Benki ya Vijana ya CCM kuanzishwa

Benki ya Vijana ya CCM kuanzishwa

Hata wakianzisha nini, wewe jiulize CCM ilikuja na propaganda za BENKI YA WANAWAKE NA IKFUNGULIWA KWA MBWEMBWE ZA HALI YA JUU, SASA JIULIZE NI WANAWAKE WANGAPI WA VIJINI KULE LINDI, LOLIONDO, UKEREWE NA KWINGINEKO WALIO KOPA KWENYE HIYO BENKI,

WATAKUWA WANAKOPA WAKINA SOFIA SIMBA NA WAPAMBE WAO

Msipate tabu kung'amua hilo;serikali hii inatokana na ccm na mpaka sasa Serikali hii ya ccm inaelekea kupiga sarakasi(kichwa chini miguu juu),tusitarajie jipya zaidi ya haya tuliyokwisha kuyaona ufisadi wao wizi Wa Mali za umma wao Kama EPA/B.O.T /RiCHMoNdi/DoWANs/ na mengine ya kufanana na haya mpaka baraza la mawaziri linavunjwa mara mbili na mara zote kutokana na wizi(upotevu Wa Mal ya umai).Hii bank ni Yao kwa wao na walishagawana long time Kama tabia Yao ilivyo.
 
Ukiona chama cha siasa kinaanza kufikiria kufanya biashara ya kuahalalisha rushwa kwenye uchaguzi (Mtu anakopeshwa akishindwa lipa anaambiwa apigie kura CCM asamehewe) basi ujue kuwa kipo taabani. Hii ni idea mfu na itakufa kama yalivyokufa mabilioni ya JK.

CCM walipokuwa wanauza makampuni ya umma walikuwa wanafikiria nini?. Kabla ya kuanzisha Bank hii wawaeleze watanzania ilipofia SUKITA na miradi mingine ya chama. Is this the best UVCCM can do to attract more youths?. Umoja wa vijana wa CCM na CCM kwa ujumla wanatakiwa kusimamia sera za kukuza uchumi na ajira ili waweze kuaminiwa na vijana na si kuja na PONZI SCHEMES za kurubuni vijana kuelekea 2015.

Haya ni mawazo mufilisi kabisa, huwezi kujenga chama endelevu kinachopata support ya kweli ya wananchi wa kawaida wasiokuwa na direct economic benefit kama walivyo viongozi wanaolipwa na CCM au wanaongombea nafasi za uongozi kama ubunge n.k kupitia CCM bila ya kuhakikisha kuwa mwananchi wa kawaida ana opportunity kujinasua na maisha na kuishi katika dream yake kama tu atakuwa tayari kufanya kazi kwa bidii ambazo zitakuwepo.

Vinginevyo utakuwa umejenga chama kwa misingi ya chama kuwahumia watu si watu kukihudumia chama kwa resources. Kitendo cha mabalozi wa nyumba kumi kugombea kuendelea kuongoza ni mfano mzuri kuwa CCM haiwezi kula bila kuliwa, hawa mabalozi wameona wanatumiwa kama tissue paper wakati wa uchaguzi na chaguzi zikiisha wanakuwa bench for five years. Matokeo yake wamejikuta wakiwa ni watu wanaoombea uchaguzi kila siku ili waweze kupata posho.

Kosa kubwa lililofanywa na CCM ni kuruhusu matumizi ya pesa kwenye chaguzi na kuitungia sheria wakiita 'TAKRIMA' miaka hiyo. Utamaduni huu umejengeka kiasi kwamba sasa imekuwa 'HAIPENDWI CCM' - bali ni 'PESA'. Hii imekuwa ni distraction kubwa sana ya kuleta maendeleo nchini kwani viongozi wamekuwa mstari wa mbele kuwaibia wananchi kodi zao kupitia miradi ya kifisadi kwa matarajio ya kukusanyia chama pesa ya uchaguzi ujao badala ya kuwaletea maendeleo.
 
Naamini huo ni ushauri kutoka kwa mchumi Mwigulu nchemba,
tunasubiri watakavyo zifakamia kuzikopa bila kurudisha na kabenki kenyewe katakufilia mbali.
Vijana watakaopata nafasi ya kugombea nafasi ndio watakopeshwa ili wagharimie ushaguzi, watapigwa chini mbaya na hawatakuwa tena na uwezo wa kulipa vimikopo, benki kwishnei.
 
Last edited by a moderator:
Wenye hisa watakuwa nani katika benki hii? Hizo hisa zinauzwa wapi na kwa vigezo gani? Au ni wajanja wanatawatumia vijana kama kawaida?
 



[TD="bgcolor: transparent"] NA MAGRETH KINABO-MAELEZO
SERIKALI iko katika mchakato wa kuanzisha Benki ya Vijana ili waweze kukopeshwa na kujiletea maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa leo (jana) na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makala wakati akifungua warsha ya siku mbili ya Uratibu wa Maendeleo ya Sekta ya Vijana inayoendelea katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, iliyoandaliwa na Shirika la Restless Development, kwa niaba ya Waziri husika, Dk. Fenella Mukangara.


"Wizara tayari imeanza mchakato wa kuanzisha Benki ya Vijana ambayo riba yke itakuwa nafuu kama ilivyo Benki ya Wanawake. Tutaomba fedha katika bajeti ya mwaka ujao wa ili kuianzisha," alisema Waziri Makala.

Alisema vijana pia watapewa elimu ya namna ya kuweza kukopa na kurejesha , ambapo mafunzo hayo yatafanyika Kilosa na Marangu.


Aliongeza kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya Mfuko wa Vijana kukopesha sh. bilioni 1.2, lakini fedha zilizorudishwa ni sh. milioni 60 tu.


Waziri Makala aliwataka vijana kuacha tabia ya kulalamika badala yake wafanye kazi na kutengeneza taifa lenye migogoro ya maendeleo kwa kuwa suala la maendeleo ya taifa liko mikononi mwao.


Akizungumzia kuhusu suala la ukosefu wa ajira aliwasisitizia kuwa halitatuliwa la serikali pekee, bali linahitaji ushirikiano wa pande zote zikiwe fursa za kujiari wenyewe.


Aidha aliwataka vijana hao kutoa maoni juu ya uundaji wa katiba kuhusu masuala mbalimbali yakiwemo yanayohusu vijana bila kushawishiwa viongozi wa kisiasa dini, mashirika na taasisi.
[/TD]
 
Hii ndo ile nilisikia kwamba Uvccm ina mpango wa kuanzisha Bank au zitakuwa mbili?
 
dili la nani tena hili?

Maana yale 'mabilioni ya JK' nayo yalikuja na kupita.

Mtu mwenyewe Makala? Usanii mtupu
 
Mabenki

1. Benki ya Wanawake; Hii Issue Ile Ile Wakinamama wengi Vijijini hawataona Msaada wa hii BANK sababu wengi Hawana MALI kama ARDHI kuendelesha bila kijicho cha Mme... Tanzania Wanaume wana nguvu kwenye Masuala ya Maliasili; ARDHI, NYUMBA hadi katika Maamuzi ya Maendeleo ya WATOTO kwa hiyo hii Benki ya Wanawake itasaidia Wachache wa MIJINI na SINGLE LADIES; Lakini kiundani Mantiki ya kuweko kwa hii Benki ni kusaidia kina Mama wenye VIJIJI...

2. Benki ya Vijana... Sasa Hawa VIJANA watakaokopa WANA KAZI TAYARI ? Sababu Tatizo sio kukopa MABENKI tatizo ni AJIRA;

Sasa Vijana Wenzangu wa KIJIWENI nini hii Benki itawasaidia zaidi ya watoto wa Wakubwa na Contingent YAO

* Openion yangu ingekuwa kuwaonyesha njia za kuishi; Na Vijarasilimali wapate MSAADA au MKOPO; Sababu kuna Watanzania ninaowafahamu

Dar; Mwanza - Waliandika Proposal kuomba Msaada wa kuwapatia Wana KIJIJI FULANI huko SHINYANGA UMEME ili waweze kubengua PAMBA na PIA MAFUTA

Usiku na Mchana... Mwandishi wa Proposal kapata PESA ZA MSAADA kubwa na VIFAA vya kuunganisha SOLAR POWER

Yaani Wamefanyia ka KIJIJI KIMOJA tu na kupig picha... Kijiji ni kizuri - lakini MITAMBO na VYOMBO vingine anawauzia wananchi wenye SHIDA ya UMEME

wa Tanzania; VIFAA KAPEWA BURE - KUSAIDIA kijiji] Yeye anauzia watu na ni pesa NYINGI... Mswahili Ukijua anapesa ni peleee KITUMBO kinakosa

Kifungo cha KATI...

*** HUO SIO WIZI? Sasa HII BENKI kweli haitawaibia VIJANA?
 
Pedejee makala! Kama mabilioni ya kikwete yalishindwa,je hii bank inakuja na lipi jipya? Au ndo masharti ya mkopo ndo mpaka uwe na asset isiyohamishika ila mafisadi ndo wakopeshwe? Yetu macho tunasubilia!
 
Sijaona sababu ya kutaka kuzidi kutafuna hela zetu tunazoziweka katika mifuko ya hifadhi ya jamii kwaajili ya kutafuta uungwaji mkono kisiasa na vijana. Hiyo Benki yao wangeifungua kwa kutumia zile hela zao za wizi walizoweka Uswisi na Africa ya Kusini.
 
12th May 2012

Benki ya Taifa ya Vijana inatarajiwa kuzinduliwa wakati wowote mwaka huu.

Uzinduzi utafanyika baada ya mchakato wa kufunguliwa kwa benki ya vijana ya taifa kuingia katika hatua za mwisho, Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM –(UVCCM) Taifa, Martin Shigela amesema.

Alisema hayo wakati akizindua kikundi cha wajasiliamali wa umoja huo katika kata ya Manyoni mkoani Singida.

Alifahamisha kuwa mchakato wa kuanzishwa benki hiyo kupata usajili wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Alisisitiza kuwa taasisi hiyo itawezesha wajasiriamali wa kati na wadogo yakiwemo makundi ya wanawake kujikwamua kiuchumi.

Aliongeza kuwa ni azma ya serikali ya CCM ya kuwawezesha vijana hasa kuwapatia mtaji. Alisema tayari UVCCM ngazi ya taifa imefanya mazungumzo na mifuko ya hifadhi ya Jamii pamoja na taasisi nyingine za fedha ambazo zimeonyesha nia ya kusaidia vijana wakiwemo waendesha boda boda na vikundi vingine.

Awali akisoma risala ya kikundi hicho cha wajasiriamali, Katibu Uhamasishaji wa Kikundi Bahati Matonya alisema kikundi hicho kinakabiliwa na changamoto ya vitendea kazi zikiwemo zana za kilimo.

Alisema hali hiyo inakwamishwa maendeleo ya shamba la kikundi lenye hekari zaidi ya 200 na kumuomba Katibu Shigela kusaidia kupata wafadhili.
CHANZO: NIPASHE

Pamoja na vyanzo vingi vya mapato Jumuiya zao za Chama zinakaribia kuwatoa mgoro; wataweza Bank? Anza kwanza na kutambaa ii ukifikia kushikiia na kutembea uwe umekomaa!

Hiyo Bank kama inafunguliwa sasa hivi ni KIAMA KINGINE
 
Umenikumbusha Mradi wa mabasi ya wanafunzi Dar ulioanzishwa na ccm, sijui una mabasi mangapi sasa hivi, Nayakumbuka Magofu na makazi ya vibaka Sukita, hivi na ile super maket pale Lumumba itakuwa imekuwa kubwa na matawi nchi nzima sasa, Mbwa Mzee hafundishwi mbinu mpya za kuwinda
 
Hivi ile Benki ya Wanawake imeshafika kwa Wanawake wa Vijijini au bado ipo pale Posta inawakopesha kina Sofia Simba tu?

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),

tumbiri@jamiiforums.com
 
Back
Top Bottom