Biashara ya Vinywaji vikali

Biashara ya Vinywaji vikali

db63

Member
Joined
Jul 3, 2018
Posts
17
Reaction score
10
Wakuu habari ,

Nahitaji ushauri ninataka kuanzisha biashara ya pombe kali na pombe laini lakini za kuimport kama brutal, mliotembea ni pombe ipi nikiileta Tanzania naweza kupata faida na kukuza biashara ?

Je naweza kupata nafasi ya kuingiza brutal ilihali kuna mtu mwingine anaingiza? Au bidhaa ikishakuwa na agent hakuna mwingine anayeruhusiwa.
 
Location (mkoa,wilaya) unayo tamani kufanyia hiyo biashara ni wapi..?

Mtaji unao tazamia kuanzanao ni around pesa ngapi..??

Muda wako utakao utumia kwenye hiyo biashara (unatazamia) itakua masaa magapi...??

Class ya watu wanao zunguka/kwa wingi katika eneo hilo la biashara ni gani (juu, kati, chini)...??

Unapo fikiria kuweka hiyo business ni high way, kichochoro ama eneo lenye mrundikano wa watu wengi...??
 
Mimi nataka kuuza kwa jumla , sihitaji kuwa na Bar wala liquor store,nataka kuwekeza tu kama agent wa kuimport kisha nawauzia wengine
 
Wakuu habari ,

Nahitaji ushauri ninataka kuanzisha biashara ya pombe kali na pombe laini lakini za kuimport kama brutal, mliotembea ni pombe ipi nikiileta Tanzania naweza kupata faida na kukuza biashara ?

Je naweza kupata nafasi ya kuingiza brutal ilihali kuna mtu mwingine anaingiza? Au bidhaa ikishakuwa na agent hakuna mwingine anayeruhusiwa.
Mkuu Ni Idea nzuri.

Ila nadhani unatakiwa kuchagua vinywaji ambavyo havipo hapa Tanzania kwa sasa. Kwa sababu vinyaji unavyoona ambavyo ni Imported kuna watu wame monopolise vibali vya kuleta hapa nchini. Au labda niseme kuna authorised dealers wa vinywaji hivyo.. Kwa mfano kinywaji kama Windhoek kuna supplier wake ambaye ukileta wewe vyakwako basi unakuwa umeingilia soko la watu..(Same applied kwa Heineken, Brutal na vingine)

So mimi ndio nijuavyo hivyoo
 
Asante sana kwa maoni ,bila shaka nami nafikiri huwa iko hivyo.
 
ndugu mleta mada majibu utakayo pokea mida hii mpka saa 11 asubuhi naomba uyafanyie kazi maana hap utakua unazungumza na watu wenye utimamu,, ila pakikucha kuwe changanyikeni walevi wakajaa humu unaweza ukaukimbia uzi wako😆😆,,

all the best bro
 
Ni kweli ila majibu yote nitachukua na kupata mwanga wa jambo langu, asante pia na wewe
 
nasubiri na mimi nijifunze...hasa hii ya kutengeneza vinywaji vikali
 
Kwa maoni yangu unaanzia mbali mno ndugu, ni kheri ungeanza na hizi hizi za humu nyumbani (bado still ni hot cake), na za nje ila uwe distributor mkubwa wa jumla, ukisha master hiyo utajiongeza na hzo imports. Tafuta chimbo, miji iliochangamka na inayokua kwa kasi, mfano kahama, chunya, mbeya city, tunduma-songwe. Anza na products za TBL na zngne ambazo ni common nchini. Bia za kopo zote kama safari, klmanjaro, redds, fish, castle lite Konyagi, kvant, valeur, choice, Tzee, black&white, redlebell, brand tofauti za wine za dodoma, 4cousins, autumn harvest, drosthof, bia za cane za nje km windhoek, heineken, savanna, desperados, etc(list ni ndefu). NB. Ukitaka kuwa agent wa TBL (kwa bia za kreti) ni kipengele chenye mchakato mgumu na uvumilivu na itahitaji mtaji si chini ya M100, hawatoi kizembe uwakala pamoja na kuwa na hyo fedha ila ukiupata umeula. Utahitaji pia uwe na nyenzo za kazi kama magari na vyombo vdgo vya usafiri kwa usambazaji.

Kupata jina kubwa kwa biashara ya pombe ni kugusa tu.
 
Mimi nataka kuuza kwa jumla , sihitaji kuwa na Bar wala liquor store,nataka kuwekeza tu kama agent wa kuimport kisha nawauzia wengine
ukileta nishtue niwe msambazaji
 
Wakuu habari ,

Nahitaji ushauri ninataka kuanzisha biashara ya pombe kali na pombe laini lakini za kuimport kama brutal, mliotembea ni pombe ipi nikiileta Tanzania naweza kupata faida na kukuza biashara ?

Je naweza kupata nafasi ya kuingiza brutal ilihali kuna mtu mwingine anaingiza? Au bidhaa ikishakuwa na agent hakuna mwingine anayeruhusiwa.
Kuna pombe ilikuaga inaitwa PINGU, wakati kwa kunywa ulishauriwa kubana kisawa sawa suruali kwenye miguu
 
Sawa ukitaka kulinda biashara yako hiyo juu ya nguvu za giza na kuosha nyota yako uje Inbox ndugu nitakusaidia
 
Back
Top Bottom