Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,498
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imekanusha taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kuchapishwa kwa fedha na kuzisambaza kwa ajili ya uchaguzi, huku baadhi ya watu wakihamasisha wananchi kuondoa fedha zao kutoka mabenki kwa madai ya uhaba wa fedha.
BoT imesisitiza kuwa taarifa hizo siyo za kweli na zinapaswa kupuuzwa. Kuchapishwa kwa fedha kunafanywa kwa mujibu wa Kifungu cha 26 cha Sheria ya Benki Kuu, Sura 197, na kuziingiza kwenye mzunguko kulingana na mahitaji ya kiuchumi na kubadilisha fedha zilizochakaa zinazorudiwa na benki za biashara. Benki Kuu pia imeendelea kutekeleza Sera ya Fedha kwa ufanisi, huku mfumuko wa bei ukiwa chini ya wastani wa asilimia 3.3 kwa miezi 10 ya mwaka 2025, thamani ya shilingi ikaimarika kwa asilimia 8.8, na akiba ya fedha za kigeni kufikia Dola bilioni 6.7, ikikidhi uagizaji wa bidhaa nje kwa miezi 5.4.
Soma: Mange Kimambi adai Benki Kuu Tanzania (BoT) imechapisha pesa Makontena kwa Makontena (Money Printing)
Aidha, BoT imethibitisha kuwa mabenki yote nchini yanaendeshwa kwa kuzingatia sheria, kanuni, miongozo na viwango vya kimataifa, ukiwa na mitaji na ukwasi wa kutosha, faida endelevu, na kiwango kidogo cha mikopo chechefu (asilimia 3.3 Septemba 2025). BoT imewaonya wananchi kutohamisha fedha zao kutoka benki na kuzitunza nyumbani, ikisema utamaduni huo ni hatari na unaweza kupelekea wizi, kupotea au uharibifu wa fedha.
Badala yake, kutunza fedha benki kunalinda amana, kunalipia riba au faida ya mwaka, na kunasaidia benki kupata mitaji ya kukopesha wananchi. Benki Kuu pia inawaonya wote wanaosambaza taarifa zisizo sahihi mitandaoni waache mara moja, kwani uvumi huo hauna tija kwa maendeleo ya sekta ya fedha na uchumi wa taifa kwa ujumla.
BoT imesisitiza kuwa taarifa hizo siyo za kweli na zinapaswa kupuuzwa. Kuchapishwa kwa fedha kunafanywa kwa mujibu wa Kifungu cha 26 cha Sheria ya Benki Kuu, Sura 197, na kuziingiza kwenye mzunguko kulingana na mahitaji ya kiuchumi na kubadilisha fedha zilizochakaa zinazorudiwa na benki za biashara. Benki Kuu pia imeendelea kutekeleza Sera ya Fedha kwa ufanisi, huku mfumuko wa bei ukiwa chini ya wastani wa asilimia 3.3 kwa miezi 10 ya mwaka 2025, thamani ya shilingi ikaimarika kwa asilimia 8.8, na akiba ya fedha za kigeni kufikia Dola bilioni 6.7, ikikidhi uagizaji wa bidhaa nje kwa miezi 5.4.
Soma: Mange Kimambi adai Benki Kuu Tanzania (BoT) imechapisha pesa Makontena kwa Makontena (Money Printing)
Aidha, BoT imethibitisha kuwa mabenki yote nchini yanaendeshwa kwa kuzingatia sheria, kanuni, miongozo na viwango vya kimataifa, ukiwa na mitaji na ukwasi wa kutosha, faida endelevu, na kiwango kidogo cha mikopo chechefu (asilimia 3.3 Septemba 2025). BoT imewaonya wananchi kutohamisha fedha zao kutoka benki na kuzitunza nyumbani, ikisema utamaduni huo ni hatari na unaweza kupelekea wizi, kupotea au uharibifu wa fedha.
Badala yake, kutunza fedha benki kunalinda amana, kunalipia riba au faida ya mwaka, na kunasaidia benki kupata mitaji ya kukopesha wananchi. Benki Kuu pia inawaonya wote wanaosambaza taarifa zisizo sahihi mitandaoni waache mara moja, kwani uvumi huo hauna tija kwa maendeleo ya sekta ya fedha na uchumi wa taifa kwa ujumla.