Binti wa kambo anajilengesha kwa baba wa kufikia

Binti wa kambo anajilengesha kwa baba wa kufikia

Joined
Sep 9, 2014
Posts
16
Reaction score
3
Mambo vipi jamiiforum members.

Bila shaka nyote mpo pouwaa na wazima sanaa! Nina rafiki yangu ana umri kama miaka 47 hivi tupo naye ofisi moja ijumaa aliyopita alikuwa na kihoja cha mwaka.

Ni kwamba, yeye alifiwa na mkewe kama miaka mitatu iliyopita alikuwa mwanamke wa kihehe kutoka Iringa ila walibahatika kupata watoto wawili wote wa kiume wanasoma primary.

Sasa baada ya kuishi ki-bachelor kwa muda wote huo akaamua kutafuta na kumpata mwanamke mwingine mjane lakini ambaye tayari ana binti mmoja mwenye miaka takribani 23 anayeishi naye.

Sasa huyu rafiki anasema kadri siku zinavyozidi kwenda huyo binti wake wa kufikia anakuwa anabadilika tabia kwa kasi sana.

Mwanzoni alikuwa kila asubuhi lazima binti atoe shikamoo, ila kwa sasa hakuna tena.

Anaweza kumwambia za asubuhi au akaamua kukaa kimya kabisaaa. Wanaweza kuwa wapo kwenye dinning table wanakula, ila mama mwenye nyumba akiinuka kidogo kwenda jikoni kufuata kitu, binti anaweza nyanyua kijiko cha "baba yake" huyo na kuanza kumlisha.

Binti anaweza kuvaa khanga moja tu, kisha akakaa sebuleni anaangalia TV (mpira) na baba yake mama akiwa amelala, kitu ambacho mwanzoni hakuthubutu hata kumsogelea.

Jamaa akiwa ofisini meseji kila wakati za kumjulia eti anaendeleaje na kazi.

Imekuwa too much hata saa ya kulala meseji inakuja "eti baba lala salama"kweli jamani hali hii?

Cha ajabu na kusikitisha kuliko yote, binti sasa anamuuliza eti kwa nini asiwachukue waende weekend moja trip ya Bagamoyo kuliko kukaa tu home anaboreka sana.

Yote hayo ni sehemu ndogo ya mkanda mzima wa vituko vya huyo kwa jamaa.

Mimi binafsi nilichomshauri ni kwamba amvutie tu pumzi na azidi kumvumilia, ila akiona hali inazidi kuwa mbaya achukue MAAMUZI MAGUMU kama liwalo na liwe.

Wadau mnashauri vipi.
 
hayo maamuzi magumu ndo mazuri
akishindwa magumu, aamue marahisi tu yani aende bagamoyo akale mzigo
 
mmmh hiyo nayo hatari... unaposema "achukue MAAMUZI MAGUMU kama liwalo na liwe..." unamaanisha nini??? cha maana mwambie huyo rafiki yako aongee na mama wa mtoto kuhusu hiyo tabia kisha watajua wanafanya nn kunusuru aibu inayotaka kutokea.
 
kama kawa kuku na mayai yake
 
Kwanza inaelekea na wewe amekudharau sana mkuu hadi kuja kukuomba ushauri tukiangalia yalio nyuma ya pazia.... na wewe pia kuliombea ushauri hapa ni bora yake.

Kwa Mwanaume kukosa msimamo na kutokujua hadhi yake, kutojua anachokitaka ni kitu kibaya.
Hivi kwanini hili neno ''NIKAJIKUTA'' limekua rafiki sana wa sisi wanaume.... punde tu utasikia jamaa akisema nikajikuta nimeshamlala mwanangu nisaidieni mawazo.
 
Kukosa msimamo na kutokujua hadhi yako, kutojua unachokitaka ni kitu kibaya sana kwetu wanaume. Hivi kwanini hili neno ''NIKAJIKUTA'' limekua rafiki sana wa sisi wanaume.... punde tu utasikia jamaa akisema nikajikuta nimeshamlala mwanangu nisaidieni mawazo.

Kumbuka sio mimi lakini bali ni rafiki yangu
 
Ushauri wako wa kishetani kabisa, eti liwalo na liwe.
 
Mwambie Rafiki yako aache upuuzi what if kama yeye akisikia kuna mtu anataka kuwapakua hao wanae wa kuzaa? Hizo ni nyeeege pori hazitamfikisha kokote. Mkewe akifahamu upuuzi wake lazima atamfix ndo hauo tunaskia alilala hakuamka
 
huyo rafikio ni mtu wa ajabu tna mhuni sana hajui nidhamu ya baba ndani ya nyumba....
hata yeye anamtamani ndo maana anaon pouwa kuendeleza hizo tabia za kipuuzi

wanaume kama hawa majanga sana hna msimamo hana kaul ya ubaba ,...
baba ni mtu wa kuheshimika angekuwa anajiheshimu huyo binti asingeweza kufanya hayo

aone aibu kuelezea huu upuuzi kwa maana tayar anamtamani ndo mana anaendeleza kimy kimy bila kumweleza mkewe
 
Back
Top Bottom