Bill Gates kusaidia watu kufuga kuku Afrika

Pistol

Senior Member
Oct 13, 2015
194
86
160609134912_kuku_kienyeji_640x360_bbc_nocredit.jpg



Mwanzilishi wa kampuni ya Microsoft Bill Gates, amezindua kampeni ya kusaidia watu maskini zaidi barani Afrika, kusini mwa jangwa la sahara, kwa kufuga kuku.

Bilionea huyo Bill Gates anasema kuwa kufuga kuku kunaweza kuwa kifaa muhimu katika kukabiliana na ufukara hohe hahe.

Ameahidi kutoa kuku 100,000, na ukurasa katika mtandao wa mradi huo tayari umewavutia na kusambazwa kwa maelfu ya watu.

Umoja wa Mataifa unakisia kuwa asilimia 41 ya watu katika Bara la Afrika, Kusini mwa jangwa la Sahara wanaishi katika ufukara mkubwa.

Chanzo: BBC
 
View attachment 355363


Mwanzilishi wa kampuni ya Microsoft Bill Gates, amezindua kampeni ya kusaidia watu maskini zaidi barani Afrika, kusini mwa jangwa la sahara, kwa kufuga kuku.

Bilionea huyo Bill Gates anasema kuwa kufuga kuku kunaweza kuwa kifaa muhimu katika kukabiliana na ufukara hohe hahe.

Ameahidi kutoa kuku 100,000, na ukurasa katika mtandao wa mradi huo tayari umewavutia na kusambazwa kwa maelfu ya watu.

Umoja wa Mataifa unakisia kuwa asilimia 41 ya watu katika Bara la Afrika, Kusini mwa jangwa la Sahara wanaishi katika ufukara mkubwa.

Chanzo: BBC
Tatizo la ufugaji wa kuku hasa wa nyama 'broilers' ni kuruhusu wafugaji wauze kwa 'kichwa' badala ya uzito. Kwanini nyama zingine kama n'gombe, mbuzi, nguruwe, na samaki, huuzwa kwa kg.?
Na serikali inafuatilia bei za nyama mpaka ukaguzi wa mizani kwenye bucha. Halafu isiwe hivyo kwa kuku! Matokeo yake watu wanauza broiler vifaranga, tena wanaolishwa homoni za ajabu ili wakuwe haraka! Serikali haiwajali wafugaji wa broilers ndiyo sababu madalali wanapanga bei watakavyo. Serikali isipopiga marufuku uuzaji wa kuku kwa kichwa ufugaji wa broilers kama ilivyo sasa hautakuwa na tija kwa mfugaji na usalama wa afya za walaji utaendelea kuwa hatarini.
Huko nyuma wananchi wengi, hasa akinamama wa hali ya chini walifaidika na miradi ya kuku wa nyama na mayai. Na duniani kote nyama ya kuku ni chakula cha wananchi wa kawaida, lakini sio Tz.
Matumaini ya Bill Gates ya kuinua hali za wananchi masikini wa Africa kupitia ufugaji wa kuku yatakumbana na ugumu wa serikali kuweka mazingira wezeshi na kutozingatia na kondoa vikwazo vya aina hii kwa ufugaji wa kuku wa nyama.
 
sasa vipi tutanfikia Bill Get na kupata kujiunga na huo mradi?
 
daa naona kuku wetu wa kienyeji wakiharibiwa hivi hivi after ten yrs hawapo tena..
 
Binafsi nimestushwa na maneno haya ya mfanyabiashara huyu na tajiri mkubwa duniani.Bily Gate amesema kuku watano wanaweza wakakupatia faida ya 1000$ kwa mwaka.
Tafsiri yake ni kwamba kuku mmoja anakuzalishia 200$ kwa mwaka.
Kama hivi ndivyo inamaana kuku 100 watazalisha 20,000$ kwa mwaka ambazo ni sawa na takribani tsh 40,000,000/= kwa mwaka.
Sisi kama wa tz wapenda ufagaji kuna kikubwa chukujifunza hapo.
 
Binafsi nimestushwa na maneno haya ya mfanyabiashara huyu na tajiri mkubwa duniani.Bily Gate amesema kuku watano wanaweza wakakupatia faida ya 1000$ kwa mwaka.
Tafsiri yake ni kwamba kuku mmoja anakuzalishia 200$ kwa mwaka.
Kama hivi ndivyo inamaana kuku 100 watazalisha 20,000$ kwa mwaka ambazo ni sawa na takribani tsh 40,000,000/= kwa mwaka.
Sisi kama wa tz wapenda ufagaji kuna kikubwa chukujifunza hapo lakini pia kujiuliza kwanini sisi ni masikini?
Source BBC
 
View attachment 355363


Mwanzilishi wa kampuni ya Microsoft Bill Gates, amezindua kampeni ya kusaidia watu maskini zaidi barani Afrika, kusini mwa jangwa la sahara, kwa kufuga kuku.

Bilionea huyo Bill Gates anasema kuwa kufuga kuku kunaweza kuwa kifaa muhimu katika kukabiliana na ufukara hohe hahe.

Ameahidi kutoa kuku 100,000, na ukurasa katika mtandao wa mradi huo tayari umewavutia na kusambazwa kwa maelfu ya watu.

Umoja wa Mataifa unakisia kuwa asilimia 41 ya watu katika Bara la Afrika, Kusini mwa jangwa la Sahara wanaishi katika ufukara mkubwa.

Chanzo: BBC
sahel hakuna nafaka ya kuwatosha wanadam hivyo mradi wa kuku hautokuwa na manufaa
 
Hakuna kazi inayoweza kufanyika na kuleta tija bila wahusika kujishughulisha kupata maarifa ya kazi hiyo. Nashangaa wanaolalamika kuwa kuku anauzwa kwa kichwa. Mbona Mwanza kuna bucha zinauza kuku kwa kilo? Kwa mfugaji ndo wanauza kwa kichwa lakini kwa walaji wananunua kwa kilo. Hilo likizoeleka hata wanunuzi wa jumla wataanza kununua kwa kilo na sio kwa kichwa tena.
 
Back
Top Bottom