Habarini wadau.
Nataka kufungua Toto/Baby shop maana nimeona hapa mtaani kwangu hakuna biashara ya namna hii.
Duka litakuwa na vitu vya mahitaji ya msingi ya kila siku ya mtoto kuanzia siku moja mpaka miaka miwili.
Napenda kufahamu ni wapi naweza kuwa napata mahitaji ya hilo duka kwa bei ya jumla.
Diapers
Chupi za mpira(reusable)
Mafuta,sabuni,powder
Mabeseni ya watoto ( yenye starter pack na mabeseni tupu)
Mataulo,babyshow + vinguo vya pamba vya watoto wachanga.
Pacifier/soother/chupa za watoto kunyonya.
na vifaa vyote vingine vya watoto wa siku moja mpaka miaka miwili.