Usinifokee
JF-Expert Member
- Aug 10, 2015
- 2,502
- 3,522
Ukweli ni kwamba wanaokuwa i/c wanaelewa linapokuja suala la wao kwenda kuchukua statement ya malipo huko kwa wahusika....Nikiwa field hospital eneo fulani niliwahi ambiwa mama mjamzito akija clinic uliangalia tumbo hataridhika kabisa hata kama ujauzito una miezi miwili atataka tu umsikilize mtoto ivoivo ndo ataenda nyumbani na furaha.
The same kwako mtoa mada,
1. Issue ya kupimwa kipimo inaendana na level ya kituo, umeenda dispensary au kituo cha afya na maelezo yako yanakiashiria cha U.T.I kwanini usipimwe mkojo? Upo na bima ya afya kwanini usiende hospital kubwa ambapo kama unataka utapimwa kipimo cha damu, mkojo, haja kubwa etc?
Hilo la wewe kutaka kupimwa kitu ambacho hakina viashiria kiuhalisia ni kumfundisha daktari kazi hata nikiwa mimi sitakubali.
2. Vyumba vya daktari ni kweli unakuta mpaka saba ila madaktari waliopo ni watatu halafu mmoja amepata emergency, mwingine anahudumia waliopo wodini na mmoja akawepo pale kwenye chumba kimojawapo. Ni kweli hao wengine waache kuhudumia waliopo wodini wakuhudumie wewe tu?
Kama unabima ni vizuri ukaenda hospital kubwa kama unaweza hayo makasiriko yatapungua mkuu.
Unakutana na hii kitu inaitwa OVER UTILISATION OF INVESTIGATION and DRUGS kisha unakuta wamekupiga 345k ndio utaelewa ni kwanini baadhi ya Taasisi zinatoa vipimo tu kwa dalili husika na siyo anachokiamua mteja