Bima ya Afya Hospitalini ni kero

Bima ya Afya Hospitalini ni kero

hata mimi

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2017
Posts
1,356
Reaction score
1,448
Yaani mtu unajieleza weee halafu daktari anakwambia nenda maabara ukifika eti unapimwa malaria.

Daktari ukimwambia akupime na vitu fulani fulani anakataa tena mwingine anaona kama unamfundisha kazi. Yaani mtu kuandika tu ukapimwe kitu fulani anaona kama anafanya kazi ya mkwe!

Dawa kila siku ni amoxicillin piriton alu na paracetamol ndizo zilizopo. Dawa nyingi unaambiwa ukanunue

Halafu kuna kero nyingine nayo ngoja niiweke humu...
Zamani ukienda hospital fasta tu ila saivi utasotea hapo nje ukisubiri eti wamalize usafi

Usafi ukiisha wanaanza kupanga ofisi zao unakuta karibu lisaa eti wanaandaa. Mapokezi hapo foleni yake ya kufa raia na pale huwa hawana hiyana akianza kaanza

Ukitoka mapokezi unaambiwa nenda kwa daktari huko kwa daktari ndo utalia sasa. Kwanza chumba chenye uhakika wa kuwepo daktari unakuta ni kimoja tu wakati kuna milango karibu saba na yote imeandikwa chumba cha daktari.

Basi mnafika mnajazana hapo kwenye chumba cha daktari na si ajabu hayupo mpaka anakuja kuwasikiliza ni lisaa lingine mbele. Mkitoka ngwe hiyo mnakwenda kupigishwa mark time maabara nako tena

Maabara ndo kabisa kama una moyo wa hasira hutadumu yaani. Kwanza mpaka ashike hizo document zenu ni kipengele na Jamaa kisha anachukua makaratasi yenu yote anaita mmoja mmoja anawatoboa vidole na kuwapa vichupa (malaria na mkojo ndo vipimo maarufu utakavyopimwa ukifika maabara)

Ngoma majibu sasa badala atoe kwa kadiri anavyowapima eti anasubiri karibu awamalize wote ndipo utasikia akiwapa majibu mrudishe kwa daktari

Maana yake mwendapanga foleni upya kwa daktari tena. Mkitoka hapo mnaenda kupigishwa foleni kwenye dawa napo

Siku moja nimeenda Ruangwa Hospital aisee asubuhi sana nikakaa pale nje usafi wakaja kumaliza saa saa 2:30 okay tumejipanga kwenye mabenchi wakaanza kuweka vitu hapo kama haikuchukua saa na nusu sijui tukavumilia

Wameanza huduma tena wagonjwa kwenda kwenye milango ya madaktari hakuna dokta hata mmoja nakumbuka alikuja daktari mmoja kwenye kama saa nne hivi ndo akaanza kuhudumia.

Kwenda maabara nakumbuka tukamkuta mdada wa usafi anafanya usafi tulikaa pale nje kama wehu mara jamaa anavuka mara anarudi baadae ndo akaja kuchukua makaratasi hayo akapima watu weee wakaisha waliokwepo pale

Basi tulikaa pale aisee mpaka unawaonea huruma wale wagonjwa waliozidiwa. Jamaa kaja kuwapa majibu sijui saa saba halafu ndo foleni kwa daktari tena halafu foleni zinakuwa mbili sasa ya wapya wanaoingià kwa daktari na wanaorudisha majibu yaani balaa tupu

Tuache yote hayo narudi kwenye topic yangu ni kwamba TUKIONDOA VIHOMA VIDOGOVIDOGO HIVI VYA KAWAIDA NA KULAZWA- BILI YA KITANDA, UKIONDOA HIVYO VITU VIWILI BIMA YA AFYA HOSPITALINI (ZAHANATI, KITUO CHA AFYA NA HOSPITAL) HAINA MSAADA WOWOTE NI UJINGA TU
 
Nyie ndio nilikuwa nawatafuta....

Hivi ni nani alowaambia hizo bima ni kwaajili ya kufanya unalolitaka?

Nafikiri zimewekwa kwaajili ya matibabu siyo kwaajili ya kingine tofauti na matibabu....

Dr. Ndiye atakayetoa ruhusa au ku initiate kipimo ila siyo wewe ndio hivyo boss....

Vumilia tu

BIMA zinafuata muongozo wa kimatibabu STG na siyo hisia na miemko yako....

Usitoe lawama, ila waambieni na waombeni waiboreshe
 
Huduma ya Hospital ya Ruangwa uliyoenda zikiwa sawa kwa ubora na Hospital ya Aghakhan iliyopo pemben ya Ikulu Dar es salaam basi ujue thamani ya fedha imeisha


Tafuta pesa uepukane na hizo adha

kesho utalalamika mwanao kachaniwa suruali na Mwalimu wa nidhamu wa Kasimu Majaliwa secondary school kisa kashona 'modo' wakati wenzie Feza Mtoto anaingia na Modo shule na Afro Afro kichwani lakin Fresh tu

Kesho kutwa utalalamika Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa kakuweka 'lockup ' kisa hujachangia mchango wa Ulinzi shirikishi wakati tofauti ya maneno Mchango na tozo moja ni hiyari na nyingine lazima

lakin wenzio wa Masaki Hakuna mchango wa ulinzi shirikishi na defender za Polisi zinapiga patrol daily japo wote mnachangia kwa mwezi buku ya kodi ya Majengo kwny Luku

Mchawi pesa tu kama vipi apatikane Mganga wa kuipa Limbwata
 
Nyie ndio nilikuwa nawatafuta....

Hivi ni nani alowaambia hizo bima ni kwaajili ya kufanya unalolitaka?

Nafikiri zimewekwa kwaajili ya matibabu siyo kwaajili ya kingine tofauti na matibabu....

Dr. Ndiye atakayetoa ruhusa au ku initiate kipimo ila siyo wewe ndio hivyo boss....

Vumilia tu

BIMA zinafuata muongozo wa kimatibabu STG na siyo hisia na miemko yako....

Usitoe lawama, ila waambieni na waombeni waiboreshe
Wewe ni daktari ndomaana ulikuwa unatutafuta. Haya sasa umeshanipata? So what?
 
Yaani mtu unajieleza weee halafu daktari anakwambia nenda maabara ukifika eti unapimwa malaria

Daktari ukimwambia akupime na vitu fulani fulani anakataa tena mwingine anaona kama unamfundisha kazi. Yaani mtu kuandika tu ukapimwe kitu fulani anaona kama anafanya kazi ya mkwe!

Dawa kila siku ni amoxicillin piriton alu na paracetamol ndizo zilizopo. Dawa nyingi unaambiwa ukanunue

Halafu kuna kero nyingine nayo ngoja niiweke humu...
Zamani ukienda hospital fasta tu ila saivi utasotea hapo nje ukisubiri eti wamalize usafi

Usafi ukiisha wanaanza kupanga ofisi zao unakuta karibu lisaa eti wanaandaa. Mapokezi hapo foleni yake ya kufa raia na pale huwa hawana hiyana akianza kaanza

Ukitoka mapokezi unaambiwa nenda kwa daktari huko kwa daktari ndo utalia sasa. Kwanza chumba chenye uhakika wa kuwepo daktari unakuta ni kimoja tu wakati kuna milango karibu saba na yote imeandikwa chumba cha daktari.

Basi mnafika mnajazana hapo kwenye chumba cha daktari na si ajabu hayupo mpaka anakuja kuwasikiliza ni lisaa lingine mbele. Mkitoka ngwe hiyo mnakwenda kupigishwa mark time maabara nako tena

Maabara ndo kabisa kama una moyo wa hasira hutadumu yaani. Kwanza mpaka ashike hizo document zenu ni kipengele na Jamaa kisha anachukua makaratasi yenu yote anaita mmoja mmoja anawatoboa vidole na kuwapa vichupa (malaria na mkojo ndo vipimo maarufu utakavyopimwa ukifika maabara)

Ngoma majibu sasa badala atoe kwa kadiri anavyowapima eti anasubiri karibu awamalize wote ndipo utasikia akiwapa majibu mrudishe kwa daktari

Maana yake mwendapanga foleni upya kwa daktari tena. Mkitoka hapo mnaenda kupigishwa foleni kwenye dawa napo

Siku moja nimeenda Ruangwa Hospital aisee asubuhi sana nikakaa pale nje usafi wakaja kumaliza saa saa 2:30 okay tumejipanga kwenye mabenchi wakaanza kuweka vitu hapo kama haikuchukua saa na nusu sijui tukavumilia

Wameanza huduma tena wagonjwa kwenda kwenye milango ya madaktari hakuna dokta hata mmoja nakumbuka alikuja daktari mmoja kwenye kama saa nne hivi ndo akaanza kuhudumia.

Kwenda maabara nakumbuka tukamkuta mdada wa usafi anafanya usafi tulikaa pale nje kama wehu mara jamaa anavuka mara anarudi baadae ndo akaja kuchukua makaratasi hayo akapima watu weee wakaisha waliokwepo pale

Basi tulikaa pale aisee mpaka unawaonea huruma wale wagonjwa waliozidiwa. Jamaa kaja kuwapa majibu sijui saa saba halafu ndo foleni kwa daktari tena halafu foleni zinakuwa mbili sasa ya wapya wanaoingià kwa daktari na wanaorudisha majibu yaani balaa tupu

Tuache yote hayo narudi kwenye topic yangu ni kwamba TUKIONDOA VIHOMA VIDOGOVIDOGO HIVI VYA KAWAIDA NA KULAZWA- BILI YA KITANDA, UKIONDOA HIVYO VITU VIWILI BIMA YA AFYA HOSPITALINI (ZAHANATI, KITUO CHA AFYA NA HOSPITAL) HAINA MSAADA WOWOTE NI UJINGA TU
Daktari hapangiwi...ungejua ugonjwa unaokusumbua ungeenda kununua dawa na sio hospitali...kuhusu usafi ulitaka kutibiwa eneo ambalo ni chafu si ndo ungesema zaidi,kila sehemu ina utaratibu wake ,kama unataka fast track tafuta hela.....
 
Mkuu kwa maelezo yako inaonekana unaenda kupata huduma Dispensary. Ukitaka huduma bora jitahidi uwe unafika kwenye Hospitali kubwa kwa mfano kwa wakazi wa Dsm unaweza kwenda kupata huduma sehemu kama Hospitali ya Kairuki. Hizo Dispensary hazina mamlaka ya kuandika dawa kubwa kwenye Bima kutokana na kuhesabika ni ngazi ya chini, ila hizo Hospital kubwa zinaruhusiwa kufanya hivyo.

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu kwa maelezo yako inaonekana unaenda kupata huduma Dispensary. Ukitaka huduma bora jitahidi uwe unafika kwenye Hospitali kubwa kwa mfano kwa wakazi wa Dsm unaweza kwenda kupata huduma sehemu kama Hospitali ya Kairuki. Hizo Dispensary hazina mamlaka ya kuandika dawa kubwa kwenye Bima kutokana na kuhesabika ni ngazi ya chini, ila hizo Hospital kubwa zinaruhusiwa kufanya hivyo.

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
Mwenyewe nnashangaa sn mtu ana bima ya afya inamruhusu kwenda hata tmj hospital unamkuta police barracks hospital kapanga foleni
 
Nyie ndio nilikuwa nawatafuta....

Hivi ni nani alowaambia hizo bima ni kwaajili ya kufanya unalolitaka?

Nafikiri zimewekwa kwaajili ya matibabu siyo kwaajili ya kingine tofauti na matibabu....

Dr. Ndiye atakayetoa ruhusa au ku initiate kipimo ila siyo wewe ndio hivyo boss....

Vumilia tu

BIMA zinafuata muongozo wa kimatibabu STG na siyo hisia na miemko yako....

Usitoe lawama, ila waambieni na waombeni waiboreshe
Sio uliokuwa unatutafuta mkuu, Madaktari mnazingua sana, ukienda na Bima unapimwa kipimo cha malaria kisha unaandikiwa mseto!

Nusu nife, eti nina malaria, kumbe mchafuko wa damu na sumu! Nilirejea hospitali hapo kwa mara nyingine na huyo huyo dokta aliyethibitisha malaria ndo aliyenipima akakuta nina mchafuko wa damu na sumu kwenye mishipa baada ya kwenda na 50k mkononi!

Hospitali pekee inayohudumia wagonjwa wenye BIMA ni Hospitali ya Taifa ya Muhimbili! tena NHIF pekee!

Suluhisho ni katiba mpya!
 
Nadhani BIMA inaweza kuwa na changamoto huko kwenye baadhi ya hospitali za Serikali. Mie huwa natibiwa Kairuki hospital kwa BIMA na sijawahi kupatwa shida yoyote.

Sehemu nyingine ambako nimewahi kupata huduma kwa BIMA bila shida ni Regency, Agakhan Polyclinics na BESTA Polyclinic pale Kinondoni.

Sasa huenda hospitali za Serikali ndio changamoto iliko maana nina miaka mingi sijaenda hosp ya serikali kwa kweli.

Na huwa natumia BIMA ya kawaida tu (NHIF) wala sio private insurance kama Jubilee na ndugu zake.


Labda tuseme unatumia BIMA gani? Maana hata kama unatumia NHIF ile ya kifurushi cha chini zaidi bado unatakiwa upate huduma ambazo nadhani hizi shida za kawaida kawaida ina cover vizuri tu. Tatizo itakuwa ni watoa huduma na siyo BIMA yenyewe.

Zamani shida ilikuwa upande wa BIMA wenyewe maana walikuwa hawalipi pesa hosp husika kwa wakati ila naona kama hii changamoto siku hizi siisikii kabisa. Huenda ipo ila mie sijaisikia kwa sasa kama enzi za nyuma.

Pamoja na hayo, nakubali kuwa baadhi ya watumishi wa afya wanafanya kazi kwa mazoea sana na mioyo yao imejaa viburi na chuki. Na siyo wa afya tu nadhani wafanyakazi wengi wa umma bado wanatoa huduma hafifu na imekuwa ni kero kubwa kwa wanachi. Kwahiyo nyinyi watumishi wa umma hebu jirekebisheni basi mtoe huduma kwa weledi na upendo.

Nimegusia hili maana nimeona nchi za wenzetu wanavyofanya kazi ukilinganisha na sisi utajua kweli bado tuna safari ndefu sana. Japo serikali nayo inachangia kwa kulipa maslahi duni na mifumo isiyokuwa rafiki ila bado individual accountability ni changamoto kwa watumishi walio wengi.
 
Yaani mtu unajieleza weee halafu daktari anakwambia nenda maabara ukifika eti unapimwa malaria

Daktari ukimwambia akupime na vitu fulani fulani anakataa tena mwingine anaona kama unamfundisha kazi. Yaani mtu kuandika tu ukapimwe kitu fulani anaona kama anafanya kazi ya mkwe!

Dawa kila siku ni amoxicillin piriton alu na paracetamol ndizo zilizopo. Dawa nyingi unaambiwa ukanunue

Halafu kuna kero nyingine nayo ngoja niiweke humu...
Zamani ukienda hospital fasta tu ila saivi utasotea hapo nje ukisubiri eti wamalize usafi

Usafi ukiisha wanaanza kupanga ofisi zao unakuta karibu lisaa eti wanaandaa. Mapokezi hapo foleni yake ya kufa raia na pale huwa hawana hiyana akianza kaanza

Ukitoka mapokezi unaambiwa nenda kwa daktari huko kwa daktari ndo utalia sasa. Kwanza chumba chenye uhakika wa kuwepo daktari unakuta ni kimoja tu wakati kuna milango karibu saba na yote imeandikwa chumba cha daktari.

Basi mnafika mnajazana hapo kwenye chumba cha daktari na si ajabu hayupo mpaka anakuja kuwasikiliza ni lisaa lingine mbele. Mkitoka ngwe hiyo mnakwenda kupigishwa mark time maabara nako tena

Maabara ndo kabisa kama una moyo wa hasira hutadumu yaani. Kwanza mpaka ashike hizo document zenu ni kipengele na Jamaa kisha anachukua makaratasi yenu yote anaita mmoja mmoja anawatoboa vidole na kuwapa vichupa (malaria na mkojo ndo vipimo maarufu utakavyopimwa ukifika maabara)

Ngoma majibu sasa badala atoe kwa kadiri anavyowapima eti anasubiri karibu awamalize wote ndipo utasikia akiwapa majibu mrudishe kwa daktari

Maana yake mwendapanga foleni upya kwa daktari tena. Mkitoka hapo mnaenda kupigishwa foleni kwenye dawa napo

Siku moja nimeenda Ruangwa Hospital aisee asubuhi sana nikakaa pale nje usafi wakaja kumaliza saa saa 2:30 okay tumejipanga kwenye mabenchi wakaanza kuweka vitu hapo kama haikuchukua saa na nusu sijui tukavumilia

Wameanza huduma tena wagonjwa kwenda kwenye milango ya madaktari hakuna dokta hata mmoja nakumbuka alikuja daktari mmoja kwenye kama saa nne hivi ndo akaanza kuhudumia.

Kwenda maabara nakumbuka tukamkuta mdada wa usafi anafanya usafi tulikaa pale nje kama wehu mara jamaa anavuka mara anarudi baadae ndo akaja kuchukua makaratasi hayo akapima watu weee wakaisha waliokwepo pale

Basi tulikaa pale aisee mpaka unawaonea huruma wale wagonjwa waliozidiwa. Jamaa kaja kuwapa majibu sijui saa saba halafu ndo foleni kwa daktari tena halafu foleni zinakuwa mbili sasa ya wapya wanaoingià kwa daktari na wanaorudisha majibu yaani balaa tupu

Tuache yote hayo narudi kwenye topic yangu ni kwamba TUKIONDOA VIHOMA VIDOGOVIDOGO HIVI VYA KAWAIDA NA KULAZWA- BILI YA KITANDA, UKIONDOA HIVYO VITU VIWILI BIMA YA AFYA HOSPITALINI (ZAHANATI, KITUO CHA AFYA NA HOSPITAL) HAINA MSAADA WOWOTE NI UJINGA TU
Bora hay uliyoyasema mkuu, vituo vingine vya afya vya ksta havina nyumba za watumishi ilawalazimu kufunga kituo na kwenda kulala mjini, havina maji wala umeme uko kilometa 2, watumishi waliko ni wawili. Vimejengwa kiasasa kabisa karibu na shamba la diwani
 
Yaani mtu unajieleza weee halafu daktari anakwambia nenda maabara ukifika eti unapimwa malaria

Daktari ukimwambia akupime na vitu fulani fulani anakataa tena mwingine anaona kama unamfundisha kazi. Yaani mtu kuandika tu ukapimwe kitu fulani anaona kama anafanya kazi ya mkwe!

Dawa kila siku ni amoxicillin piriton alu na paracetamol ndizo zilizopo. Dawa nyingi unaambiwa ukanunue

Halafu kuna kero nyingine nayo ngoja niiweke humu...
Zamani ukienda hospital fasta tu ila saivi utasotea hapo nje ukisubiri eti wamalize usafi

Usafi ukiisha wanaanza kupanga ofisi zao unakuta karibu lisaa eti wanaandaa. Mapokezi hapo foleni yake ya kufa raia na pale huwa hawana hiyana akianza kaanza

Ukitoka mapokezi unaambiwa nenda kwa daktari huko kwa daktari ndo utalia sasa. Kwanza chumba chenye uhakika wa kuwepo daktari unakuta ni kimoja tu wakati kuna milango karibu saba na yote imeandikwa chumba cha daktari.

Basi mnafika mnajazana hapo kwenye chumba cha daktari na si ajabu hayupo mpaka anakuja kuwasikiliza ni lisaa lingine mbele. Mkitoka ngwe hiyo mnakwenda kupigishwa mark time maabara nako tena

Maabara ndo kabisa kama una moyo wa hasira hutadumu yaani. Kwanza mpaka ashike hizo document zenu ni kipengele na Jamaa kisha anachukua makaratasi yenu yote anaita mmoja mmoja anawatoboa vidole na kuwapa vichupa (malaria na mkojo ndo vipimo maarufu utakavyopimwa ukifika maabara)

Ngoma majibu sasa badala atoe kwa kadiri anavyowapima eti anasubiri karibu awamalize wote ndipo utasikia akiwapa majibu mrudishe kwa daktari

Maana yake mwendapanga foleni upya kwa daktari tena. Mkitoka hapo mnaenda kupigishwa foleni kwenye dawa napo

Siku moja nimeenda Ruangwa Hospital aisee asubuhi sana nikakaa pale nje usafi wakaja kumaliza saa saa 2:30 okay tumejipanga kwenye mabenchi wakaanza kuweka vitu hapo kama haikuchukua saa na nusu sijui tukavumilia

Wameanza huduma tena wagonjwa kwenda kwenye milango ya madaktari hakuna dokta hata mmoja nakumbuka alikuja daktari mmoja kwenye kama saa nne hivi ndo akaanza kuhudumia.

Kwenda maabara nakumbuka tukamkuta mdada wa usafi anafanya usafi tulikaa pale nje kama wehu mara jamaa anavuka mara anarudi baadae ndo akaja kuchukua makaratasi hayo akapima watu weee wakaisha waliokwepo pale

Basi tulikaa pale aisee mpaka unawaonea huruma wale wagonjwa waliozidiwa. Jamaa kaja kuwapa majibu sijui saa saba halafu ndo foleni kwa daktari tena halafu foleni zinakuwa mbili sasa ya wapya wanaoingià kwa daktari na wanaorudisha majibu yaani balaa tupu

Tuache yote hayo narudi kwenye topic yangu ni kwamba TUKIONDOA VIHOMA VIDOGOVIDOGO HIVI VYA KAWAIDA NA KULAZWA- BILI YA KITANDA, UKIONDOA HIVYO VITU VIWILI BIMA YA AFYA HOSPITALINI (ZAHANATI, KITUO CHA AFYA NA HOSPITAL) HAINA MSAADA WOWOTE NI UJINGA TU

Pole sana,

Nini kifanyike na katika ngazi gani ya mfumo wa afya vimepangwa kulingana na mwongozo wa wizara yetu ya afya:

Hii ni kulingana na:

1: Uwezo wa watoa huduma/qualification katika ngazi husika

2: Uwezo wa maabara husika katika ngazi iliyopo.

3: Uwezo wa pharmacy iliyopo katika kituo cha afya husika.

4: Mchakato wa nini kifanyike kwa mgonjwa husika, huzingatia maongezi kati yako na mtoa huduma na ukaguzi/physical examination aliofanya na kupata mwelekeo wa tatizo.

Si kosa kutoa maoni yako ni nini ungependa upime, ila utahitaji kutetra hicho kipimo ni kwa nini unahitaji kukifanya na kama kina matokeo chanya kulingana na shida zako za kiafya kwa wakati husika au daktari atakueleza kama hakina uzito au umuhimu na au hakifanyiki kwenye kituo husika.

Mengine uliyoeleza, ni matatizo ya mfumo wa kiutendaji kwa hospitali husika kama tu muda wa kufanya usafi unaingilia mpaka wakati wa kuanza kazi. Ni vyema kujirekebisha.

Kulingana na mfumo wa afya ulivyokuwa, kuna vituo vya afya vinafanyakazi zaidi ya uwezo viliopewa kimfumo. Mfano: kuna operationzs, vipimo au procedures kufanyika kwenye vituo visivyo na uwezo kiutaratibu

NB: Bima ya afya hasa NHIF inajikita kwenye kusisitiza taratibu hazo hapo juu. Kama mgonjwa anahitaji husuma zaidi ni vyema kwenda ngazi ya juu ya mfumo wa afya.
 
Huduma ya Hospital ya Ruangwa uliyoenda zikiwa sawa kwa ubora na Hospital ya Aghakhan iliyopo pemben ya Ikulu Dar es salaam basi ujue thamani ya fedha imeisha


Tafuta pesa uepukane na hizo adha

kesho utalalamika mwanao kachaniwa suruali na Mwalimu wa nidhamu wa Kasimu Majaliwa secondary school kisa kashona 'modo' wakati wenzie Feza Mtoto anaingia na Modo shule na Afro Afro kichwani lakin Fresh tu

Kesho kutwa utalalamika Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa kakuweka 'lockup ' kisa hujachangia mchango wa Ulinzi shirikishi wakati tofauti ya maneno Mchango na tozo moja ni hiyari na nyingine lazima

lakin wenzio wa Masaki Hakuna mchango wa ulinzi shirikishi na defender za Polisi zinapiga patrol daily japo wote mnachangia kwa mwezi buku ya kodi ya Majengo kwny Luku

Mchawi pesa tu kama vipi apatikane Mganga wa kuipa Limbwata
Aisee
 
Sio uliokuwa unatutafuta mkuu, Madaktari mnazingua sana, ukienda na Bima unapimwa kipimo cha malaria kisha unaandikiwa mseto!

Nusu nife, eti nina malaria, kumbe mchafuko wa damu na sumu! Nilirejea hospitali hapo kwa mara nyingine na huyo huyo dokta aliyethibitisha malaria ndo aliyenipima akakuta nina mchafuko wa damu na sumu kwenye mishipa baada ya kwenda na 50k mkononi!

Hospitali pekee inayohudumia wagonjwa wenye BIMA ni Hospitali ya Taifa ya Muhimbili! tena NHIF pekee!

Suluhisho ni katiba mpya!
Narudia BIMA zinafuata muongozo wa kimatibabu STG....

Unakutana na Mteja anakuambia nimekuja kwenye matibabu lakini features alizonazo ni za allergic rhinitis (Mafua) mfano lakini anakupangia vipimo....

Badala asikilize ungependa umfanyie nini au ufanye nini.... Yeye anataka apime choo, mkojo, ESR, Full blood Picture, B/S na MRDT

Hivi vituo hamta vifunga nyie?

Nafikiri kuna haja hasa wenye makampuni ya BIMA kutoa ELIMU kwa wanufaika na kuwaelewesha kuwa anaye initiate kipimo ni Dr. siyo mteja....

La mwisho, Taasisi husika (BIMA) isitizame kupata faida ila inatakiwa kutoa huduma.... Nilishangaa kipindi cha mwendazake eti BIMA inatoa gawio la faida kwa sirikali [emoji22][emoji22][emoji22][emoji22]

Hili ni tatizo

Msitulaumu jamani, tunafuata miongozo ya kimatibabu
 
Narudia BIMA zinafuata muongozo wa kimatibabu STG....

Unakutana na Mteja anakuambia nimekuja kwenye matibabu lakini features alizonazo ni za allergic rhinitis (Mafua) mfano lakini anakupangia vipimo....

Badala asikilize ungependa umfanyie nini au ufanye nini.... Yeye anataka apime choo, mkojo, ESR, Full blood Picture, B/S na MRDT

Hivi vituo hamta vifunga nyie?

Nafikiri kuna haja hasa wenye makampuni ya BIMA kutoa ELIMU kwa wanufaika na kuwaelewesha kuwa anaye initiate kipimo ni Dr. siyo mteja....

La mwisho, Taasisi husika (BIMA) isitizame kupata faida ila inatakiwa kutoa huduma.... Nilishangaa kipindi cha mwendazake eti BIMA inatoa gawio la faida kwa sirikali [emoji22][emoji22][emoji22][emoji22]

Hili ni tatizo

Msitulaumu jamani, tunafuata miongozo ya kimatibabu
Si bure, hapa kuna CCM oye!
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nikiwa field hospital eneo fulani niliwahi ambiwa mama mjamzito akija clinic uliangalia tumbo hataridhika kabisa hata kama ujauzito una miezi miwili atataka tu umsikilize mtoto ivoivo ndo ataenda nyumbani na furaha.

The same kwako mtoa mada,
1. Issue ya kupimwa kipimo inaendana na level ya kituo, umeenda dispensary au kituo cha afya na maelezo yako yanakiashiria cha U.T.I kwanini usipimwe mkojo? Upo na bima ya afya kwanini usiende hospital kubwa ambapo kama unataka utapimwa kipimo cha damu, mkojo, haja kubwa etc?
Hilo la wewe kutaka kupimwa kitu ambacho hakina viashiria kiuhalisia ni kumfundisha daktari kazi hata nikiwa mimi sitakubali.

2. Vyumba vya daktari ni kweli unakuta mpaka saba ila madaktari waliopo ni watatu halafu mmoja amepata emergency, mwingine anahudumia waliopo wodini na mmoja akawepo pale kwenye chumba kimojawapo. Ni kweli hao wengine waache kuhudumia waliopo wodini wakuhudumie wewe tu?

Kama unabima ni vizuri ukaenda hospital kubwa kama unaweza hayo makasiriko yatapungua mkuu.
 
Back
Top Bottom