Bima ya Afya hili halijakaa vizuri kabisa

Bima ya Afya hili halijakaa vizuri kabisa

samakinchanga

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2014
Posts
2,024
Reaction score
1,237
Watumishi wanakatwa mishahara na kujiunga na Bima ya Afya lakini sasa wanaweka masharti kwamba wategemezi kama watoto wako mwisho miaka 18 kama hasomi basi hapati Huduma,hii si sawa vijana wanamaliza wanakosa ajira na wakati huo wazazi wanaendelea kukatwa mshahara mpaka kustaafu miaka 60.hebu rekebisheni hili.
Wadau wengine changieni.
 
Binafsi nilikwenda ofisi yao ya wilaya fulani kutaka ufafanuzi lakini meneja wake alishindwa kutoa majibu na kudai niende makao makuu ndiko kwenye majibu.
Huyu anayekaimu nafasi ya mkurugenzi mkuu ndiye mwenye kuleta hoja hii ya kuwaondoa watoto wetu kwenye huduma kwa madai wajiunge na bima nyinginezo kwani umri wao ulishapita.
Swali kwa bima ya afya:-
mimi ndiye mchangiaji, kwanini mnaniingilia uhuru wangu wa kuwachagua ninaotaka wanufaike na michango yangu? Ina maana sina uhuru na michango yangu? Kwanini hamjatushirikisha wadau? Acheni ubabe kwenye pesa zetu! Natamani kuwepo na vikao vya kutushirikisha wadau kabla hamjaanza kutekekeleza mnachofikiria.
Hivi kwanini hakuna vikao na wanachama wenu? Nataka kujua mapato na matumizi ya fedha zangu ati!
 
mimi niliambiwa katika bima kuna policy ambazo zinakua zimewekwa na bima husika.aaagh nilijibiwa vizuri sana na meneja wa bima kanda ya Ilala nikaelewa...
 
Hii bima ya Afya kimsingi ina ukiritimba mkubwa. Na kubwa kabisa ni kwa sababu wapo wenyewe, serikali ilitakiwa kuruhusu mfuko zaidi ya mmoja kama walivyofanya kwenye hifadhi ya jamii.
 
Si ajabu pesa yetu imepigwa sasa wanabana matumizi.
 
Bima ya Afya ni wezi kama wezi wengine, sijaona sababu ya wao kuweka masharti kwenye fedha ya mtu mwingine, wanatumia fedha zetu kufanya vikao na kujilipa posho kwenye mahotel makubwa, huku sisi wachangiaji tunapata huduma hafifu kwenye hospitali tunazoambiwa tukapate huduma, wananunua mashangingi ya bei mbaya wakati sisi tunakosa dawa hospitalini na hata baadhi ya waganga kututaka kutoa rushwa kwa kisingizio cha bima ya afya hailipii huduma hiyo, ukipiga simu kufuatilia haki yako unajibiwa siasa,

Binafsi sioni umuhimu wa kuwa na hawa bima ya afya maana wamekaa kiudalali zaidi kuliko huduma kwa raia, binafsi ningependekeza uanzishwe mfumo wa fedha zetu za michango kwenda kwenye account maalum ambayo itakuwa na smart card itakayo muwezesha client kuwasilisha card husika kwenye hospitali husika na malipo kutolewa moja kwa moja toka kwenye account na salio kubakia humo badala ya malipo kufanywa na wakala ambaye matumizi yake ni makubwa kuliko mchangiaji
 
Wanahaki ya kufanya lolote ila tunataka iwe hiari na kujiunga na hili dubwana
 
Si hivyo tuu wameingiza na mambo ya unyanyasaji wa kiimani kwa watu wa dini fulani na kuwapa masharti waliyoweka wao kinyume na serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania.

Ukiuliza makao makuu wameagiza kunyanyasa hii na mimi nimeipata baadhi ya mikoa.
 
Hii bima ya Afya kimsingi ina ukiritimba mkubwa. Na kubwa kabisa ni kwa sababu wapo wenyewe, serikali ilitakiwa kuruhusu mfuko zaidi ya mmoja kama walivyofanya kwenye hifadhi ya jamii.
Actually mifuko ya hifadhi ya jamii ingekuwa na jukumu pia ya kutoa matibabu. Hakuna haja ya kuwa na mifuko ya social security mingi. Inatakiwa uwe mwanachama wa mfuko mmoja na u take care all of your social security issues.
 
Sasa hivi wameamua kusajili upya wanachama wake na kuweka deadline ya usajili vinginevyo huduma itasitishwa. Ninachowaomba kama wakiamua kusitisha huduma kwa wanachama wao pia wasitishe makato wanayomkata mhusika vinginevyo itakua ni wizi,
 
Mkuu likasu umenena kweli.mbona watakaoumia ni wengi lakini wako kimyaa
 
Actually mifuko ya hifadhi ya jamii ingekuwa na jukumu pia ya kutoa matibabu. Hakuna haja ya kuwa na mifuko ya social security mingi. Inatakiwa uwe mwanachama wa mfuko mmoja na u take care all of your social security issues.

Kweli mkuu..
 
CAG chunguza Mfuko huu wa Bima ya afya(NHIF) kunaharufu mbaya,. Hivi hizi taaasisi zetu za Uchunguzi mbona zimelala?... Ukiona mahali panalalamikiwa ujue hapo lazima kuna tatizo, Chunguzeni.
 
Haya ..... 😎KABWE chambua hii mambo chaap
 
yaani ni uonevu wa hali ya juu pesa yangu halafu mnaeka masharti mnajua yule mdogo wangu mi ndo mama ake mlezi yani mimi nataka nionane na mkurugenzi maana kitendo cha kumtoa mzigo unarudi kwangua acheni hizo
 
unakatwa pesa rundo, ila ukiugua dawa wapata panadol na asprin tu!!!
wizi kweupeeeee!
 
Wanahaki ya kufanya lolote ila tunataka iwe hiari na kujiunga na hili dubwana

Kwa kweli nakuunga mkono kwa hapo. Mimi nakatwa mafedha mengi tu, watoto wamefikisha miaka 18 na zaidi, sasa ni vyema wanirudishie hela yangu nyengine. Au turuhusiwe na kujiunga na bima za afya nyengine kwani lazima hii tu?
 
unakatwa pesa rundo, ila ukiugua dawa wapata panadol na asprin tu!!!
wizi kweupeeeee!

Baadhi ya maeneo mikoa mbali mbali ilikewepo wilaya za mkoa wa lindi wenye kadi wanaumia tu na bado inawagharimu hakuna huduma
Ni kudhulumu tu na kunufaisha wachache kwa mbwembwe na matangazo (Show)lakini wengine hawapati huduma istahiki

Fuatilieni kwa wateja wenu na wategemezi mutapata majibu
 
Back
Top Bottom