Biashara ya kuuza genge

Biashara ya kuuza genge

Haoa
Viazi JE + Viungo vya chai na Pilau!? Akiba JE?! na pia Laki 3 unaanza sijakataa na

hata ukitaka genge la mtaji 50,000 inawezekana lakini swali ni kwamba upo serious

na hiyo biashara? Kama jibu ni "ndio" basi huwezi anza biashara ya mali kuoza na mtaji wa kusua sua.
Hapa umeandika kama anayeanza na 50K anapenda kumbe ndipo muscle yake ilipoishia.
 
Haoa

Hapa umeandika kama anayeanza na 50K anapenda kumbe ndipo muscle yake ilipoishia.
SIO kila anaeanza biashara na mtaji mdogo ni kweli "kakosa mtaji mkubwa au hana" kuna watu biashara ipo damuni (hata mimi siingiii),wanapenda anzia chini chini chini,hawa raia ndio hata mimi nawaogopa,hawa sio watu nawafananishaga na marobot

hela anayo ila anaishi kama hana,mtaji anao ila ukimwambia "upgrade" biashara yako (hataki) yani miaka na miaka utamuona anauza karanga kwenye ungo,au anauza kahawa kijiweni au ana genge lina vitu vya kuhesabika,nk nk..Hawa unaweza fikiri wanasindikiza wengine

ila "hapana" wakkupeleka wanapoishi,wana majumba,wanasomesha,maisha ya kawaida na mazuri tu,sema ndio hivyo ukimkuta kazini na biashara yake ina mtaji wa 50,000 unaweza hisi maskini ndio anaanza biashara huyu kumbe mtu yupo kwenye game huu mwaka wa 8 unaenda ila kaganda kama robot yupo vile vile.NO CHANGES. ukimchukulia poa SHAURI lako.
 
Nilichogundua Watanzania kuja kuondokana na adha ya Umasikini sio leo. Mtu hata atoe ushauri mzuri namna gani lkn bado atatukanwa au kupewa kejeri. Any way hii labda inatokana na stress ambazo tuko nazo asee....!!!
Ni kweli asee,, ht mi nimefuatilia madam nyingi nimeiona hili janga
 
Unajua ukiwa unazungumzia biashara unazungumzia numbers, hakuna kitu kinachoitwa "inalipa sana" au "biashara inafaida sana" ingawaje wafanyabiashara wengi tumekua tukitumia sana haya maneno.

Unachotakiwa kusema (mfano) kwa msimu mzuri nyanya tenga nanunua 30, 000/= nikiuza napata around 40,000/= mpaka 45,000/= so faida inakua 10k to 15k. Tenga moja linaisha after one week. Unaona sasa hesabu inavyoeleweka? Kwa mfano tu hivyo ndo mfanyabiashara anatakiwa kusema biashara inalipa or namna gani vepe!
Kwanza kabisa hii biashara inagusa hitaji la msingi la mwanadam ambalo ni chakula, ni lazima ule ili uweze kuishi na kila siku mahitaji yetu tunayapata sokoni, dukani au gengeni kwahiyo ni uhakika kabisa kuwa na wateja tena kila siku asubuhi mchana na usiku

Kingine nina rafiki yangu mimi ana hii biashara ndo inamuweka mjini anatengeneza faida nzuri sana na wateja wanamiminika kwa wingi sana na tips anazotumia ndo hizo hizo nilizoelezea hapo juu!!!!
 
Huyo anayesema mtaji zaidi ya laki 5 na huyu aliyesema ina faida mno wote maelezo yao hayafanani na genge la mama
 
Swali 1:

Mimi ni mkazi wa Dar es Salaam, ningependa kufanya biashara ya kuuza genge, naomba msaada wenumwenye kujua naweza nunua wapi vitu vya sokoni kwa bei nzuri, na nikimuajiri mtu aniuzie inabidi nimlipaje?

Natanguliza shukurani..

Swali 2:

Pinkshlady
habari wana jf, nawazo lakuanzisha biashara ya genge, lakini la kitofauti kidogo na haya tuliyozoea, nikiwa na imani nitawateka watu wengi, sababu itakuwa karibu na barara kuu na paking ipo ya kutosha,

nikitarajia kuuza matunda ya aina zote, vitu vya sokoni, mayai, ikiwezekana na kuku.

Naomba ushauri wenu niwe na mtaji kiasi gani wa kuanzia? ni soko gani naweza kupata vitu kwa bei ya chini?

na kuna ulazima wa kuwa na leseni ya biashara?

Ushauri:
Genge nyumbani kwako wakazi wa Dar tunakufikishia bidhaa zote za gengeni kwa Bei nafuu
 
Miongoni mwa biashara zenye hela nzuri ni biashara ya genge. Genge linataka mtaji mdogo lakini faida yake ni nzuri sana na kwa mtu anayetaka afanye hii biashara ni nzuri sana

Pia, ni biashara nzuri ambayo hautapata usumbufu wa TRA na pia hutowaza sana kuhusu wezi tofauti na biashara yengine

Cha kuzingatia ili biashara yako hii ya genge ifanikiwe:-

Kwanza unatakiwa uwe mtu social sana uwe unaongea na wateja vizuri pia uwe ni mtu wa tabasamu mteja akija wakati mwingine mfano kitunguu ni 200 yeye kaja na mia basi usisite kumpa kwa mia hii itamsogeza kwako

Kingine ni ubora wa bidhaa, chagua bidhaa zenye ubora na zenye mvuto mfano ukichagua nyanya bamia au nyanyachungu ziwe ni zenye ubora na mvuto hata mtu akipita akiziona azisiache .

Usiuze vitu ghali sana uza walau bei ya sokoni au inayokaribiana na sokoni ili hata mtu akiwaza unavyouza aone ni sawa tu na sokoni aone kwenda buguruni sokoni kununua nyanya ni sawa tu na kununua kwako maana unauza sawa tu na sokoni

Kingine ni kiwango cha bidhaa uzingatie usipunje wateja uza kama kiwango cha vipimo vya sokoni ili kumfanya mtu awe mtejawako wa kila siku aachane na mpango wa kwenda sokoni

Kwa mbinu hizi utapata wateja na utauza sana

Kila la kheri!
Hongera sana kiongozi kwa mawazo yako mazuri,ila biashara hii haiko hivyo unavyozani,kiufupi ni biaharayenye changamoto nyingi sana na imejaa fitina/ushirikina wa kila aina,ukiweza kujipanga(kwa Mungu/miungu) hapo sawa.
 
Habari za wasaa huu wakuu naitaji msaada mwenye kujua vizuri biashara ya uuzaji genge.

ikiwemo mtaji,faida,hasara na pamoja na kuliendeleza zaidi na kuwa la kisasa kabisa Asante na nawasilisha.
 
Biashara nzuri sana mbali na location na mtaji, pia kama unaajiri mtu usimueke kijana wa kiume....

Mana kuna wanawake wanakuja na mia tano but watataka warudi na vitu vya buku...
 
Biashara ya genge jitahidi ujenge connection na wauzaji toka mkoan,hakika utafurahia
 
Back
Top Bottom