Betting sio biashara halali

Betting sio biashara halali

Nenda thailand uone watu wakibet kwa mchezo wa kuku kupigana na vibosile wako wanabet tembea ujionee.
 
Mtoa mada leo kazi unayo, sijui kama utapata mtu wa kukusapoti, watu wameshakua addicted na huo uchafu

Sitafuti kusapotiwa, ila naeleza ukweli kama ulivyo.
Siku wakiamka usingizini, watayaelewa haya.
 
Juzi SOUTH AFRICA KUNA JAMAA AMEPATA PESA AMBAYO UKILINGANISHA NA SHILINGI YA TANZANIA NI MILIONI 980.

SASA MAKRITA AMANI NIAMBIE WEWE KATIKA SHUGHULI ZOTE UNAZOFANYA ZA KUKUINGIZIA KIPATA ULISHAWAHI KUPATA KIASI KAMA HICHO????

Naamini hujawahi na pengine hutakuja kupata.

Fanya zoezi moja dogo sana;

Toka umeanza kufanya kazi yako inayokuweka mjini mpaka Leo hii ni kiasi gani ulichoweza kusave??..
Katika huyo mmoja aliyepata kiasi hicho, ni wangapi ambao wameliwa?
Maana huwa mnachukua hadithi ya mtu mmoja na kuacha wengi ambao wanaliwa.
 
Hujui unachokizungumza.

Ngoja nikupe limu kidogo kwa kukujibu kwa hoja kabisa ili uelewe biashara hii ilivyo halali.

Je, Biashara halali ni ipi? Biashara halali ni ile ambayo ipo kwa mujibu wa sheria za nchi, kama nchi kupitia serikali imeridhia na kuruhusiwa kuendeshwa nchini humo basi hiyo biashara ni halali. Hii pia huambatana na usajili pamoja na utambuzi.

Kubeti (betting) inatambulika rasmi nchini na ipo chini ya Tanzania Gambling Board.

Twende kwenye hoja zako;
1. Unajua maana ya Odds? Hiyo ndiyo thamani halisi ya Betting slip yako. Kama hujui kajisomee ili ujue maana yake. Ukiangalia uwiano wa kutokea kwa Ubashiri wako, bila shaka zinalandana. Endapo timu itaonekana kuwa na uwezekano Mkubwa wa kushinda ndivyo hivyo mtu atakapokuwa na kiasi kidogo cha kubashiri na kushinda.

2. Betting kama ilivyo biashara zingine na uwekezaji, ni biashara yenye risk kubwa sana kulinganisha na biashara zingine nyingine. Kutokana na kuwa na risk kubwa pia ina higher rate of return. Sasa uhalali wa hoja yako ya kusema kuwa betting inadanganya vijana kuwa ni rahisi i wapi?

3. Mwanzoni kabisa nimekuambia kuwa hujui unachokizungumza na ndiyo maana hujui ninkwa kiasi gani watu wanavyohangaika kuangalia katika predicting sites na kuangalia uwezekano wa kupatia katika ubashiri. Kuangalia rekodi za timu zinapokutana, kuangalia nafasi ya timu katika ligi, kuangalia idadi ya mechi zzilizoshinda na hata kuhusisha utabiri wa nyota ya timu husika ni njia za kufanikisha ubashiri uwe mubashara na mkeka ukubali.

4. Ukiliwa ni faida kwa aliyewekeza (mwenye betting) na ukila ni faida kwako. Huwezi tu from no where ukaanzisha kampuni ya kubet. Lazima uwe na mtaji ili ukiliwa hata kabla hujaingiza watu waweze kupata fedha zao. Kwa hiyo nadharia yako ya kusema kuwa ni ukusanyaji kwa ajili ya watu wachache ni Uongo . Alafu pia, mbona kuna kampuni za betting zinafilisika baada ya kuliwa tu? Tulia hapo acha biashara ifanyike.
Majibu yako ni tofauti na maswali niliyouliza, na hata maelezo niliyotoa.
Sikuomba nifafanuliwe kuhusu betting,
Bali jibu swali la msingi; NI THAMANI IPI INATENGENEZWA KWENYE BETTING?
 
Unaingilia faragha za watu hizi ni starehe zetu jamani. Mimi si mpenzi wa beer wala wanawake lakini ni mpenzi wa gambling. Matajiri wote unaowajua wamewekeza kwenye bet na wana bet.
Katika orodha ya matajiri wakubwa duniani, africa na hata tanzania, hebu nitajie waliofika pale kwa kutumia betting, ili tuwatumie kama mfano kuwashawishi watoto wetu wakazane na kubet zaidi.
 
Katika orodha ya matajiri wakubwa duniani, africa na hata tanzania, hebu nitajie waliofika pale kwa kutumia betting, ili tuwatumie kama mfano kuwashawishi watoto wetu wakazane na kubet zaidi.
Sijasema walipata utajiri kwa kubet bali huo ni mchezo wao pendwa na wao ndyo walioanzisha na wanahisa na kuidhamini hyo michezo nenda las vegas marekani ujionee lile ni jiji la michezo ya kubashiri. Maana ya mchezo ni ule ama uliwe au ushinde au ushindwe.
 
Kwa wale wote wanaotetea Beting kama BIASHARA HALALI, nasema siyo. Na haijalishi kama serikali imeruhusu au la, swala ni kwamba hii siyo biashara halali kwa sababu zifuatazo;

1. Hakuna thamani inayotengenezwa. Biashara yoyote halali na yenye manufaa kwa kila mtu, kuna thamani ambayo inatengenezwa. Hivyo kuna kubadilishana fedha kwa thamani. Una njaa unakwenda kwa anayeuza chakula, unampa fedha anakupa chakula, hapo kuna thamani imebadilishwa. Sasa niulize thamani gani inatengenezwa kwenye beting?

2. Beting inawadanganya vijana kwamba zoezi la kupata fedha n rahisi sana, ukae tu na kubashiri matokeo halafu unapata fedha nyingi. Fedha haijawahi kuwa rahisi kiasi hicho, na hapa tunatengeneza taifa la watu wavivu, wasio tayari kuweka juhudi kubwa kwenye kazi inayozalisha thamani. Badala yake wanatafuta njia ya mkato ya kupata fedha, ambayo siyo ya uhakika.

3. Hakuna juhudi zozote mtu anaweza kufanya kwenye beting kuongeza uwezekano wa yeye kupata anachotaka. Kwa mfano kama wewe unauza nguo, na biashara siyo nzuri, unaweza kuongeza juhudi zaidi kwa kuwafikia wateja zaidi ili kuuza. Au unaweza kuongeza bidhaa nyingine kuongeza mauzo. Lakini kwenye beting hilo halipo, ukishatabiri timu A itashinda, huwezi kuingia uwanjani kuhakikisha inashinda, unabaki tu kuombea ishinde, na maombi siyo mkakati wa kupata unachotaka.

4. Beting ni wizi wa kihalali. Anayebashiri na kupatia, anapewa fedha, lakini jiulize hizi fedha zinatoka wapi? Zinatoka kwa wengine ambao wameshindwa. Kwa hiyo kwa kifupi, beting ni kukusanya fedha kwa watu wengi, kuwapa wachache na nyingine ikawa faidia kwa anayechezesha hiyo betting.

5. Beting inaleta uteja, mwanzoni watu huanza taratibu na kuona ni kitu kidogo tu, baadaye wanajikuta wamekuwa wategemezi wa beting na hawawezi kuacha. Inafika hatua mtu anaiba ili aende akabet, au anauza vitu vyake cya thamani ili apate fedha ya kubet.

Nimalize kwa kuwashauri vijana wenzangu kwamba betting siyo biashara halali, na wala siyo mkakati wa kupata fedha. Fedha zinapatikana kwa kufanya kazi, inayoongeza thamani kwa wengine. Kuruhusiwa kwa hii beting na serikali hakuifanyi kuwa halali, kwa sababu mara nyingi serikali huwa haioni madhara ya vitu hivi kwa haraka, yenyewe inafurahia kukusanya kodi. Kwenye nchi nyingine beting inafanyika kwenye maeneo maalumu, kwa sababu inachukuliwa kama sehemu ya starehe na siyo mkakati wa kutengeneza fedha. Ila hapa kwetu beting inafanyika kila mahali, mpaka mtaani kabisa, na mpaka watoto nao wanabet. Nasema kwamba biashara hii ina madhara makubwa kwa taifa kuliko faida ambazo watu wanaziona juu juu.

Kwa kijana yeyote mwenye akili timamu, nashauri achana na mchezo huu, na yeyote unayemwona anacheza, mshauri aache. Peleka akili na nguvu zako kutengeneza biashara ambayo itawasaidia wengine na itakuwezesha kutengeneza kipato cha uhakika, unachoweza kuongeza kama ukiweka juhudi. Acha kutumika kuwanufaisha watu wengine.

Kocha Makirita.
www.amkamtanzania.com
Utakuwa umeliwa sana kwenye kubet,acha kudanganya uma kijana
 
Kuna mateja ya unga na mateja ya betting, kwa bahati mbaya wanatetea addiction, ila ipo siku mtajua mnachokifanya ni upuuzi tu.
 
Juzi UEFA barca vs juve jamaa odds ya droo ilikuwa na point 20 jamaa kajitoa fahamu kaweka 50000,sisi wajanja oohh barca anashinda hii mechi tena handicap!!!maanina zake jamaa kalamba 1mill ,,,high risk high return and vice versa is true!!!
 
94e35e16b275f869608fda40903120d5.jpg
 
Kubet ni jambo la hatari sana. Kwanza ni 'habit forming' yaani ukishazoea kubet huwezi kuacha. Utaiba pesa au uuze vitu vya nyumbani kwako ili mradi upate pesa za kubet. Unazoea kama vile mtu anavyokuwa mtumwa wa kuangalia picha chafu (pornography). Pili kama Makirita alivyoandika, kwenye nchi za wenzetu betting inafanyika kwenye maeneo maalum tu (yaani kwenye casino tu). Huko hakuna mtoto anayeruhusiwa. Hapa kwetu hata watoto wa shule wanabet. Wanajengewa mazoea mabaya sana. Tatu wanaobet wanadhani wanaweza kupata pesa kirahisi. Jiulize: Kama kila mtu anayebet anapata pesa kama alivyobet je, huyo mwenye kampuni inapolipa watu inapata wapi pesa za kulipa watu waliobet wakapata? Lazima ninyi mnaobet mjue kwamba wenye hayo makampuni wanapata mabilioni wakati wewe ukibet elfu 20 labda unapata laki tano ukibahatisha. Kama wewe unabet hebu andika mzigo unaoweka kwa miezi mitatu ulinganishe na kiasi unachoshinda kwa wakati huo. Utaona wazi kwamba utakuwa umeshakula hasara kubwa. Nne na mbaya zaidi ni kwamba unajijengea mazingira ya kuzoea kubahatisha mambo yako badala ya kuyapangilia kiakili
 
Katika huyo mmoja aliyepata kiasi hicho, ni wangapi ambao wameliwa?
Maana huwa mnachukua hadithi ya mtu mmoja na kuacha wengi ambao wanaliwa.
Sasa mkuu kama 50cent anayeingiza dola laki 2 kwa kila SAA kutokana na Muziki pamoja na Investments zake anabet sembuse sisi ambao hatuna uwezo wa kuingiza hata Milioni 2 kwa siku...???
 
Back
Top Bottom