John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Mshambuliaji Bernard Morrison hakuonekana katika mchezo wa jana Februari 3, wa timu yake ya Simba dhidi ya Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Mkapa katika Ligi Kuu Bara.
Hakuna taarifa rasmi juu ya Mghana huyo, lakini mapema leo amepost picha akiwa amebeba mabegi kama vile mtu ambaye anajiandaa kusafiri. Hajaweka wazi zaidi ya kuandika:
“Something huge about to BLOW”
"Guess what??
Sasa anadaiwa kuwa alisimamishwa na uongozi baada ya kile kilichoelezwa kuwa alitoka kambini bila ruhusa, kitendo ambacho ni utovu wa nidhamu.
Viongozi wamekasirishwa na kilichotokea na kuna uwezekano mkubwa akaondoka baada ya mkataba wake kumalizika au hata kabla ya mkataba kumalizika kwa kuwa timu imekuwa haifanyi vizuri hivi karibuni, huku Morrison mwenyewe akishindwa kuonyesha kiwango cha juu.