Biashara ya Miamala M-PESA YAS. N.K bado zinalipa

Biashara ya Miamala M-PESA YAS. N.K bado zinalipa

Hakuna biashara isiyolipa , ukiona hailipi basi jua haukfuata misingi ya biashara wakati unaanzisha.

Nilivyofundishwa na mwalimu wangu wa biashara aliniambia biashara inahitaji vitu vikuu vitatu vinavyoenda kwa Pamoja.

1.Capital (Mtaji)
2.Knowledge(Maarifa)
3.Market(Soko).
Hizi elimu za makatatasi mara nyingi hazitumiki mtaani ingia mtaani ndio utapata elimu halisi
 
Mi ni muumini sana kupiga simu. Ilivyoingia tu text ya kwanza ningepiga simu.
Ili upate muumini wa kupiga simu na mwenye akili angalau lazima umlipe vizuri. Kwa kuwa ana akili, anatafakari anafanya maamuzi kufuata kazi ya maslahi. Sasa tajiri bahiri anataka wafanyakazi cheap ambao ndio hao hawana akili sawasawa.
 
Hizi elimu za makatatasi mara nyingi hazitumiki mtaani ingia mtaani ndio utapata elimu halisi
Sasa unaweza kuingia mtaani kufanya biashara bila Mtaji? Utawezaje kufanya biashara bila kuwa na ABCs za hizo biashara? Je bila kujua Soko lako unaweza kufanya biashara? Au ndiyo mambo ya kwenda kufungua stationary karibu na BAR badala ya Shule.

Kabla ya kuingia mtaani lazima ujue hivyo vitu vitatu(Capital,knowledge na market)......Maarifa utapata kwa waliotangulia/kuona na kujifunza.
 
Lazima kwanza wewe uwe umebobea katika tathnia ya miamala ndio unaweza kummudu na huyo mfanyakazi ila kama huelewi chochote mtalizwa wewe na mfanyakazi wako
Kiukweli mimi sijawai kufanya hii biashara Experience sina ila kwa baadhi ya research zangu najiona kama nikichukua tahadhari zote juu ya utapeli wowote kwenye hii kazi naweza kupambana freshi muhimu umakini wa hali ya juu
 
Sasa unaweza kuingia mtaani kufanya biashara bila Mtaji? Utawezaje kufanya biashara bila kuwa na ABCs za hizo biashara? Je bila kujua Soko lako unaweza kufanya biashara? Au ndiyo mambo ya kwenda kufungua stationary karibu na BAR badala ya Shule.

Kabla ya kuingia mtaani lazima ujue hivyo vitu vitatu(Capital,knowledge na market)......Maarifa utapata kwa waliotangulia/kuona na kujifunza.
Unaweza ukavijua na bado usitoboe akili kumkichwa
 
Habari za wakati huu wakuu,
Naitwa Godfrey, nina mpango wa kuanzisha biashara ya M-Pesa nikiwa na mtaji wa takriban milioni 3. Nipo Dar es Salaam (eneo la Tegeta na Mwenge) na nimekuwa nikifuatilia kwa muda, ila bado nina maswali kadhaa:

1. Je, biashara hii bado inalipa kweli ?

2. Kuna changamoto zipi kubwa ninazopaswa kujiandaa nazo?

3. Na kama mtu ana mtaji kama wangu, kuna kitu gani bora zaidi ya M-Pesa unashauri nifanye?

Naomba ushauri kutoka kwa waliowahi au wanaofanya biashara hii kwa sasa.
Ushauri wenu utanisaidia sana kabla sijarisk hela yangu yote. Nimeipata kwa shida sana hii na kwa mda mrefu

Asanteni sana 🙏
Miamala inalipa vizuri ukiwa na wateja wengi (muamala ya mara kwa mara) nje na hapo utaichukia

Hivyo eneo lenye watu wengi na mizunguko ya hela ndio itakuwa sehemu inayofaa

Kwa Mwenge- eneo lenye watu wengi ni sehemu ya machinga wa mitumba pale karibu na Jose saloon.

Changamoto
1) mawakala ni wengi saivi kila eneo unakoenda haukosi mawakala zaidi ya 3 au nne wananyang'anyana wateja ,
2) utapeli - utapeli kwenye muamala attempt zake ni nyingi kushinda biashara zingine maana kuna matapeli wa cyber crime(kama sijakosea) na matapeli wale wa kuingia dukani- hii ni changamoto kubwa kuliko zote wanazokutana nazo mawakala, hivyo angalau uwe mjuzi kidogo au uwe umewahi kufanya ndio unazihandle kwa haraka

4) mtaji- wengi wanasumbuliwa na mtaji -kwa 3M bado ni ndogo maana ukigawanya unatakiwa uwe na float(hela ya kwenye simu- mteja akitaka kuweka) na cash(ili mteja akitoa umpe)
- ukigawanya vizuri hapo maana yake inabidi uwe na float laki 5 kwa kila mtandao(Airtel,voda, mixx, halotel) inakuwa milion2 ,unabakiwa na cash 1M ,

- implication yake ni kwamba mteja anaetoa 1M au kuweka huwezi kumhudumia ni nje ya uwezo wako. Kumbuka muamala mikubwa ndio ina commission nzuri ,
 
Kiukweli mimi sijawai kufanya hii biashara Experience sina ila kwa baadhi ya research zangu najiona kama nikichukua tahadhari zote juu ya utapeli wowote kwenye hii kazi naweza kupambana freshi muhimu umakini wa hali ya juu
Sasa utawezaje kumuelekeza mtu(mfanyakazi) kitu ambacho hukijui
 
Kiukweli mimi sijawai kufanya hii biashara Experience sina ila kwa baadhi ya research zangu najiona kama nikichukua tahadhari zote juu ya utapeli wowote kwenye hii kazi naweza kupambana freshi muhimu umakini wa hali ya juu
Yes kila kazi ina risk hakuna kazi haina risk , muhimu umakini
 
Unaweza ukavijua na bado usitoboe akili kumkichwa

Kufanya vizuri kibiashara na kutoboa ni vitu viwili tofauti.

Successful bizness ni ile inayoleta faida na kumake Fortune(Kutoboa) kupitia biashara ni siri ya MTOBOAJI.
 
Sasa utawezaje kumuelekeza mtu(mfanyakazi) kitu
Sasa utawezaje kumuelekeza mtu(mfanyakazi) kitu ambacho hukijui

Lazima kwanza wewe uwe umebobea katika tathnia ya miamala ndio unaweza kummudu na huyo mfanyakazi ila kama huelewi chochote mtalizwa wewe na mfanyakazi wako
Kwa hapa nitakupinga mwanangu, mfano mzuri kuna mshikaji wangu mmoja Ana bodaboda zake kama 7 ivi amewapa vijana na wanamletea hesabu ila yeye hajawai kua dereva boda na wala hajui hata kuisogeza ila Ana,uwelewa mzuri kwenye iyo biashara anacheza na hesabu tu na mambo yanaenda na nikazi yenye risk balaa
 
njoo kifanya kwa siku hata uwe na m30 utaishiwa cash had front hasa jumam
 
Kuna tajiri mmoja siku nilikuta anampiga makofi mfanyakazi wake wa kike....


Jamaa alikua na cashpoint sijui Hawa matapeli wanatumia njia gani wakaja kubadilisha alivyo save jina la bosi wake, dada akaanza kuombwa miamala kutoka Kwa bosi Kuna namba akawa anamuelekeza atume pesa huko Kuna magari yake yamekwama kuchukua mzigo....Kila baada ya muda anaambiwa atume pesa kwenye namba flani, miamala mizito mizito tu..... Mpaka float akaishiwa akawa anataka kwenda kujaza float ndo akakutana na mtu wanafahamiana na bosi wake, yule mtu anamuuliza mbona huku tena ofisini umemuacha nani? Ndo dada anamwambia bosi Leo msumbufu Kila saa anaomba pesa mpaka nimeishiwa float, jamaa ndo akamuambia subiri kwanza akampigia bosi wake, bosi kufika aisee anaangalia miamala alipiga ukunga nusu amuue mtoto wa watu.....


Boss anadai alishampiga marufuku kumtumia pesa hata awe na shida gani ni heri akachukue sehemu nyingine, lakini ndo hivo tena jamaa wakapita na zaidi ya 10M+
Hatari sana
 
Kwa hapa nitakupinga mwanangu, mfano mzuri kuna mshikaji wangu mmoja Ana bodaboda zake kama 7 ivi amewapa vijana na wanamletea hesabu ila yeye hajawai kua dereva boda na wala hajui hata kuisogeza ila Ana,uwelewa mzuri kwenye iyo biashara anacheza na hesabu tu na mambo yanaenda na nikazi yenye risk balaa
Kwahiyo walinganisha bodaboda na miamala sawa
 
Kuna tajiri mmoja siku nilikuta anampiga makofi mfanyakazi wake wa kike....


Jamaa alikua na cashpoint sijui Hawa matapeli wanatumia njia gani wakaja kubadilisha alivyo save jina la bosi wake, dada akaanza kuombwa miamala kutoka Kwa bosi Kuna namba akawa anamuelekeza atume pesa huko Kuna magari yake yamekwama kuchukua mzigo....Kila baada ya muda anaambiwa atume pesa kwenye namba flani, miamala mizito mizito tu..... Mpaka float akaishiwa akawa anataka kwenda kujaza float ndo akakutana na mtu wanafahamiana na bosi wake, yule mtu anamuuliza mbona huku tena ofisini umemuacha nani? Ndo dada anamwambia bosi Leo msumbufu Kila saa anaomba pesa mpaka nimeishiwa float, jamaa ndo akamuambia subiri kwanza akampigia bosi wake, bosi kufika aisee anaangalia miamala alipiga ukunga nusu amuue mtoto wa watu.....


Boss anadai alishampiga marufuku kumtumia pesa hata awe na shida gani ni heri akachukue sehemu nyingine, lakini ndo hivo tena jamaa wakapita na zaidi ya 10M+
Noma sana walinikosaga hii.

Mfumo wa kumtumia mtu hela ni vizuri kujiridhisha kwa kumpigia simu usikie sauti yake hata kama unaona ni namba yake , hasa kama anakuelekeza kutuma kwenye namba huijui
 
Kila biashara inalipa mkuu n ww tu ujuee jinsi yakukabiliana na changamoto zakee ,,,hata ukiwa Kwenye ajira Kwan changamoto ukutanagi nazoo 🤔 na c unazitatuaga na kazi inaendeleaaa😀

Ndivyo hvyo biashara ilivyo..usiwe muoga ila location nzuri na palipo na movemet ya watu n muhimu Kwa hyo biashara yakoo
Hyo common sanaa....na asilmia 70 ya wezi hutoboa.

Makosa hufanywa na mfanyakazi kutoa simu yake hovyo kwa wateja...
 
Back
Top Bottom