Wang chung
Member
- Oct 26, 2024
- 32
- 48
Biashara ya nafaka ni biashara nzuri sana. Nimefanya tafiti toka mwaka 2021 nemegundua kuwa mahindi Huwa yanashuka sana mwezi wa 7 Hadi 9 bei hufika Hadi tsh 6000 kwa debe moja(Lita 20) kwa maeneo ya vijijini (utafiti wangu nilifanyia njombe). Ila ikifika mwezi wa 2 Hadi 6 mahindi huuzwa tsh 10000 Hadi 12000.
Pia magunia ya kuhifadhia mahindi(haya ni magunia ambayo huitwa hermetic bags kitaalumu, ni magunia yenye layer zaidi ya moja) huuzwa tsh 6000 kwa Kila gunia moja linaloweza kubeba zaidi ya debe 6. Kiufupi Kila gunia moja la debe sita linakupa faida ya tsh 24000. Ukiwa na Dunia zako 100 za mahindi unapata faida ya milioni 2.4
. Jitaidi kupepeta mahindi Yako vizuri kabla hujaweka kwenye magunia Ili kuzuia wadudu kuhalibu mazao Yako na wewe kukosa soko .
JAPO FAIDA SIO KUBWA SANA ILA SIO SAWA NA KUWEKA HELA BANK ZIKAE TU
Karibuni
Pia magunia ya kuhifadhia mahindi(haya ni magunia ambayo huitwa hermetic bags kitaalumu, ni magunia yenye layer zaidi ya moja) huuzwa tsh 6000 kwa Kila gunia moja linaloweza kubeba zaidi ya debe 6. Kiufupi Kila gunia moja la debe sita linakupa faida ya tsh 24000. Ukiwa na Dunia zako 100 za mahindi unapata faida ya milioni 2.4
. Jitaidi kupepeta mahindi Yako vizuri kabla hujaweka kwenye magunia Ili kuzuia wadudu kuhalibu mazao Yako na wewe kukosa soko .
JAPO FAIDA SIO KUBWA SANA ILA SIO SAWA NA KUWEKA HELA BANK ZIKAE TU
Karibuni