyu mama hana umakini wowote zaidi ya kuwa mkurukukaji. Na huu ukurupukaji unaweza ukawa na faida vilevile kwa sababu hii inaonyesha ni jinsi gani serikali haijui waajiriwa wake wako wapi. Kama serikali haina taarifa juu ya locations za watumishi wake, hiki ndicho chanzo cha kutafunwa kwa pesa za serikali. Iwapo serikali inatambua mtumishi wake yuko labda hospitali ya Manyoni wakati mtumishi huyo yuko hospitali ya Musoma. Hii inamaanisha kuwa kuna mshahara mmoja utaenda Manyoni na huku kule Musoma akilipwa mshahara wake. Sasa huo unaokwenda Manyoni nani anapokea?

Serikali especially Utumishi wanatakiwa kuwa na Database ya watumishi wake na kuwe na uwezo wa wizara tofauti ku-access database hiyo kwa watumishi wa wizara husika. Hiki ni kitu rahisi, hata mimi mwenyewe naweza kutengeneza. Lakini tatizo vijana wasomi ndiyo wanapondwa kuwa wameharibiwa na mageuzi au demokrasia. Hapa kuna shamba la mtu kuvuna.
Let us get SERIOUS kuwatendea wananchi wetu HAKI.
 
Vita ya kibiashara unaleta huku.kwani yeye ndie purchasing officer?
Kabombe

nadhani una matatiz kidogo... Blandina may not be a purchasing officer but she has influence on decisions

Hii thread has come out very late... I am sure one day yatakuja yote but binafsi nimepata wasiwasi na maonyesho, ajira, vitisho kwa madaktari, fraud mbalimbali, nepotism kwenye selection ya board members (confirmed) nk.

she is a hard working woman, but she sometimes reward herself too much
 
Blandina Nyoni aliwahi kuwa mhadhiri Mzumbe university, akafanya kazi USAID, kabla ya kuwa Mhasibu Mkuu wa Serikali, alikuwa kamishna TRA. Yeye ana sifa ya kufuatilia watu wake wa chini kwa kweli anaijua kazi yake ipasavyo:smile-big:
hizi feva zitatuua.........
 
safi sana, wewe ni mdau

Mama nyoni ni mchapa kazi, lakini she is overly corrupt na ana issues nyingi sana za kuvunja taratibu, power abuse etc

Ila hili la kuingilia madaktari amekosea.... tukumbuke kwamba hata zile ajira walizotangaza mwaka jana za wataalam wa afya, hakufuata taratibu kadhaa na tumeajiri hawakuwa involved

ana calliber ya kuvimba kichwa na kusahau taratibu

but with the current blunder, reality is zeroing on her
 
Naomba niwaombe pia tujadili jinsi hii Mariedo inavyoshinda hzo tenda,maana mleta mada amejaribu kuonyesha wasiwasi wake
 
Naomba niwaombe pia tujadili jinsi hii Mariedo inavyoshinda hzo tenda,maana mleta mada amejaribu kuonyesha wasiwasi wake
kushinda tender ni moja but kutumia bilioni wakati wagonjwa tena wake zetu na dada zetu wanajifungua mbele ya watoto ni another issue
 
kushinda tender ni moja but kutumia bilioni wakati wagonjwa tena wake zetu na dada zetu wanajifungua mbele ya watoto ni another issue

Mariedo hashindi zabuni hata moja bali kinachofanyika ni kwamba Chief Supplies Officer anaambiwa tu 'fanya utakachofanya lakini nataka nguo zitoke duka la Mariedo'. Na Chief Supplies officer hawezi kupinga kwa vile ni yeye Blandina aliyemleta hapo baada ya kumwondoa mtangulizi wake ambaye alikuwa ni strict katika procedures za manunuzi.
 
Wadau,

Kwa kifupi sana huyu ni small house ya mamvi' kwisha
 
Du haya mambo yanatisha,huyu mama si board member wa Wama!!!!!???
Au haya yanayojadiliwa yanauhusiano!MOD MSIITOE THREAD HII , TUTAONA MENGI......KUMBUKA MAONESHO MENGINE YANAKARIBIA !
Kwani TAKUKURU HAWAWEZI KUFUATILIA MCHAKATO WA DUKA LAMARIEDO KUSHINDA TENDA HIZI MARA ZOTE, JE FEDHA HIZI ZILIPITISWA NA BUNGE!!!!!!!!????????????
 
She is more of a liability to the Kikwete regime than an asset; the sooner they offload her the better for their survival!! Mama huyu ana madudu mengi sana toka alivyokuwa katibu mkuu wizara ya Maliasili, how she manages to survive with all these dubious deals only God knows!
 
kwa hiyo leo kimenuka rasmi hiii ilikuwa mwaka jana may 2011,kafanya madudu mangapi wizarani?
 
Kweli siku za mwizi ni arobaini. Naona leo ndiyo siku ya arobaini.
 
Achukuliwe hatua.. Apelekwe mahakamani kujibu tuhuma hizo.
 
Maumivu ya kichwa huanza polepole kisha.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…