BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Date::3/11/2009
Bilionea Mo Ibrahim ataka Afrika iache kuombaomba
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi
Bilionea Mo Ibrahim ataka Afrika iache kuombaomba
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi
MFANYABIASHARA maarufu duniani Mo Ibrahim, amesema Afrika inapaswa kuongeza nguvu katika kuvutia wawekezaji badala ya kuomba misaada.
Kauli ya Mo ambaye ni mwanzilishi wa shindano la Tuzo ya Rais Bora barani Afrika, imekuja wakati sehemu kubwa ya nchi za Afrika zikiwa zinategemea misaada ya wafadhili.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mo alisema pamoja na nchi za Afrika kuhitaji msaada lakini bado zenyewe zinahitaji kuongeza nguvu na mikakati ya kujitegemea.
Kwa mujibu wa Mo, nguvu kubwa zinazotumiwa na Afrika katika kutafuta misaada nje, kama zingetumika kuvutia wawekezaji, ni dhahiri zingewezesha mafanikio makubwa.
"Afrika inapaswa kuongeza nguvu kwa ajili ya kujitegemea, inatumia nguvu nyingi kuomba misaada," alisema Mo na kuongeza:
"Ingeweza kupiga hatua kama ingetumia nguvu hizo katika kuvutia wawekezaji barani Afrika."
Akionyesha msisisitizo, alisema rasilimali nyingi za barani Afrika zinatosha kuliwezesha bara hilo kujijengea misingi ya kujitegemea.
Kwa mujibu wa Mo, Afrika inaweza kuomba misaada, lakini si kutegemea kwa sehemu kubwa.
Wakati huo huo, mkutano kati ya nchi za Afrika na IMF umemalizika jana kwa kutoa maazimio mbalimbali, ambayo ni pamoja na kuhakikisha nchi za Afrika zinaendelea kudumisha uhusiano na shirika hilo la fedha na nchi za Afrika kuendelea kutekeleza sera za IMF,
Azimio lingine ni nchi za Afrika na IMF kuangalia jinsi ya kufanya mabadiliko ya kimfumo katika kupata uwakilishi wa viongozi wa shirika hilo.
Mkutano huop ambao uliwashirikisha mawaziri na magavana wa benki kuu barani afrika pamoja na wahisani na IMF ulianza juzi wakizungumzia jinsi ya bara hili linavyoweza kukabiliana na msukosuko wa fedha duniani.
Kabla ya kuanza kwa mkuano huo, Mkuruegenzi Mkuu wa IMF, Dominique Struss-Kahn aliitaka tanzania kubuni njia za kujitegema kwa kutumia rasilimali zake na fursa zote za uwekezaji kwa kutengeneza mazingira mazuri yanayoweza kuwavutia
Wawekezaji badala ya kutegemea misaada kutoka kwa wahisani.
Wakati huo huo IMF ilisema itafungua ofisi yake nchini kama sehemu ya mpango wake wa kusogeza huduma zake katika nchi za Afrika.
Mpango huo uliotangazwa juzi ni changamoto muhimu kwa nchi yetu ambayo ilitanganzwa na IMF kuwa moja kati ya nchi zinazotekeleza vizuri sera za uchumi za shirika hilo.
Kahn alisema Tanzania imefanya vizuri katika kutekeleza sera za uchumi za IMF pamoja na kudhibiti mfumuko wa bei.
Alifahamisha kuwa Mpango wa Kupunguza Umasikini na Kukuza Uchumi (Mkukuta) ni mfano hai wa jinsi Tanzania ianavyofanya vizuri katika kukabiliana na umasiki nchini.
Kahn alifahamisha kuwa mpango huo pia unatarajiwa kutekelezwa katika nchi kadhaa za ukanda wa Afrika Magharibi.