William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,584
- 10,466
Nakubaliana na wewe. Hata mimi sijaona sababu ya kushtusha isipokuwa ilipodaiwa na watu wa Chadema kuwa baba yake Oscar hakuwa mtanzania. Hivyo, kiukweli kabisa siamini kama Oscar kama Oscar ana kosa lolote la yeye kutokuwa raia isipokuwa aidha kwa kutokujua au kwa wazazi kutozingatia kuwa mtoto wao alitakiwa aukane uraia wa wazazi wake alipofikisha miaka 18.
Hivyo, kama ilivyokuwa kwa Jenerali au wengine Oscar anaweza kujikuta ni majeruhi wa kutozingatia sheria. Yawezekana muda wote huu yeye amekuwa akijitambua na kutenda kama Mtanzania. Hivyo, endapo ataenguliwa kwa kweli itamuumiza sana.
Ndiyo maana swali la msingi haliko kwa Oscar bali kwa wazazi wake. Uraia wa Oscar unategemea uraia wa wazazi wake. Kama wazazi walikuwa ni Watanzania/Watanganyika wakati Oscar anazaliwa basi Oscar ana uraia wa Tanzania na kesi kwishnei! Lakini, kama wazazi wake hawakuwa Watanzania au Watanganyika basi Oscar ana kazi kweli. Ila anachoweza kufanya ni kujitoa kwenye kinyang'anyiro, kuomba uraia na mwakani kugombea tena.
-
- Ninajadili hii ishu na openmind, kwamba anything is possible, lakini facts kwanza sijaona za kuni-convince kwamba jamaa sio raia!
FMEs!
- Mkuu Mag3, nimeuliza wanaohusika huko ndani ya CCM baada ya kuiona hii article, ukweli ni ina utata kidogo kwa sababu waliokutana na kuamua sio NEC, ila ni CC ambayo imekutana kwa niaba ya NEC kuepuka gharama za kuita kikao kizima cha NEC na kwamba hiyo inakubalika ndani ya chama cha CCM.
- Pili nimeambiwa kwamba aliyepitishwa ni Oscar ambaye ana jina la mwisho Mukasa, lakini jina la Mukasa ni moja ya sababu kubwa zilizoleta kizaa zaa ndani ya kikao cha kumpitisha huko CC, kwa hiyo ninajaribu again kuthibitisha kama either ni yeye huyo huyo ameamua kuondoa jina la Mukasa, na kutumia Rwegasira, au ni mwingine kabisaa na kama ni mwigine kabisa sitasita kuiomba radhi JF
Respect.
FMEs!
- Mkuu samahani kwa kukukwaza tatizo langu ni haya maneno hapo juu, ninayaona ni unfair kwa Oscar, kwa sababu hukuwepo akizaliwa sasa hujui alizaliwa wapi, huenda alizaliwa hapo wakahama na wakarudi baada ya ku-retire!
Respect.
FMEs!
Bila samahani Mkulu,
Mimi pia ningependa kijana wa "Familia Bora" (hapa simaanishi bora kwa ukwasi) aingie mjengoni. Lakini rejea ya historia na uasili wa familia ndo vyaweza kuleta kikwazo.
Unajua hapa B'mulo baada ya choya kuwafanyia kitu mbaya wagombea wenye nguvu na kufuatia kifo cha Balampama sikuona kama Oscar alikuwa na mpinzani. Hili tu lanaURAIA WA WAZAZIndo tu laweza kuleta kipingamizi.si Uraia wa Oscar
Sawa Mkuu ila ulipoandika haya yafuatayo ulikuwa na maana gani ?
Naona hapa kulikuwepo na utata kuhusu jina Mukasa/Rwegasira. Sasa tupe sababu ya jina Mukasa kuleta kizaa zaa kwenye kikao cha CC . Je na hapa tutegemee ufisadi wa majina kama ule wa Rostamu Chakaar Aziz Abdulrasul etc ..kwi kwi kwi !!!
Bila samahani Mkulu,
Mimi pia ningependa kijana wa "Familia Bora" (hapa simaanishi bora kwa ukwasi) aingie mjengoni. Lakini rejea ya historia na uasili wa familia ndo vyaweza kuleta kikwazo.
Unajua hapa B'mulo baada ya choya kuwafanyia kitu mbaya wagombea wenye nguvu na kufuatia kifo cha Balampama sikuona kama Oscar alikuwa na mpinzani. Hili tu la na ndo tu laweza kuleta kipingamizi.
- Mkuu kumbe unaandika ukiwa Biharamulo? duh! that is wasup! akili bwana kweli ni nywele kila mmoja ana zake, endelea kutuletea dataz za huko mkuu.
- Lakini kwenye hii ishu, ningependa sana kumsikia Mkulu Kiungani what he has to say ninaamini kwamba ana authority kubwa sana na hii ishu, kwa sababu in one way or another ni lazima anamfahamu Oscar, kuliko sisi wengine wengi.
Respect.
FMEs!
Nani ana mzigo wa hakikisho kuthibitisha ukweli wa uraia wa Rwegasira?
- Mkuu sikuwepo kwenye kikao ila aliyenipa dataz hakutaka niweke yote wazi, lakini all and all siamini kwamba CCM wanaweza kuwa low kiasi hicho cha kumpitisha a foreigner kuwa mgombea wao, ndio maana ninasema ninataka kusubiri more fatcs.
Respect.
FMEs!
Rwegasira mwenyewe, katika umri huu anajijua kama ni raia ama la ili kurefute hilo pingamizi.
...
Nani ana mzigo wa hakikisho kuthibitisha ukweli wa uraia wa Rwegasira?
Sikusema Rwegasira anajua au hajui uraia wake, au ana umri mdogo ua mkubwa.
Nani ana mzigo wa hakikisho kuthibitisha ukweli wa uraia wa Rwegasira?
Rwegasira, kama wazazi wake ni raia wa Tz anatakiwa apeleke vithibitisho kwa tume, kama wazazi wake sio raia anatakiwa apeleke uthibitisho wa kukana uraia wake wa awali, I stand to be corrected.
Rwegasira, kama wazazi wake ni raia wa Tz anatakiwa apeleke vithibitisho kwa tume, kama wazazi wake sio raia anatakiwa apeleke uthibitisho wa kukana uraia wake wa awali, I stand to be corrected.
Rwegasira mwenyewe, katika umri huu anajijua kama ni raia ama la ili kurefute hilo pingamizi.
Mara ngapi wamefanya hayo, ama unataka kutufanya hatuna kumbu kumbu? Akina Ulimwengu et al?
Mkuu Dilunga,
Kwa uelewa wangu, swala hili linatakiwa kwenda kwa ngazi.
Ngazi ya kwanza ni mgombea wa CHADEMA kuweka pingamizi, na ninadhani mtu anapoweka pingamizi ambalo limepelekea/sababisha Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo kumwandikia barua mgombea wa CCM basi lazima kuna evidence za kiwango fulani ambazo zina hitaji majibu.
Ngazi ya pili ni majibu ya Bwana Oscar ambayo yatasaidia kutoa uamuzi wa Tume ya Uchaguzi ili kuona kama pingamizi limejibiwa ipasavyo au la.
Iwapo Tume ya Uchaguzi itatupilia mbali pingamizi hilo, basi mgombea wa CHADEMA ana haki ya kwenda mahakamani kuomba Mahakama isimamishe uchaguzi mpaka kwanza kesi ya uraia ya mgombea wa CCM imalizwe kwanza. Na kama uchaguzi ukifanyika na CCM wakashinda basi mgombea wa CHADEMA anaweza kwenda mahakamani kupinga ili jamaa avuliwe ubunge.
Katika stage ya 3, option zote mbili zina advantage kwa CCM kwa kuwa wanaweza kuweka mtu mwingine just in case mahakama ikiweza ku-rule kwamba kijana siyo raia. Na kwa kuzingatia kwamba kesi za uchaguzi huwa zinachukua muda mrefu inaweza kuwa haina maana kulipa shilingi milioni 5 kwa ajili ya kupinga matokeo ya uchaguzi na kesi inaweza kuisha mwakani mwezi Oktoba wakati wa uchaguzi mwingine. Kuna kesi za uchaguzi za mwaka 2005 mpaka leo hii bado ziko mahakamani na hazitolewa hukumu.
....
Nikisema Uwiano ni Mkenya, huna jukumu kuthibisha we si Mkenya. Mzigo wa kuthibisha tuhuma ni wa mtuhumu.
Mzee umeanza P.....hivi Arcado Ntagazwa aliwahi kuwa na kesi na uraia wake kama nakumbuka vizuri, alikuwa Mbunge na waziri wa mazingira..lakini uraia wake ulileta utata sijui kesi ilishia wapi.....- Kama umeamua kujifanya mbumbu ni tatizo lako sio langu, yaani mimi ninaandika hoja wewe unajiona mbumbumbu halafu unataka kunilaumu mimi? Nitakusaidia vipi hapo?
what the hell is "mzigo wa hakikisho".. una maana ya "burden of proof"? duh.. tafuta lugha yake ya Kiswahili usitafsiri neno kwa neno!
Hiki ni kitu Rwegasira anatakiwa kufanya iwapo yeye ndio ana mzigo wa hakikisho la kuthibitisha uraia wake.
Kama Rwegasira ndio ana mzigo wa uthibitisho wa kuanisha uraia wa Rwegasira kwa sababu unasema Rwegasira ndio anajua ukweli, maana yake CHADEMA hawajui. Na kama hawajui, basi wasituhumu.
Nikisema Uwiano ni Mkenya, huna jukumu kuthibisha we si Mkenya. Mzigo wa kuthibisha tuhuma ni wa mtuhumu.