Amanijua
JF-Expert Member
- Mar 7, 2014
- 1,776
- 1,632
WELL SAID MKUU.Hujui unachokizungumza.
Ngoja nikupe limu kidogo kwa kukujibu kwa hoja kabisa ili uelewe biashara hii ilivyo halali.
Je, Biashara halali ni ipi? Biashara halali ni ile ambayo ipo kwa mujibu wa sheria za nchi, kama nchi kupitia serikali imeridhia na kuruhusiwa kuendeshwa nchini humo basi hiyo biashara ni halali. Hii pia huambatana na usajili pamoja na utambuzi.
Kubeti (betting) inatambulika rasmi nchini na ipo chini ya Tanzania Gambling Board.
Twende kwenye hoja zako;
1. Unajua maana ya Odds? Hiyo ndiyo thamani halisi ya Betting slip yako. Kama hujui kajisomee ili ujue maana yake. Ukiangalia uwiano wa kutokea kwa Ubashiri wako, bila shaka zinalandana. Endapo timu itaonekana kuwa na uwezekano Mkubwa wa kushinda ndivyo hivyo mtu atakapokuwa na kiasi kidogo cha kubashiri na kushinda.
2. Betting kama ilivyo biashara zingine na uwekezaji, ni biashara yenye risk kubwa sana kulinganisha na biashara zingine nyingine. Kutokana na kuwa na risk kubwa pia ina higher rate of return. Sasa uhalali wa hoja yako ya kusema kuwa betting inadanganya vijana kuwa ni rahisi i wapi?
3. Mwanzoni kabisa nimekuambia kuwa hujui unachokizungumza na ndiyo maana hujui ninkwa kiasi gani watu wanavyohangaika kuangalia katika predicting sites na kuangalia uwezekano wa kupatia katika ubashiri. Kuangalia rekodi za timu zinapokutana, kuangalia nafasi ya timu katika ligi, kuangalia idadi ya mechi zzilizoshinda na hata kuhusisha utabiri wa nyota ya timu husika ni njia za kufanikisha ubashiri uwe mubashara na mkeka ukubali.
4. Ukiliwa ni faida kwa aliyewekeza (mwenye betting) na ukila ni faida kwako. Huwezi tu from no where ukaanzisha kampuni ya kubet. Lazima uwe na mtaji ili ukiliwa hata kabla hujaingiza watu waweze kupata fedha zao. Kwa hiyo nadharia yako ya kusema kuwa ni ukusanyaji kwa ajili ya watu wachache ni Uongo . Alafu pia, mbona kuna kampuni za betting zinafilisika baada ya kuliwa tu? Tulia hapo acha biashara ifanyike.
Na kwa kumsaidia huyu MAKRITA ni kwamba kwa Tanzania ili usajili kampuni ya Betting lazima uwe na mtaji wa Shilingi Bilioni MBILI au zaidi.