Bima ya afya (NHIF) kwa hili sio sahihi mnatuibia

bushland

JF-Expert Member
Mar 6, 2015
7,016
4,961
Mfuko wa afya wa bima ya afya wameleta mabadiliko ambayo wengi hatukutarajia, sijajua shida ni uchumi kuwa mbaya au sababu ni nini haswa.

leo nimetoka hospitali kutibiwa nikatoa kadi yangu mapokezi kama kawaida wakati nasubiri kuitwa kama ilivyo ada,nikaitwa nikaambiwa kadi yako ya bima imekataliwa nikauliza sababu sikupewa nikatoka hapo chapu nikaenda hospitali nyingine kubwa tu wanayotumia bima, basi nikatoa kadi kama kawaida wakati nasubiri kuitwa muda ukafika nikaitwa nikaambiwa kuwa kadi yangu ya bima imekuwa rejected nikauliza kivip nikaambiwa niende hapo zilipo ofisi za bima vile sio mbali nikaulize sababu.

dakika saba tayari nipo ofisi za Bima nikauliza mbona imekuwa hivi hospitali nilikotoka wakaniuliza Bima yangu nani alikata nikamtajia ni mlezi wangu, wakasema utaratibu umebadilika siku hizi anaetakiwa kukukatia ni mzazi pekee, nikamwambia mlezi mwenyewe alikuwa hana mtoto hata mmoja na mimi ndie niliekuwa kama mtoto wake wakanijibu hiyo haijalishi.

la pili wanadai pale mtu anapostaafu basi wale wategemezi wake hawana chao tena ,yani ukomo wa matumizi ya bima ndo unafikia hapo.

sasa nauliza huu utaratibu wa aina hii unalenga kumnufaisha nani?
yani kila sehemu pamebanwa hamna hata pa kukimbilia kwa sasa.

alichosema mzee watu wataishi kama masheatani nimeamini.

=====

UPDATE:

=====


Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), unapenda kufafanua juu ya taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa baadhi ya taratibu za Mfuko katika utoaji wa huduma zinalenga kuwaibia wanachama. Madai hayo sio ya kweli na Mfuko unapenda kufafanua Taratibu sahihi zilizopo kwa lengo la kufanikisha utoaji wa huduma kwa wanachama wake kama ifuatavyo;

Habari zaidi soma=>Ufafanuzi juu ya suala la wategemezi wa wanachama wa NHIF, wanachama wastaafu
 
Kuzuia sijaona tatizo tatizo ni kutokutoa taarifa kwa wateja

Je ungekuwa umezidiwa usiku na huna pesa unategemea kadi ingekuwaje? Na hosp zetu hiz huna pesa/bima hakuna matibabu

Wamekosea sana tena sana maana wangesema pamema ungekuta ushajipanga kivingine kabisa
 
Mfuko wa afya wa bima ya afya wameleta mabadiliko ambayo wengi hatukutarajia, sijajua shida ni uchumi kuwa mbaya au sababu ni nini haswa.

leo nimetoka hospitali kutibiwa nikatoa kadi yangu mapokezi kama kawaida wakati nasubiri kuitwa kama ilivyo ada,nikaitwa nikaambiwa kadi yako ya bima imekataliwa nikauliza sababu sikupewa nikatoka hapo chapu nikaenda hospitali nyingine kubwa tu wanayotumia bima, basi nikatoa kadi kama kawaida wakati nasubiri kuitwa muda ukafika nikaitwa nikaambiwa kuwa kadi yangu ya bima imekuwa rejected nikauliza kivip nikaambiwa niende hapo zilipo ofisi za bima vile sio mbali nikaulize sababu.

dakika saba tayari nipo ofisi za Bima nikauliza mbona imekuwa hivi hospitali nilikotoka wakaniuliza Bima yangu nani alikata nikamtajia ni mlezi wangu, wakasema utaratibu umebadilika siku hizi anaetakiwa kukukatia ni mzazi pekee, nikamwambia mlezi mwenyewe alikuwa hana mtoto hata mmoja na mimi ndie niliekuwa kama mtoto wake wakanijibu hiyo haijalishi.

la pili wanadai pale mtu anapostaafu basi wale wategemezi wake hawana chao tena ,yani ukomo wa matumizi ya bima ndo unafikia hapo.

sasa nauliza huu utaratibu wa aina hii unalenga kumnufaisha nani?
yani kila sehemu pamebanwa hamna hata pa kukimbilia kwa sasa.

alichosema mzee watu wataishi kama masheatani nimeamini.
Pole sana,bado tunajenga viwoondoooo,ila bima ni wakatili sana piga moyo kondo,piga kazi
 
Usihangaike na ma bima, ukiugua waite shilawadu waki report kipindi we andaa tenga la pesa kutoka ikulu, mwenzako Wastara alipata milioni 37, anaumwa mguu na alipelekwa india.
Acheni kung'ang'ana na mikadi ya bima na kulalamika, jiongeze mkuu anakesha shilawadu hao ndio mpango mzima.
Ukiumwa kichwa, koo linawasha wajulishe SHILAWADU.
 
Usihangaike na ma bima, ukiugua waite shilawadu waki report kipindi we andaa tenga la pesa kutoka ikulu, mwenzako Wastara alipata milioni 37, anaumwa mguu na alipelekwa india.
Acheni kung'ang'ana na mikadi ya bima na kulalamika, jiongeze mkuu anakesha shilawadu hao ndio mpango mzima.
Ukiumwa kichwa, koo linawasha wajulishe SHILAWADU.
Mbona yule wa tyu tyu tyu Kule Dodoma hawamlipii matibabu
 
walichofanya ni kusitisha bima ambazo hazina wachangiaji. mlezi akishastaafu nani anailipia hiyo bima? ni wazi kwamba itakuwa ilikuwa inatumika buree. kwa maneno mengine ni kwamba wameamua kutoa huduma kwa kadi zinazochangiwa tuu.
 
Dogo acha kulalamika sana,

Kwa sheria za NHIF
Dependant ni watoto wako wa kuzaa,


Hizi sheria hufanyiwa mabadiliko kunapokuwa na ulazima,


NHIF wameweka utaratibu mzuri kuwa
Wastáafu,

mzee akistáafu atapewa bima yake special ya kustáafu yeye na mke wake !

Nitajie bima gani ingine inatoa kadi za matibabu kwa watumishi wao walio stáafu kazi
AAR
Jubilee
Strategis
Momentum
Etc
 
Ukweli hii haiko sawa kabisa kwa kuwa kama mtu ameajiriwa na kwa mujibu wa sheria anatibiwa yeye na Spouse plus dependents wanne ni vema wafuate hiyo regardless of whether ni neucleous family na wazazi miaka 60 plus. Unaweza ukawa na watoto wa ndugu au ndugu ambaye hana uwezo na ninategemea bima yangu imhudumie yeye. Mbaya zaidi hakuna taarifa kabisa kwa watumishi wanaolipia bima hizi. Paazeni sauti wahusika ili ukweli uwekwe wazi.
 
Back
Top Bottom