Benki ya Vijana ya CCM kuanzishwa

Benki ya Vijana ya CCM kuanzishwa

abdulahsaf

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2010
Posts
858
Reaction score
130
12th May 2012

Benki ya Taifa ya Vijana inatarajiwa kuzinduliwa wakati wowote mwaka huu.

Uzinduzi utafanyika baada ya mchakato wa kufunguliwa kwa benki ya vijana ya taifa kuingia katika hatua za mwisho, Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM –(UVCCM) Taifa, Martin Shigela amesema.

Alisema hayo wakati akizindua kikundi cha wajasiliamali wa umoja huo katika kata ya Manyoni mkoani Singida.

Alifahamisha kuwa mchakato wa kuanzishwa benki hiyo kupata usajili wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Alisisitiza kuwa taasisi hiyo itawezesha wajasiriamali wa kati na wadogo yakiwemo makundi ya wanawake kujikwamua kiuchumi.

Aliongeza kuwa ni azma ya serikali ya CCM ya kuwawezesha vijana hasa kuwapatia mtaji. Alisema tayari UVCCM ngazi ya taifa imefanya mazungumzo na mifuko ya hifadhi ya Jamii pamoja na taasisi nyingine za fedha ambazo zimeonyesha nia ya kusaidia vijana wakiwemo waendesha boda boda na vikundi vingine.

Awali akisoma risala ya kikundi hicho cha wajasiriamali, Katibu Uhamasishaji wa Kikundi Bahati Matonya alisema kikundi hicho kinakabiliwa na changamoto ya vitendea kazi zikiwemo zana za kilimo.

Alisema hali hiyo inakwamishwa maendeleo ya shamba la kikundi lenye hekari zaidi ya 200 na kumuomba Katibu Shigela kusaidia kupata wafadhili.
CHANZO: NIPASHE
 
Washe wa funguwe Bank lakini wajuwe tume ya uchunguzi wa pasa chafu Mh Zitto Kambwe na Vijana wake wako, tutawatuma kuzipitia jee hamuna pesa za Umma? mara hii ccm honga honga ya kutumia pesa za Umma kuimarisha chama itakuwa ngumu kwa vile mfereji waliokuwa wakitumia umebanwa.
 
Zitakuwa hizi hizi ambazo ilikuwa ziende kulipia mikopo yetu vyuoni wao wanafungulia Bank,,eti ya vjana wa ccm,,hatudanganyiki!
 
safi sana ndio maana naipenda ccm

Hata wakianzisha nini, wewe jiulize CCM ilikuja na propaganda za BENKI YA WANAWAKE NA IKFUNGULIWA KWA MBWEMBWE ZA HALI YA JUU, SASA JIULIZE NI WANAWAKE WANGAPI WA VIJINI KULE LINDI, LOLIONDO, UKEREWE NA KWINGINEKO WALIO KOPA KWENYE HIYO BENKI,

WATAKUWA WANAKOPA WAKINA SOFIA SIMBA NA WAPAMBE WAO
 
Yewoooomiiiiiii! Naona sasa CCM wanatafuta sehemu ya kuhamishia hela zetu zote, ili CDM tukiingia madarakani tusikute kitu. Wemeshajua 2015 hawana chao.
 
mimi nitaomba kuwa cashier.
najua madili humo ndo mahali pake kwasababu kama waliweza kupinga ndani ya b.o.t kwenye benk yao kila anayewahi kuchukua hakuna wa kumuuliza.

ccm=chukua chako mapema.
 
Ulaji tena huo!

Wanaanza kuunda mikakakati na myanya na mazingira ya kupora pesa zetu za walipa kodi na maliasili zetu kwa uchaguzi ujao.Walikua wapi kuanzisha bank hii hapo awali??Kwanini iwe bank ya vijana wa CCM?Na kwanini isiwe bank ya vijana?Ni vigezo gani vitatumika kutoa mikopo?Hapa kunamawili,kwanza ni mradi mwingine wa wajanja ndani ya CCM katika mkakati wa chukua chako mapema kabla chama hakijaporomoka,au hongo kwa vijana CCM kwa jinsi mlivyo ovyo hata kama kunania nzuri katika hili na mengine ni vigumu kuwaamini kwani imekua kawaida kushuhudia wakati wote,nia na maazimio yenu wakati wote ni kama ardhi na mbingu.Imefikia wakati kua mnatoa maelezo na uchunguzi wa kimahesabu katika miradi mlioanzisha kabla ya kuanza mipya.MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Kula CCM, kura CDM, mikopo CCM, mioya CDM. Kwanza ni mapesa yetu.
 
hata wafungue kituo cha kugawa hela bure bado haitasaidia!
Ikifika siku ya kufa hata uende India utarud mait!
 
Hahahaaaaa, huuuuuuwiiiiii sipati picha watakavyoitafuna!!!!!
 
Ndo mwarubaini wa matatizo ya watz? wapi sukita?
 
Kweli siku ya kufa nyani miti yote huteleza....wanahangaika, sisi inakaribia kukata roho, kikubwa ni kuandaa matanga tu...NO WAY OUT....!!!!
 
mimi nitajiunga kuchukua mihela hiyo.kura si ni siri.?
 
Back
Top Bottom