Biashara ya Uokaji (Bakery): Mbinu, Ushauri na Changamoto Zake

Short white

Senior Member
Jan 6, 2011
124
32
Bakery.jpg


Salaams JF,

Nilipata wazo la kuanzisha bakery maeneo ya Sinza. Products ni ; Mikate, Maandazi na cakes aina mbalimbali. Sikuomba au kutafuta ushauri kwa mtu yeyote. Pia sijafanya research ya uhakika kuhusu mahitaji halisi ya hizo bidhaa ninazotaka kuingiza sokoni. Pia sijafanya utafiti kuhusu ushindani wa hii biashara. Nimeamua kuchukua RISK 100% katika kuwekeza huko kwenye bakery. Kwahiyo bado sijaelewa / sijajua kama nipo njia sahihi au nimekosea. Naomba ushauri na uelewa wenu kwenu hii biashara.

Hadi sasa nimefanikiwa kupata vitu vifuatavyo;
- Machines- 3 Ovens ( moja kubwa inaingiza paltes 6 na nyingine mbili ni ndogo zinaingiza plates 2 kila moja); 1 Mixer aina ya B30; Shelf; 30 Oven Plates,
-Nimepanga Jengo na kulifanyia ukarabati kulingana na mahitaji ya kazi.
-Nimesajili jina la biashara
-Nimeshapata na TIN
-Nimeshapata leseni

Vitu vinavyohitajika kwa sasa ni;
-Connecting service line ( electricity) kwenye jengo ambalo nimeshafanya wiring
-TFDA authorization
-Source of more finance
-Hard working, knowledgeable and skilled person ( Baker) ambaye ataweza kutengeneza bidhaa mbalimbali
-Bread slicer
-Manager and cashier
-Marketing and sales person
-Distributor

Je mnaonaje wakuu? Je nipo sahihi? Nawakilisha

WADAU WENGINE WANAOHITAJI UFAHAMU WA BIASHARA HII
Ndg zangu wanaJF, kwanza poleni sana kwa msiba wa mwanaJF mwenzetu RM iliyotuchukua almost the whole week kuomboleza.

Napenda kusema yote ni mipango ya Mungu na tulio bado hai let us make this world a better place for US and next GENERATION.

Naomba wenye UELEWA na biashara ya BAKERY wanijuze if it is a good business to engage in (is it paying?), tayari ninayo OVEN yenye uwezo wa kutengeneza walau Mikate 20 at once.

Nashindwa kuanza bcoz nimeambiwa lazima niwe na TIN no, LESENI, TFDA, Mazingira masafi etc, so where can i get all these things guyz or is it possible nikaanza bila moja ya hivyo vitu?

Mie ningependa nianze polepole wakati biashara ikikuwa, walau hata nikianza atleast na mikate 50 per day i have NO PROBLEM with that.

Natanguliza shukrani zangu ndg zangu.
Nataka kufanya biashara ya bakery lakini sina hakika kama inalipa au la.

80% ya mikate na bishaa zitakuwa za brown hivyo hatutegemei volumes bali itakuwa ni quality kwenda kwa juu japo itakuwa na bei ya juu kidogo

Naskia kuna wazungu wa Denmark wako Dar wanafanya ila sina hakika jina la bakery yao na kama wanauza sana

Washindani wakubwa wangu ni wale jamaa pale shoppers plaza na pia jamaa wa pale jengo la mkapa. Lakini sisi tutawekeza zaidi kwenye quality, usafi, na niche market ya wasio kula mitake ya white

Je, italipa? na inahitaji kiasi gani?
Wadau habari za leo?

Natamani kufungua biashara ya mikate yaani Bakery hivi karibuni ila sina uelewa kuhusu biashara hii. Hivyo naomba wenye uzoefu mnielimishe gharama halisi zinazohitajika katika biashara hii ikiwa ni pamoja na vifaa/mashine na bei zake, sehemu zinakopatikana/zinakouzwa kwa hapa Tanzania, gharama nyingine za uendeshaji na jinsi ya kukokotoa faida/hasara katika biashara hii.

Asanteni


MICHANGO YA WADAU
Mkuu Hongera sana kwa jitihada zako, mkuu hizi ndo moja ya aidia ambazo zinamshiko mkuu.

- Labuda mimi nikushauri kitu kimoja mkuu,
1. Hii biashara kama ziilivyo biashara nyingine ni lazima ziww zinatambulika na serikari yetu, hii ni pamoja na kuwa na
- TIN NO
- LESENI
- TFDA CHETI
Mkuu huwezi fanya hiyo viashara bila kuwa na hivi vitu na kitu kama TBS kupata nembo yao si kitu cha mchezo mkuu inaweza kukuchukua miaka kama usipo kuwa makini, make hawa jamaa wanataka
- ENEO LA KUOKEA LIWE SAFI
- VIFAA VISAFI
- NYUMBA AMBAYO IMEJITENGA YENYEWE NA HAISHI BINADAMU HUMO NA IWE NA MADIRISHA NA MWANGA WA KUTOSHA
- WAFANYA KAZI WAKO LAZIMA WAVAE MAVAZI MALUUMU
- NA MENGINEYO
Mkuu si kwamba ukitimiza haya ndo utapewa TBS, razima wakapime na hiyo mikate yako na watakuwa wakifanya ukaguzi wa kushitukiza kuona kama unafuata taratibu zote, na hawakuambii siku wanakuja, na wakikukuta umevunja baadhi ya masharti ndo sahau kabisa, itabidi uanze tena mwanzo

MKUU KUHUSU ENEO LA KUWEKA HII KITU,

- Mkuu naamini Dar, Arusha, Mwanza, Mbeya na miji mingine mikubwa kuna viwanda vya kutosha vya mikate, na ukisema uweke Dar, inakuchukua muda mrefu sana kuja kukopinti na watangulizi ambao wameisha kamata soko vya kutosha, na itakuhitaji kuwa na mtaji wa kutosha ili ufanye matangazo na lazima uwe na Distribution chanel za ukweli, so inahitaji capita ya uhakika.

  • MKUU SASA UFANYE NINI?
  • Mimi ningekushauri fanya utafiti wa kutosha katika miji mingine hapa Tanzania ambayo hakuna kiwanda cha hii kitu, na ukiona kuna demand fungua huko mkuu, ili uweze kukua vizuri, si razima Dar tu.

- Mkuu hata wawekezaji unao waona huku Africa wamekimbia stiff competition huko Ulaya, Marekani na Asia na kuja huku, mitaji yao haiwaruhusu kuendesha biashara huko kwao kwa sababu ya competition kubwa sana

- So hata sisi sometime ili kuepuka kutumia nguvu nyingi kufungua biashara kwenye miji mikubwa ambayo tiyali kuna business za aina hiyo nyingi tunaweza enda mikoani ambako tutatumia capital kidogo na ukisha kuwa unaweza rudi mjini kushindana na hao waliopo
DONDOO ZA MTAJI WA BAKERY NDOGO
Kuhusiana na Mtaji inategemeana unataka kutengeneza bidhaa gani na kwa kiwango gani kwa siku etc. Mfano kwa minimum hata 3 mill unaweza anaza kwa keki ndogo. Kwa kununua mixeer ya kg 5 kwa laki 9, Oven single deki ya 1.5 then laki sita ikawani pans na ingredients.

Vifaa vinavyohitajika kwa mradi wa bakery yaani unatengeneza wa keki, mikate, biscuits etc ni kama ifuatavyo commercial Oven, mixer mashine, slicer, improver, kabati, Pan/ filling, nozzels and mashine, decorations accesories, neckbag na vingine vidogo vidogo.

Maduka ya vifaa nayafahamu baadhi yako ambayo ni ya vifaa bei rahisi na mengine juu kidogo:

1. Maduka ya vifaa expensive ila vifaa vyao vina ubora wa hali ya juu. Duka la kwanza liko mtaa wa samora avenue inatazamana na PPF house, duka la pili liko posta mkabala na wizara ya sayansi na taknolojia na duka la tatu liko tazara veterani pale Penye petrol station. Haya. maduka vifaa vyao vinatoka UK, Turkey na baadhi ya nchi za Ulaya.

2. Vifaa vya at least bei rahisi ni kutoka China maduka ni moja liko Kariakoo mtaa wa agreey ukimaliza Bakhresa mbele kuja jengo lina hospitali. Pili ni maduka mawili yanatazamana na kituo cha mafuta Bigborn.

Nakaribisha uwanja wa maswali kwa jambo lolote kuhusiana na bakery.
VIFAA UNAVYOHITAJI NA USHAURI
Hapo kwenye sehemu ya kufanyia kazi (jengo) itabidi kwanza uwaone TFDA wakague kwanza jengo lako.
TFDA wana regulations zao kuhusu ramani na 'ubora' wa majengo ya bakery.

Waone hao ili watembelee jengo lako kabla hujawekeza. Watakuelekeza vizuri.

Ukianza kabla ya wao kuhakiki jengo lako, wakija na kukuta jengo lako halina 'ubora' watafunga bakery yako na kukuamuru urekebishe jego. Hii itakuwa ni hasara na gharama kubwa sana.

TFDA wakishapita, basi kila kitu ni rahisi kabisa.

Vifaa vya lazima kwenye bakery ni hivi hapa:

1.) Mixer (mashine ya kukandia mikate)

2.) Oven ya kuokea mikate

Baking_Equipment.jpg


3.) Slicer (Machine ya kukatia mikate)

bc20.jpg


4.) Proofer (Machine ya kuumulia mikate)

Proffer_Bakery_Prover_Bakery_Equipment.jpg
KUTENGENEZA MAANDAZI

Salute wakuu,

Natumaini wote mko poa.. Leo naomba ni-shee na nyie huu mradi mdogo kama jinsi watu wanavyoweza kuuona lkn kwa kiasi fulani unawaingizia watu mkwanja wa nguvu na wanalisha familia kama kawaida, sio lazima wewe uufanye huu mradi, la hashaa.

Ila unaweza kumshauri mtu akaufanya kupitia mawazo haya ama na wewe ukaboresha zaidi {mwisho wa huu uzi nimekuwekea file unaweza kulipakua na kujisomea ama kumuonesha mtu unayetaka afanye huu mradi} haya twende sasa

MRADI WA KUTENGENEZA MAANDAZI
Mradi huu utahusisha utengenezaji wa vitafunwa aina ya maandazi na kuyasambaza maduka mbali mbali kwa ajili ya kununuliwa na wateja. Hivi ni vitafunwa vinavyojulikana na wengi mijini na vijijni.

Vitafunwa hivi hutengenezwa na ngano inayouzwa madukani pamoja na mchangavyiko wa viungo vingine mahsusi. Ni mradi mdogo sana kwa kuutizama lakini kama ukifanywa kwa umakini unafaida kubwa na inaweza hata kumpatia mtengenezaji pesa nyingi.

Usambazaji
Kama nilivyoainisha awali kuwa hii biashara itafanyika kwa kuweka maandazi haya madukani {maduka ya kawaida kwa kuwaomba marafiki na hata kuwa na makubaliano fulani}. Kwa mfano hapa mtengenezaji atakuwa na madeli {makontena} madogo kumi {10 ama pungufu} ambayo kila moja wapo litakuwa na maadazi 100.

Yote haya yata wekwa maduka tofauti tofauti kwa makubaliano Fulani Fulani na muuzaji. Hapa ujanja wa kuweka maandazi ma2 ama ma3 kwa kila deli ili kumpatia muuzani nae atafute kama ujira wake. :):) ama unaweza kutafuta watu/madogo wakawa wanakuuzia mashuleni hasa shule za msingi n.k

Utengenezaji
Maandazi yatatengenezwa na msambazaji mwenyewe kwa mikono yake ili kuepuka gharama kubwa za uwekezaji huu. Vifaa vitanunuliwa humu humu ndani ya masoko yetu ili kuepuka gharama za uzalishaji na kujihakikishia faida kubwa.

Mbinu za kuyafanya yauzike.
Kwa sababu huu ni ujasiriamali makini, sasa ili kuifanya hii bidhaa iuzike ni muhimu kuwa mbunifu. Nazani inaeleweka kuwa vipo aina nyingi ya vitafunwa madukani vizuri tuu lakini ni vema kuyafanya maandazi haya yakauzika mapema na haraka ili kuufanya mzunguko wa biashara uwe mzuri na wa haraka zaidi.

Kwa mfano size ya andazi iwe ya kuridhisha kulingana na gharama za ununuzi wa bidhaa {kuepuka tamaa}, kuweka viungo ili angalau andazi liwe na harufu na radha ya kuvutia, kuweka tui la nazi, maandazi yakae katika hali ya usafi yaani yakae ndani ya deli linalo yaonesha {transparent} lililofunikwa na pia ili kuepuka mandazi yasiwe na unyevu nyevu ni vema deli likatobolewa matundu kiasi ili kupitisha hewa.

Ifutayo ni mchanganuo wa bajeti na mambo mengineyo ya jinsi ya kuifanya hii biashara kuwa na faida kubwa.
Gharama za awali,mchanganuo, faida na changamoto

Changamoto.
Bithaa hii ikiwa sokoni itakutana na bidhaa nyingine kama hizi, kwa hiyo ni vema ubunifu wa hali ya juu ukatumia ili kuifanya biashara hii kuwa ya kipekee na kupendwa na watu.

Mpango na idadi ya mauzo kwa siku,mwezi,mwaka na FAIDA katika mradi.
{WAKUU HAPA NAOMBA M-DOWNLOAD FILE NIMELIWEKA HAPO CHINI NAONA HAPA MAJEDWALI HAYAKAI VEMA}

MWISHO
Uzuri wa biashara hii ni kuwa haiitaji mtaji mkubwa saaaana yani hata laki nne haifiki kwa kuanzia. lakini pia unaweza kubuni mbinu ya kuyaweka maandazi yako mashuleni ambapo kama yakopoa madogo janja lazima wayanunue sana.

MWISHO KABISA
Ukiangalia kwenye hilo file labda kuna hesabu zimekosewa kwa njia moja ama nyingine lkn napenda kuwafungua macho watu waliokuwa wanaichukulia poa hii biashara, labda niwaambie mama yangu mzazi mimi kwa % Fulani kanilea mimi na ndugu zangu wengine kwa biashara ya maandazi.

Sasa wewe mdau ni kazi yako wewe kusuka ama kunyoa. Ikumbukwe huu mradi unaweza kuufaya na vijana wako home hata kama unafanya kazi kwa {DEREVA WA ROLI} ˂≈≈ Usini-quote tafadhali.

Nakaribisha
*maoni
*marekebisho
*matusi hapana {Sikaribishi}
*chochote

Salute Wakuu
VIFAA VYA MUHIMU KUWA NAVYO
1. Anatakiwa awe na oven hii kwa ajili ya kuchomea mikate.
2. Anatakiwa awe na mixer hii kwa ajili ya kuchanganya unga.
3. Anatakiwa awe na bread slicer hii ni kwa ajili ya kukatia mikate slesi.
4. Anatakiwa awe na profer hii ni machine kwa ajili ya kuimulia mikate.
5. Anatakiwa pia awe na hand sealing hii machine kwa ajili ya kufunga vibanio katika mfuko baada ya mkate kuingizwa katika mfuko wake.
6. Anatakiwa awe na vibati kwa ajili ya kuekea mikate katika oven.
 
Kuna ndugu ameniomba ushauri wa kununua vifaa vya bakery.

Naomba maelekezo ya vifaa umenunua wapi? Ni hapa nchini au umeagiza nje na je ni brand gani?

Usiwe na wasiwasi mkuu, pengine mimi ni mshindani, la hasha, hata hivyo Dar ni kubwa, kwenye soko kila mtu ana riziki yake.
 
Hongera sana! sasa kaza mwendo kuifanya kazi kwa bidii zote,utafanikiwa tu ,usihofu wala haihitaji others approval.Mungu awe nawe.tupe jina la hiyo sehemu,tuwe wateja.
 
Kuna ndugu ameniomba ushauri wa kununua vifaa vya bakery.

naomba maelekezo ya vifaa umenunua wapi? Ni hapa nchini au umeagiza nje na je ni brand gani?

Usiwe na wasiwasi mkuu, pengine mimi ni mshindani, la hasha, hata hivyo Dar ni kubwa, kwenye soko kila mtu ana riziki yake.

Newazz, vifaa vya bakery vinapatikana city center opposite na JMO building kwenye duka la BAJERYA. Bajerya ni brand name ya hizo vifaa. Ahsante kwa comments zako.
 
hongera sana! sasa kaza mwendo kuifanya kazi kwa bidii zote,utafanikiwa tu ,usihofu wala haihitaji others approval.Mungu awe nawe.tupe jina la hiyo sehemu,tuwe wateja.

Mutisya Mutambu, nashukuru sana kwa ushauri wako na baraka zako. Nitazifanyia kazi. Ahsante
 
Hongera sana kwa udhubutu wa kujaribu kufanya,,usiangalie kushindwa kamwe, kuwa na mtazamo chanya wa kushinda maana yote yanawezekana, jipange vizuri, angalia wengine walio kwenye hiyo biashara wanafanyaje na ujifunze kwao, buni njia binafsi za ushindani ili uweze kupenya kwenye soko na kushindana na nao, mtangulize MUNGU akupe busara, hekima, maarifa na nguvu ya kuendelea kufanya (persistence) hata utakapofikia pagumu, (put in mind that good idea, good plans, hardworking, perseverance and persistence will make you at the top of the ladder)
 
Hongera kaka kwa kudhubutu,kwani ni wachache wanaoweza kufanya hvyo.

Ushauri: jitahdi kutangaza biashara yako, pia tafuta masoko kwenye maduka madogo madogo na makubwa,kwani kuna kuwa na ugumu kuingza bidhaa mpya sokoni kwasababu maduka takribani yote yanatayari mali inayofanana ya zako, kwahyo pitia ktk maduka kwa kuchunguza wanauziwaje bidhaa kama yako ili wewe uweze kupunguza kidogo ili bidhaa yako iweze kuingia sokoni.

Then ujitahdi kutengeneza kitu cha tofauti na unaowakuta sokoni.

Ntarudi tena baadae.
 
Hongera kaka kwa kudhubutu,kwani ni wachache wanaoweza kufanya hvyo.

Ushauri: jitahdi kutangaza biashara yako, pia tafuta masoko kwnye maduka madogo madogo na makubwa,kwani kuna kuwa na ugumu kuingza bidhaa mpya sokoni kwasababu maduka takribani yote yanatayari mali inayofanana ya zako, kwahyo pitia ktk maduka kwa kuchunguza wanauziwaje bidhaa kama yako ili wewe uweze kupunguza kidogo ili bidhaa yako iweze kuingia sokoni.
Then ujitahdi kutengeneza kitu cha tofauti na unaowakuta sokoni.

Ntarudi tena baadae.

Huu ushauri ni wa great thinker. Naomba uuzingatie sana utafanikiwa
 
Short White hongera sana kwa kuamua kuwa mjasiriamali.

Bidii na kutokata tamaa ndiyo kitu cha msingi changamoto kwako zifanye mlango wa kupata fursa pia.

Ukiangalia bidhaa nyingi sana za kutoka Bakery, ikiwemo mikate, skonsi, keki na vinginevyo bado havijamlenga mtu wa kipato cha chini unaweza kubuni jinsi yakuwafikia hao ikiwa na pamoja kutengeza bidhaa watakazomudu, ikiwa ni kufungasha kwa kiasi fulani. Mfano mfuko wa skonsi unakuwa na skonsi kumi unaweza kufanya nusu yake, sina uhakika na eneo ulilopo lakini hapo ulipo unaweza pia kuuza bidhaa zako kwa kufungua duka, ikiwa na pamoja watu kupata mikate, skonsi fresh.

Chunguza ladha ya bidhaa nyingine za kutoka Bakery na watu wanapenda ladha ipi,kwani kuna watu wamepotea kwenye biashara hii kwa kuharibu ladha la bidhaa zao.

Huu ni mtazamo wangu,nakutakia kila la kheri katika kufanikisha ndoto zako.
 
Salaams JF,

Nilipata wazo la kuanzisha bakery maeneo ya sinza. Products ni ; Mikate, Maandazi na cakes aina mbalimbali. Sikuomba au kutafuta ushauri kwa mtu yeyote. Pia sijafanya research ya uhakika kuhusu mahitaji halisi ya hizo bidhaa ninazotaka kuingiza
You are already a business personality. Why going back, wanna be 'poor dad'?
 
Hongera kwa Kuthubutu.

kupata baker mzuri siyo jambo rahisi,ila inawezekana kumuiba mmoja kutoka ktk bakery nyingine,hapo inabidi utembelee bakery nyingine ujue average ya mishahara ,then uanze zoezi la kupata a good baker.uichukue unemployed baker, tafuta aliyekazini umuamishe.

2.distribution nzuri ni via watu wa baiskeli/pikipiki.hapo ukifanikiwa kinachobaki ni smiles all the way to the bank
 
Good Trial Mzee, Nadhani ni mwazo mzuri sana na kikubwa hapa ni ninavyoona Jf ilivyo msaada kwa kila kitu, kwa kweli hii ni home of Great Thinker hakuna kitu una-initiate then usipate walau Mchango wa mawazo utakaosaidia kwa namna moja ama nyingine.

My contribution:

Fanya Utafiti wa namna unavyoweza kuongeza uimara, Decorations na ubora wa packaging Material.
Ukifanikiwa kupata Graphics designer mzuri akakusaidia ku-design ile mifuko mizuri kwa maana ya mwonekano na hata ilawa tofauti na hii iliyozoeleka Naamini itakuwa ni Moja ya bao utakalopiga.

Ili kuwa tofauti na washindani wako unaowakuta sokoni, unaweza kuwa unaweka hata Kiasi kidogo sana (Ujazo wa Kijiko Kimoja kikubwa cha chakula) Blue band ambazo pia unaweza kuwa umeagiza special Order kwa Watengenezaji ikiwa na Logo yako then kwenye hiyo packaging ya kate unaweka hiyo Blue band yenye logo yako.
 
Kuna jamaa anaitwa Thomas mikate, yeye yupo DAR, anuaza mikate mingi sana kwa kutwa,ni rafiki yangu kwa uteja kwake.

- Hana brand wala Duka la mikate yeye anauzia ktk gari lake,ni suzuki mini van,kadogo hivi rangi ya blue na pia anayo nyeusi,huwa anapaki station opposite TRA offices ,jioni na pia huwa anakuwa maeneo ya posta karibu na CRDB holland house or ifm area.

Mwaka 2009 aliniambia kuwa anapata daily profit ya 140,000. na kuwa mikate yake huwa haibaki.jaribu kumtafuta atakushauri ni mtu muelewa,ila hapendi watu wa TRA(kodi etc) walishawahi kumsumbua ndio maana hana BRAND ya mikate yake,

Inasadikika kuwa bakressa wa Azam huwa ananunua mikate yake kwa matumizi yake na wajukuu zake.
 
Umesahau kitu kimoja mkuu, sasa nikuchapa kazi kwa nguvu zote, high supervision bila kuleta mchezo especiallly kwa vijana wakowa kazi, pesa imeshatoka inatakiwa irudu na faida sinza ni good location, watu wa sinza hawapiki bwana utawapata tu. usisahahu na kuwawekea ka cafe kwa ajri ya chai.
 
Naomba ushauri,

Tuna kikundi chetu cha kina mama na tunataka kuanzisha project ya bakery, Please naomba ushauri ya makadirio ya gharama ya kuanzia,Kama inawezekana orodha ya vifaa vinavyoitajika ili kutuwezesha kuanza project yetu.

Natanguliza shukrani.
 
Back
Top Bottom