Biashara na mahusiano hayatanitesa kweli?

Biashara na mahusiano hayatanitesa kweli?

Hatari kwa upande upi?
Kwa nionavyo kwa upande wako, watu wanabadilika Mkuu, alafu ushauri wangu kuwa makini manake kama na duka ushafungua. Mchepuko huo ukishapata mtoto na wewe utaanza kunyanyua mabega na kujilinganisha na huyo (wife material wako kama ulivyomuita.) mwisho wa siku matokeo hayatakuwa mazuri.
 
Bahati nzuri hiki ninachokianzisha kitakuwa chini ya mimi na mke wangu, ila huyu mchepuko ataonekana muajiriwa ingawa atakuwa anajilipa vizuri kutokana na faida inayopatikana.
Kwangu nimeona ni fursa kwa sababu ana muda wa kusimamia na kuhakikisha pesa inapatikana.
Muhimu zaidi mi naona, ni bora kuweka mifumo ya kumdhibiti pale atakapotamani kudokoa dokoa​
Yaani wewe mke wako mchepuko wote mko ofisi moja 😆
 
Vyote mkuu
Tukiweka uzani unaonekana ulitumia KICHWA cha CHINI zaidi kufikiri kuliko KICHWA cha JUU ungetumia KICHWA cha JUU zaidi kufikiri usingemtia Mimba huku unajua fika una Mwanamke Mwingine ambae ndio unataka umuite MY WIFE, nakuambia umejivalisha BOM la Muda wakati ukifika litalipuka
 
Ila sisi wanawake tunakazi sana, unajua kabisa mtu anakutreat kama option tena bado unajiongeza na mawazo ya biashara mara sijui nini nini mwisho wa siku anaenda kufanya na mke wake unabaki unashangaa shangaa.. . Ukishakua option make sure unakua option kweli kweli hakuna kujipendekeza wewe akupe tu hela na utamu,. Mambo yako mengine hatakiwi kuyafahamu tena kwake ujifanye mjinga kweli kweli ukiwa unajipigia zako mpunga kimyakimya..

Jinga sana huyo mchepuko wako😬😬

Nb. Mimi sina character za uchepuko, nimetoa tu ushauri
Kwa kweli hata mimi amenifikirisha, yaani niwafanyie kazi yeye na mkewe na familia yake khaaaa kama yupo sharp hivyo si angeomba tu mtaji afanye yeye kama yeye ... women 😡
 
kwanza yeye atakua na vyeo vifuatavyo
Assistance CEO
business operator
accountant
Sells manager

Nyanja muhim zote ameshika yeye cha kwako mtaji tu
"Money bring bitches"
Uko sahihi, ndio maana nimefikiria kuweka mtu mwingine kwa ajili ya kusimamia mauzo
 
Tukiweka uzani unaonekana ulitumia KICHWA cha CHINI zaidi kufikiri kuliko KICHWA cha JUU ungetumia KICHWA cha JUU zaidi kufikiri usingemtia Mimba huku unajua fika una Mwanamke Mwingine ambae ndio unataka umuite MY WIFE, nakuambia umejivalisha BOM la Muda wakati ukifika litalipuka
Ebu fafanua zaidi mkuu
 
Kwa kweli hata mimi amenifikirisha, yaani niwafanyie kazi yeye na mkewe na familia yake khaaaa kama yupo sharp hivyo si angeomba tu mtaji afanye yeye kama yeye ... women 😡
Yeye sio mchoyo kama nyie, ameamua kunipa fursa akiwa na malengo naye huko mbeleni atapata vya kwake na maisha yasogee
 
Ebu fafanua zaidi mkuu
Soma Comment za Wanawake wa JF wanakufafanulia nini kitajiri baadae yaan wanakupa picha mapema, cha kwanza utaambiwa yaan Mimi nikufanyie kazi wewe na Mkeo kwani Mimi sijakuzalia Mtoto?
 
Ila bado unautoto mwingi sana.

Rudia hayo uliyoyaandika kwenye hii post yako utagundua umezingua pamoja na kuitwa babu.
Ukiwa mjasiriamali usiogope 'risk'; wapo wafanyabiashara wamewamilikisha michepuko yao kampuni n.k kutokana na umuhimu wa kuwafanya wafanikiwe.
 
Yeye sio mchoyo kama nyie, ameamua kunipa fursa akiwa na malengo naye huko mbeleni atapata vya kwake na maisha yasogee
HAO viumbe wanabadirika na Muda Muda huu atakwambia hivi kuna Muda utafika hakuna 50/50 atataka 100
 
Back
Top Bottom