Binafsi nadhani Tulia Ackson asingechukua fomu ya kuwania uspika kwa sasa

Mgeni wa Jiji

JF-Expert Member
Jul 27, 2017
7,923
13,405
Waungwana salamu

Nisipoteze muda mwingi niende moja kwa moja kwenye mada.

Kujiuzuru uspika kwa Mhe. Ndugai kumezidi kuonesha ni kwa namna gani kama Taifa bado hatufahamu mambo mengi ya kisiasa, kiutawala, uraia na kiutendaji.

Wapo waliombeza Mhe. Ndugai wapo walioshitushwa na wapo walioangalia kujiuzuru kwake kama fursa kisiasa na hawa ndio lengo la mada yangu japo wengine nitaongelea kwa uchache sana.

Wanasiasa wetu bado wanasiasa za ama kubahatisha au siasa zisizo na mikakati ya muda mrefu. Bila kupepesa nimuongelee mhe. Tulia.

Binafsi nadhani asingechukua fomu ya kuwania uspika kwa sasa, huu ni moja ya mkakati mbovu aliowahi kupanga.

Ipo wazi Mhe. Tulia ni ngumu kwake kuukwaa uspika na hili si kwamba hawezi kufanya kazi hapana ni kutokana tu na muundo wa awamu ya sasa unampa wakati mgumu sana kuwa spika wa bunge.

Mbaya zaidi uwezekano wa Mhe. Tulia kubaki kuwa mbunge pekee ni mkubwa pia. Nadhani alipaswa kutulia asome mchezo asubiri 2025 kama uhai ukiwepo aingie mchakatoni.

Hili somo liwaguse wanasiasa wote hasa vijana, ikitokea nafasi ya ama uchaguzi au kinyang'anyiro chochote kama haukuwa na mpango nao bora ukaacha ikakupita, siasa sio mchezo wa bahati nasibu ni mipango na mikakati.

Kama ukiona kila nafasi zikitokea unataka kugombea jua bado haujaijua siasa unayoifanya, jipange vizuri.

Kila la kheri
 
Naibu Speaker anaelinda ufisadi kwenye Taifa hafai kuwa speaker,labda akawe speaker wa familia yake🐒🐒🐒
 
Kama katiba inamruhusu basi ni haki yake.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Mkuu nadhani hujamuelewa mtoa mada.

Katiba inamruhusu almost kila mtu kugombea uspika na ni haki zetu sote lakini si lazima kugombea kutokana na mazingira. Mimi na wewe tuna vigezo vyote hivyo lakini hatujagombea, si bahati mbaya ila sio kila ruhusa upatayo mkuu unaitumia

TULIA KACHEMKA KUGOMBEA USPIKA
 
Huyu yafaa kula kichwa ili akae pembeni manake mtaka yote kwa pupa, hukosa yote. Mtu bado Naibu Spika halafu anataka awe Spika. Achia cheo kimoja ili upate kingine, anaona kama atapokosa Uspika atabaki na Unaibu wake. Hiyo ni tamaa ya madaraka!!
 
Kama katumwa uspika ni wake,Ila Wabunge wa CCM wakimchagua huyo Tulia tumekwisha,hajapewa nafasi tayari anajipendekeza kwenye mhimili mwingine akipewa tumekwishaaaa,litakuwa Bunge la ndio mzee Kama bunge la Ndugai enzi za Magu
 
Kujiuzuru uspika kwa Mhe. Ndugai kumezidi kuonesha ni kwa namna gani kama Taifa bado hatufahamu mambo mengi ya kisiasa, kiutawala, uraia na kiutendaji.
Naunga mkono hoja!, twende mdogo mdogo, Ndugai, kosa lake ni nini?.
Wapo waliombeza Mhe.
Its true tupo, tuliombeza kuomba msamaha wa uongo kwa matamshi yake, na tukamshauri awajibike
wapo walioangalia kujiuzuru kwake kama fursa kisiasa
Ni kweli, kwanza kujiuzulu kwake ni mpango wa Mungu, ili tupate fursa ya kupata Spika Bora
Binafsi nadhani asingechukua fomu ya kuwania uspika kwa sasa, huu ni moja ya mkakati mbovu aliowahi kupanga.
Ubovu ni upi?.
Ipo wazi Mhe. Tulia ni ngumu kwake kuukwaa uspika na hili si kwamba hawezi kufanya kazi hapana ni kutokana tu na muundo wa awamu ya sasa unampa wakati mgumu sana kuwa spika wa bunge.
Ugumu ni wapi?, wakati ni kawaida yetu akitoka Spika mmoja, naibu spika ndio huwa anakuwa spika!.
Mbaya zaidi uwezekano wa Mhe. Tulia kubaki kuwa mbunge pekee ni mkubwa pia.
How?, huyu tayari ni Naibu Spika, hata asipopitishwa na CCM kuwania uspika, yeye ataendelea kuwa Naibu Spika.
Hili somo liwaguse wanasiasa wote hasa vijana, ikitokea nafasi ya ama uchaguzi au kinyang'anyiro chochote kama haukuwa na mpango nao bora ukaacha ikakupita, siasa sio mchezo wa bahati nasibu ni mipango na mikakati.
Ikijotokeza fursa, hakuna ubaya wowote kwa vijana kuchangamkia fursa, aim high, the sky is the limit!
P
 
Sidhani kama ni mjinga hivyo, huwezi jua nini kimepangwa, wameanza na uraisi, wamekuja Bunge, next siajabu Jeshi, hawa Viongozi wote ni marionette na Big Boss hayuko Tanzania…
 
Back
Top Bottom