Biashara ya online ni nzuri sana lakini watanzania wengi ni wezi

Cashman

JF-Expert Member
Jun 8, 2018
2,296
3,967
Ni kweli kabisa utaona kwa sasa ni rahisi kufanya biashara ukiuza online.Nchi nyingine hasa za Asia wamefanikiwa sana katika biashara ya kuuza vitu online kwa sababu ya uaminifu wao.

Kwa hapa Tanzania,tuna tatizo kubwa sana ambalo sina uhakika kama hata jamii inaliona kama tatizo.Suala la kutokuwa waaminifu.Suala la kutojali kumuumiza mtu mwingine kwa kumdhulum.
Hili lipo kwenye vizazi vyetu na ndio maana hata watu wanaoingia serikalini,asilimia kubwa ni wezi na wasio na huruma hata kidogo.

Kusema kweli kwa wengi halionekani kama ni tatizo.Ndio maana hata Dar inaitwa "bongo" bongo maana yake ni utapeli.Kutumia akili "siyo ya ubunifu katika vitu" bali akili ya kuwatumia "washamba" kujinufaisha.Kuwaliza watu ambao hawajaamka kujua dunia hii ni ya watu "makatili" Watu ambao nafsi zao bado zina dhamiri safi.Kuwaliza watu kama hao ndio inaonekana ujanja.

Kuna umuhimu wa suala hili kulifanya mjadala wa kitaifa.Watu wanaokuwa na tabia ya ujanja ujanja wa kiswahili,waonekane ni wabaya kwenye jamii,tofauti na sasa ambapo utapeli ni sifa njema.
Ukisikia Sinza kwa wajanja haimaanishi hawa watu ni wema.Maana yake ni wale wanaokuuzia vitu feki kwa bei ya vitu halisi.Ni wale wanaofeki hadi maisha yao ili waonekane wa mjini kuliko watu wengine.Ni pale utakuta watu wanauza miili yao hadi makaburini.Hizi ndizo sifa za "wajanja"

Ni muhimu tubadilike ili tusiwaogopeshe watu kutumia fursa ambayo dunia ndiyo inaitumia kwa sasa.Siyo mtu anaagiza mitumba gredi A,kisa kaagiza mtu wa Katavi,anatumiwa vitu vya hovyo gredi D.Tuweni waaminifu.Tumwogope Mungu
 
Ni kweli kabisa utaona kwa sasa ni rahisi kufanya biashara ukiuza online.Nchi nyingine hasa za Asia wamefanikiwa sana katika biashara ya kuuza vitu online kwa sababu ya uaminifu wao.

Kwa hapa Tanzania,tuna tatizo kubwa sana ambalo sina uhakika kama hata jamii inaliona kama tatizo.Suala la kutokuwa waaminifu.Suala la kutojali kumuumiza mtu mwingine kwa kumdhulum.
Hili lipo kwenye vizazi vyetu na ndio maana hata watu wanaoingia serikalini,asilimia kubwa ni wezi na wasio na huruma hata kidogo.

Kusema kweli kwa wengi halionekani kama ni tatizo.Ndio maana hata Dar inaitwa "bongo" bongo maana yake ni utapeli.Kutumia akili "siyo ya ubunifu katika vitu" bali akili ya kuwatumia "washamba" kujinufaisha.Kuwaliza watu ambao hawajaamka kujua dunia hii ni ya watu "makatili" Watu ambao nafsi zao bado zina dhamiri safi.Kuwaliza watu kama hao ndio inaonekana ujanja.

Kuna umuhimu wa suala hili kulifanya mjadala wa kitaifa.Watu wanaokuwa na tabia ya ujanja ujanja wa kiswahili,waonekane ni wabaya kwenye jamii,tofauti na sasa ambapo utapeli ni sifa njema.
Ukisikia Sinza kwa wajanja haimaanishi hawa watu ni wema.Maana yake ni wale wanaokuuzia vitu feki kwa bei ya vitu halisi.Ni wale wanaofeki hadi maisha yao ili waonekane wa mjini kuliko watu wengine.Ni pale utakuta watu wanauza miili yao hadi makaburini.Hizi ndizo sifa za "wajanja"

Ni muhimu tubadilike ili tusiwaogopeshe watu kutumia fursa ambayo dunia ndiyo inaitumia kwa sasa.Siyo mtu anaagiza mitumba gredi A,kisa kaagiza mtu wa Katavi,anatumiwa vitu vya hovyo gredi D.Tuweni waaminifu.Tumwogope Mungu
Pole sana Mkuu,
Siku zingine kua makini
 
Kiongozi una hoja japo sio wote
Niwakumbushe tu watu wenye TABIA HIYO YA UTAPELI, kama wanataka waendelee kuwa masikini maisha yao yote, wendelee na huo mchezo
Watu wakitapeliwa bidhaa (wasipotumiwa bidhaa waliyolipia) kwa jinsi wanavyo walaani
Amini usiamini; huwezi kutoboa maisha!!!
Vijana: Tafuta bidhaa hata huko Kariakoo (duka la mtu) weka cha juu kidogo uza. Mtu akitaka Simu, nenda chimbo pata bei weka cha juu kidogo; ukilipwa hela chukua cha kwako cha juu, tumia mtu simu yake....
KUFANYA UTAPELI NI KUJIONGEZEA UMASIKINI!!!
Na kwa bahati mbaya hutaweza kuwapata ulio watapeli ili uwaombe msaamaha!
 
Nimewahi kudondosha infix kwenye gari yaani ndani ya dakika sifuri imetoweka
 
Mimi nikiona mtu anatapel mtandaon namuona haha akili...sababu mtandain hujui unamuuzia nani ao unakuwa unajiweka kwenye hatar sana

Mimi nauza bidhaa online
Kuna matukuo yashawahi kunitokea ikanifanya niwe muaminifu mara 100 zaidi

Kuna mteja alinifwata Facebook inbox akawa anaitaji saa (Ilikuwa ni kipindi kile corona imepamba moto) mteja alikuwa dodoma alikuwa anaitaji Saa, chat zetu hazikuwa ndefu yani alikuja messenger akataka kuona picha za saa vizuri baada ya kumtumia akataka kujua mzigo unamfikiaje maana alikuwa Dodoma nikamuelezea then akaomba namba yakutuma pesa apo n messenger (nilishangaa kwa mteja wa mkoani kuwa direct vile, nishazoea wateja wa mikoan ad uwaaminishe sana kuhusu uwaminifu wako ndio watume pesa) Basi nikamtumia yule mzee namba ya kutuma pesa, dakika mbili nyingi muamala ukasoma baada ya muamala kusoma nikaona jina kwanza nikashangaa uyu ndio mwenyewe au ni majina tu yanafanana, basi nikaandaa mzigo then nikamwambia anitumie ma jina ya kuandika kwenye mzigo na namba ya simu lahaulla si akaamua kunitumia na picha kabisa na jina la utambulisho na kila kitu basi nikautuma mzigo adi dom saa zikafika alifurahi sana saa zilikuwa nzuri sana asa ya mke wake aliipenda sana (kiukwel mpaka time hii sikuamin kama ni yule mzee kweli nilijua labda mtu tu wanafanana majina kaamua kunichekecha ili asatapeliwe)

Basi bwana siku zikapita akawa anaona Status zangu yeye alikuwa sio mtu wakuweka ata Status, tuliendelea kufanya biashara akiitaji Saa nikawa namtumia

Asa kuna kipindi akaja dar alikuwa yupo bize sana ila alikuwa anaitaji saa, akaweka oda ya saa 2 kama kawaida ya kwake na mkewe si nikampelekea bale bana ndio namkuta ni yeye mwenyewe nikasema eeeeeh ni kwel yan

Hii kitu ilinifundisha uaminifu sana, nilijiuliza lqbda ningekuwa tapeli yan yule mzee asingetumia ata nguvu kunikamata maana yeye mwenyewe ananguvu

Ninachoshukuru yule mzee alitokea kuniamin yan vitu vyake vingi akiwa ananunua kama vinaitaji kukaguliwa lazima aniagize mimi nivi check

Yan namba yake ndio namba ya mtu mzito sana kwenye hii nchi niliyo nayo
 
Mimi nikiona mtu anatapel mtandaon namuona haha akili...sababu mtandain hujui unamuuzia nani ao unakuwa unajiweka kwenye hatar sana

Mimi nauza bidhaa online
Kuna matukuo yashawahi kunitokea ikanifanya niwe muaminifu mara 100 zaidi

Kuna mteja alinifwata Facebook inbox akawa anaitaji saa (Ilikuwa ni kipindi kile corona imepamba moto) mteja alikuwa dodoma alikuwa anaitaji Saa, chat zetu hazikuwa ndefu yani alikuja messenger akataka kuona picha za saa vizuri baada ya kumtumia akataka kujua mzigo unamfikiaje maana alikuwa Dodoma nikamuelezea then akaomba namba yakutuma pesa apo n messenger (nilishangaa kwa mteja wa mkoani kuwa direct vile, nishazoea wateja wa mikoan ad uwaaminishe sana kuhusu uwaminifu wako ndio watume pesa) Basi nikamtumia yule mzee namba ya kutuma pesa, dakika mbili nyingi muamala ukasoma baada ya muamala kusoma nikaona jina kwanza nikashangaa uyu ndio mwenyewe au ni majina tu yanafanana, basi nikaandaa mzigo then nikamwambia anitumie ma jina ya kuandika kwenye mzigo na namba ya simu lahaulla si akaamua kunitumia na picha kabisa na jina la utambulisho na kila kitu basi nikautuma mzigo adi dom saa zikafika alifurahi sana saa zilikuwa nzuri sana asa ya mke wake aliipenda sana (kiukwel mpaka time hii sikuamin kama ni yule mzee kweli nilijua labda mtu tu wanafanana majina kaamua kunichekecha ili asatapeliwe)

Basi bwana siku zikapita akawa anaona Status zangu yeye alikuwa sio mtu wakuweka ata Status, tuliendelea kufanya biashara akiitaji Saa nikawa namtumia

Asa kuna kipindi akaja dar alikuwa yupo bize sana ila alikuwa anaitaji saa, akaweka oda ya saa 2 kama kawaida ya kwake na mkewe si nikampelekea bale bana ndio namkuta ni yeye mwenyewe nikasema eeeeeh ni kwel yan

Hii kitu ilinifundisha uaminifu sana, nilijiuliza lqbda ningekuwa tapeli yan yule mzee asingetumia ata nguvu kunikamata maana yeye mwenyewe ananguvu

Ninachoshukuru yule mzee alitokea kuniamin yan vitu vyake vingi akiwa ananunua kama vinaitaji kukaguliwa lazima aniagize mimi nivi check

Yan namba yake ndio namba ya mtu mzito sana kwenye hii nchi niliyo nayo
Nani huyo mkuu
 
Back
Top Bottom