GLOBAL CITIZEN
JF-Expert Member
- Jun 5, 2014
- 767
- 1,655
Wakuu, ngoja nianze kutiririka bila kupoteza muda.
1 • Digital marketing agency.
There so much money to be made in this area.
Kwa ufupi ni business itakayofanya vizuri kwa miaka nyingi sana sana kwasababu siku zote wamiliki wa biashara wanatafuta watu waliobobea kuwasaidia kupata wateja wa bidhaa au huduma wanazouza.
Sasa kama wewe unauwezo wakuchanga karata zako vizuri na kuanzisha digital marketing agency utakuwa vizuri sana 2021.
2 • Kumiliki Online Store inayouza bidhaa ndani na nnje ya nchi.
Sababu hapa ni kuimarika kwa mifumo ya malipo ya kimtandao. Kwa mfano sasa hivi hata usipokuwa na bank account unaweza kutengeneza virtual bank account kwa kutumia SIM card yako ya Vodacom, Tigo au Airtel. Ukiwa na hii vurtual card utaweza kuweka pesa na kununua chochote unachotaka mtandaoni.
Sasa tunapoelekea watanzania nao watazoea haya. Pesa nyingi itamiminika hapa. I’m telling you.
3 • Tourism
Watanzania sisi nchi yetu imejaliwa tourists attractions nyingi. Kuanzia utamaduni wa watu wetu hadi mbuga zetu za wanyama, mito, bahari, misitu na maziwa.
Kwasababu corona inaisha hiyo maana yake mwakani tourism inaenda kusimama tena.
Muhimu tusifanye tourism kimazoea.
Wiki iliyopita nilienda camping trip kuona indigenous bribes lake eyasi. Nilikuwa na wageni wangu toka United States. Hii trip ilikuwa nzuri sanaaaaa. Wageni wali rate *5. Na nilichofanya ni kwanza kuifanya trip hii iwe memorable kwao. Kwamba naprovide good service zaidi na walivyotarajia.
Pesa ipo sana kwenye tourism tukizidi kuwa wabunifu. Kwahiyo ukiwa na pesa na unaelewa unachofanya unaweza wekeza hapa.
4 • Restaurant yakuuza healthy food kwenye mji mkubwa, Arusha, Dar, Mwanza, etc.
Wakuu, sasa hivi watu wangi wanapendelea healthy food. Binafsi mimi ni vegan for many many years. Maana yake situmii product yoyote inayotokana na mnyama.
Sasa nilichoona watu wengi wanahamia huku. Ukiweza kuwekeza ukafungua modern restaurant kwenye mji mkubwa kama hapa Arusha na unaandaa vyakula vitamu tena heathy? Trust me utapiga sana pesa hapa. Ukiwa Arusha mimi nitakuwa mteja wako nambari one.
5 • Real Estate
Kwa mfano hapa Arusha real estate (viwanja, nyumba za kunua/kupangisha) bei inakwenda juu kila mwezi. Hapa unaweza anza taratibu kama agent baadaye ukipata pesa zaidi unaanza na wewe kununua real estate.
6 • Affiliate Marketing
Covid 19 imechangia pakubwa kubadili tabia za watu wanaonunua mtandaoni.
Katika kipindi hiki cha covid 19 watu wengi wamekuwa tayari au niseme wamekuwa comfortable kununua online bila woga.
Sasa hapa kuna opportunity.
Na ndiyo hii affiliate marketing.
Kwa wasiofahamu affiliate marketing ni biashara ya kupromote bidhaa za wengine mtandaoni na wewe kulipwa commission kwa kila mtaja atakaye nunua kupitia wewe.
Kwa kawaida kabla hujaanza affiliate marketing business inabidi kwanza ufanye mawasiliano/application na mzalishaji wa bidhaa unayotaka kumsaidia ku-promote ili ukiuza ulipwe promotion. Sasa kwasababu hii bisiness utakuwa unafanyia online basi utapatiwa special link inayokutumblisha ni wewe ndiye umemleta mtaja kila mara mteja atakapo click hiyo link unayotumia kupromote bidhaa husika.
Kwa hii business model inawezekana sana tu Tz na kwa mwaka 2021 watu watakaokuwa serious na hii business watatengeneza pesa.
Lakini niseme hapa lazima ujipange.
Unahitaji uwe na review website ambayo affiliate marketer wa kawaida itamchukua miaka mingi kufanya unachofanya.
Hii si ku-copy na ku-paste links kwenye groups za Facebook na Whatsapp. Hizo ni mambo za watoto.
Affiliate Marketing ni big money industry. Na inafanyika kwa umakini wa hali ya juu.
7 • Online Business Consulting
Hapa napo kuna pesa.
Watu wengi sana sana wanatafuta namna watakavyosaidiwa kuanzisha au kukuza Online Business. Sasa ukiwa vizuri hapa pesa zote zitakuja kwako.
8 • Fixer
Wakuu, mwaka 2021 watu wengi watapitia misukosuko kama inavyokuwa miaka yote. Sasa hapa kama wewe ni mtu wakuweza kutatua changamoto za watu bila kujali ni zakibinafsi basi nakwambia utatengeneza sana pesa.
Mbinu hapa ni kuwa na connection na watu au familia zenye pesa mjini kwako. Itabidi ujiweke kuwa wewe ni mtu unayeweza kufanikisha lolote wanalohitaji.
Unajua watu wengi wenye pesa wapo na mambo mengi yakufanikishiwa. Kuanzia halali au haramu. Uchaguzi ni wako.
9 • Kilimo cha mbogamboga bila kutumia dawa zenye sumu.
Zipo high end hotels pia restaurants zinazohitaji mbogamboga zisizotiwa dawa zenye sumu.
Sasa hapa kama utakuwa vizuri ukafanya research ukaingia mkataba waku-supply mbogamboga kwenye hotels hizi nakwambia utatengeneza pesa nzuri sana bila kuwaza. Kama nilivyosema fanya research kwanza.
10 • Plambing services
Wakuu hii business yakutengeneza au kuweka sawa miundombinu ya maji au waliwato majumbani kwa watu ni Business nzuri sana.
Lakini inabidi uifanye kisasa na uwe na vifaa na vijana wanaofahamu kufanya hii kazi.
Kipindi hiki waTz wengi wanaishi kwenye nyumba au apartment zenye miundombinu hii sasa ikiharibika hawafahamu nani hasa atawatengenezea.
Mfano leo heater bafuni kwangu imegoma kufanya kazi imebidi nimpigie jamaa ana kampuni yake hapa Arusha ametuma kijana haraka amefanya kazi na nimelipa. Sasa kwa mji mkubwa kama Arusha na ukijiweka vizuri na kutangaza kampuni yako utakuwa vizuri sana.
11 • Online tutoring
Je, una Skills yoyote unayodhani unaweza kumfundisha mtu mwingine? Binafsi ninaweza kukusaidia jinsi yakufanikisha hili kwamaana ya kufahamu namna gani unaweza kuwa na Online classes na ukafundisha kwa kiwango cha juu kabisa ukitumia teknolojia.
Hii ni opportunity nzuri sana kwasababu mwaka 2021 watanzania wengi watakuwa na njaa ya maarifa kwasababu watu wanazidi kufahamu Ukiwa na rights skills zinazohitajika hasahasa mtandaoni basi unaweza kutengeneza pesa. Sasa wewe kama unafahamu let say designing, photography, coding, copy writing, cooking, kwanini usitumie hizi Skills kufundisha wengine na kutengeneza more money?
12 • Biashara ya vifaa vya ujenzi.
Miji mingi ya Tanzania inakuwa kwa haraka. Kwa uhakika kabisa takwimu zionaonyesha sekta ya ujenzi itaendele kufanya vizuri 2021. Sasa kama unamtaji wakutosha ukianzisha Store yakuuza vifaa vya ujenzi lazima utapiga pesa. Kama kawada fanya kwanza research kabla hujaweka pesa zako. Inabidi ufahamu kasi ya ujenzi katika mji wako na wapi uweke store hapo mjini.
13 • Kampuni ya ujenzi.
Kama wewe upo vizuri kwenye mambo ya ujenzi au unauwezo wakuwaleta pamoja mafundi ujenzi wenye weledi mzuri pia una vifaa basi utaweza kupata deals nyingi zakujenga nyumba za watu au project fulani za mashirika hapa Tz. Inategemea uwezo na mtaji ulio nao, hatahivyo.
14 • Kuaandaa Matamasha ya Burudani.
Wait,
Burudani? Really?
Yes, hii kitu ukifanya kwa ubunifu inakutoa 2021.
Mwezi wa 9 nilikutana na dada mmoja yeye anaandaa matamasha kubwa kwaajili ya kukutanisha watu wapate good time. Kwa huku kaskazini analenga kipindi cha December watu wanakuja mapumziko sasa yeye anatumia Hii opportunity kuandaa matamasha na niseme tu watu wana-respond vizuri sana.
Labda nikupe mfano unaofahamika na watu wengi. Matamasha ya burudani yanayoandaliwa na Clouds media group. Haya matamasha yanatengeneza pesa nyingi sana. Lakini wewe kwasababu unaanza huitaji kuandaa kwa ukubwa wa Clouds Media Group. Unaweza ukaanza na mkoani kwako. Hapa inabidi ufanye kazi kwa karibu na kampuni za vinjwaji kama vile makampuni ya vijwaji baridi au wazalishaji wa pombe.
Haya makampuni siku zote yanakaribisha wajasiriamali wanaoweza kufanya hizi mambo. Makampuni haya yanapata faida pia kwasababu katika makubaliano lazima wao ndiyo watakuwa wauzaji wa vinjwaji katika tamasha unaloandaa.
Sasa mtu wangu hapo unaona, kama upo na kichwa kizuri, unaweza ku-organize watu kufanikisha hili basi 2021 utakuwa vizuri.
Ok, kwa leo niishie hapa.
Tuonane wakati mwingine
Tuwasiliane makingmoneyonlinetz@gmail.com
Cheers 🥂
1 • Digital marketing agency.
There so much money to be made in this area.
Kwa ufupi ni business itakayofanya vizuri kwa miaka nyingi sana sana kwasababu siku zote wamiliki wa biashara wanatafuta watu waliobobea kuwasaidia kupata wateja wa bidhaa au huduma wanazouza.
Sasa kama wewe unauwezo wakuchanga karata zako vizuri na kuanzisha digital marketing agency utakuwa vizuri sana 2021.
2 • Kumiliki Online Store inayouza bidhaa ndani na nnje ya nchi.
Sababu hapa ni kuimarika kwa mifumo ya malipo ya kimtandao. Kwa mfano sasa hivi hata usipokuwa na bank account unaweza kutengeneza virtual bank account kwa kutumia SIM card yako ya Vodacom, Tigo au Airtel. Ukiwa na hii vurtual card utaweza kuweka pesa na kununua chochote unachotaka mtandaoni.
Sasa tunapoelekea watanzania nao watazoea haya. Pesa nyingi itamiminika hapa. I’m telling you.
3 • Tourism
Watanzania sisi nchi yetu imejaliwa tourists attractions nyingi. Kuanzia utamaduni wa watu wetu hadi mbuga zetu za wanyama, mito, bahari, misitu na maziwa.
Kwasababu corona inaisha hiyo maana yake mwakani tourism inaenda kusimama tena.
Muhimu tusifanye tourism kimazoea.
Wiki iliyopita nilienda camping trip kuona indigenous bribes lake eyasi. Nilikuwa na wageni wangu toka United States. Hii trip ilikuwa nzuri sanaaaaa. Wageni wali rate *5. Na nilichofanya ni kwanza kuifanya trip hii iwe memorable kwao. Kwamba naprovide good service zaidi na walivyotarajia.
Pesa ipo sana kwenye tourism tukizidi kuwa wabunifu. Kwahiyo ukiwa na pesa na unaelewa unachofanya unaweza wekeza hapa.
4 • Restaurant yakuuza healthy food kwenye mji mkubwa, Arusha, Dar, Mwanza, etc.
Wakuu, sasa hivi watu wangi wanapendelea healthy food. Binafsi mimi ni vegan for many many years. Maana yake situmii product yoyote inayotokana na mnyama.
Sasa nilichoona watu wengi wanahamia huku. Ukiweza kuwekeza ukafungua modern restaurant kwenye mji mkubwa kama hapa Arusha na unaandaa vyakula vitamu tena heathy? Trust me utapiga sana pesa hapa. Ukiwa Arusha mimi nitakuwa mteja wako nambari one.
5 • Real Estate
Kwa mfano hapa Arusha real estate (viwanja, nyumba za kunua/kupangisha) bei inakwenda juu kila mwezi. Hapa unaweza anza taratibu kama agent baadaye ukipata pesa zaidi unaanza na wewe kununua real estate.
6 • Affiliate Marketing
Covid 19 imechangia pakubwa kubadili tabia za watu wanaonunua mtandaoni.
Katika kipindi hiki cha covid 19 watu wengi wamekuwa tayari au niseme wamekuwa comfortable kununua online bila woga.
Sasa hapa kuna opportunity.
Na ndiyo hii affiliate marketing.
Kwa wasiofahamu affiliate marketing ni biashara ya kupromote bidhaa za wengine mtandaoni na wewe kulipwa commission kwa kila mtaja atakaye nunua kupitia wewe.
Kwa kawaida kabla hujaanza affiliate marketing business inabidi kwanza ufanye mawasiliano/application na mzalishaji wa bidhaa unayotaka kumsaidia ku-promote ili ukiuza ulipwe promotion. Sasa kwasababu hii bisiness utakuwa unafanyia online basi utapatiwa special link inayokutumblisha ni wewe ndiye umemleta mtaja kila mara mteja atakapo click hiyo link unayotumia kupromote bidhaa husika.
Kwa hii business model inawezekana sana tu Tz na kwa mwaka 2021 watu watakaokuwa serious na hii business watatengeneza pesa.
Lakini niseme hapa lazima ujipange.
Unahitaji uwe na review website ambayo affiliate marketer wa kawaida itamchukua miaka mingi kufanya unachofanya.
Hii si ku-copy na ku-paste links kwenye groups za Facebook na Whatsapp. Hizo ni mambo za watoto.
Affiliate Marketing ni big money industry. Na inafanyika kwa umakini wa hali ya juu.
7 • Online Business Consulting
Hapa napo kuna pesa.
Watu wengi sana sana wanatafuta namna watakavyosaidiwa kuanzisha au kukuza Online Business. Sasa ukiwa vizuri hapa pesa zote zitakuja kwako.
8 • Fixer
Wakuu, mwaka 2021 watu wengi watapitia misukosuko kama inavyokuwa miaka yote. Sasa hapa kama wewe ni mtu wakuweza kutatua changamoto za watu bila kujali ni zakibinafsi basi nakwambia utatengeneza sana pesa.
Mbinu hapa ni kuwa na connection na watu au familia zenye pesa mjini kwako. Itabidi ujiweke kuwa wewe ni mtu unayeweza kufanikisha lolote wanalohitaji.
Unajua watu wengi wenye pesa wapo na mambo mengi yakufanikishiwa. Kuanzia halali au haramu. Uchaguzi ni wako.
9 • Kilimo cha mbogamboga bila kutumia dawa zenye sumu.
Zipo high end hotels pia restaurants zinazohitaji mbogamboga zisizotiwa dawa zenye sumu.
Sasa hapa kama utakuwa vizuri ukafanya research ukaingia mkataba waku-supply mbogamboga kwenye hotels hizi nakwambia utatengeneza pesa nzuri sana bila kuwaza. Kama nilivyosema fanya research kwanza.
10 • Plambing services
Wakuu hii business yakutengeneza au kuweka sawa miundombinu ya maji au waliwato majumbani kwa watu ni Business nzuri sana.
Lakini inabidi uifanye kisasa na uwe na vifaa na vijana wanaofahamu kufanya hii kazi.
Kipindi hiki waTz wengi wanaishi kwenye nyumba au apartment zenye miundombinu hii sasa ikiharibika hawafahamu nani hasa atawatengenezea.
Mfano leo heater bafuni kwangu imegoma kufanya kazi imebidi nimpigie jamaa ana kampuni yake hapa Arusha ametuma kijana haraka amefanya kazi na nimelipa. Sasa kwa mji mkubwa kama Arusha na ukijiweka vizuri na kutangaza kampuni yako utakuwa vizuri sana.
11 • Online tutoring
Je, una Skills yoyote unayodhani unaweza kumfundisha mtu mwingine? Binafsi ninaweza kukusaidia jinsi yakufanikisha hili kwamaana ya kufahamu namna gani unaweza kuwa na Online classes na ukafundisha kwa kiwango cha juu kabisa ukitumia teknolojia.
Hii ni opportunity nzuri sana kwasababu mwaka 2021 watanzania wengi watakuwa na njaa ya maarifa kwasababu watu wanazidi kufahamu Ukiwa na rights skills zinazohitajika hasahasa mtandaoni basi unaweza kutengeneza pesa. Sasa wewe kama unafahamu let say designing, photography, coding, copy writing, cooking, kwanini usitumie hizi Skills kufundisha wengine na kutengeneza more money?
12 • Biashara ya vifaa vya ujenzi.
Miji mingi ya Tanzania inakuwa kwa haraka. Kwa uhakika kabisa takwimu zionaonyesha sekta ya ujenzi itaendele kufanya vizuri 2021. Sasa kama unamtaji wakutosha ukianzisha Store yakuuza vifaa vya ujenzi lazima utapiga pesa. Kama kawada fanya kwanza research kabla hujaweka pesa zako. Inabidi ufahamu kasi ya ujenzi katika mji wako na wapi uweke store hapo mjini.
13 • Kampuni ya ujenzi.
Kama wewe upo vizuri kwenye mambo ya ujenzi au unauwezo wakuwaleta pamoja mafundi ujenzi wenye weledi mzuri pia una vifaa basi utaweza kupata deals nyingi zakujenga nyumba za watu au project fulani za mashirika hapa Tz. Inategemea uwezo na mtaji ulio nao, hatahivyo.
14 • Kuaandaa Matamasha ya Burudani.
Wait,
Burudani? Really?
Yes, hii kitu ukifanya kwa ubunifu inakutoa 2021.
Mwezi wa 9 nilikutana na dada mmoja yeye anaandaa matamasha kubwa kwaajili ya kukutanisha watu wapate good time. Kwa huku kaskazini analenga kipindi cha December watu wanakuja mapumziko sasa yeye anatumia Hii opportunity kuandaa matamasha na niseme tu watu wana-respond vizuri sana.
Labda nikupe mfano unaofahamika na watu wengi. Matamasha ya burudani yanayoandaliwa na Clouds media group. Haya matamasha yanatengeneza pesa nyingi sana. Lakini wewe kwasababu unaanza huitaji kuandaa kwa ukubwa wa Clouds Media Group. Unaweza ukaanza na mkoani kwako. Hapa inabidi ufanye kazi kwa karibu na kampuni za vinjwaji kama vile makampuni ya vijwaji baridi au wazalishaji wa pombe.
Haya makampuni siku zote yanakaribisha wajasiriamali wanaoweza kufanya hizi mambo. Makampuni haya yanapata faida pia kwasababu katika makubaliano lazima wao ndiyo watakuwa wauzaji wa vinjwaji katika tamasha unaloandaa.
Sasa mtu wangu hapo unaona, kama upo na kichwa kizuri, unaweza ku-organize watu kufanikisha hili basi 2021 utakuwa vizuri.
Ok, kwa leo niishie hapa.
Tuonane wakati mwingine
Tuwasiliane makingmoneyonlinetz@gmail.com
Cheers 🥂