Nakumbuka enzi za mwalimu kuna mwandishi mmoja aliwahi kutoa kitabu kilichokuwa kikiitwa 'Kaptula la Max'.Maudhui ya kitabu hiki yalikuwa yakimzungumzia mtu aliyeitwa max ambaye alikuwa mnene sana na ambaye alipenda sana kuvaa kaptula.Kuna mtu mwingine alikuwa mwembamba sana ambaye alifurahishwa na uvaaji wa Max na hivyo yeye naye kuhitaji kushonewa kaptula kubwa kama la Max bila kutafakari kama ataweza kuvaa nguo ya Max.tatizo la nchi yetu ni kurukia mifumo bila kufanya upembuzi yakinifu kwa mazingira ya kwetu.Matokeo Makubwa Muda huu bila kuangalia idadi ya vitabu,maabala,walimu wenye sifa,majengo,motisha.Kweli nchi hii ni Pepo la mabwege.