Benjamin William Mkapa

tutumie akili wanajf!ni kwl bmw kama binadamu alifanya makosa,hata baba wa taifa naye akiwa mbeya alisema na yeye kuna mabaya alifanya,ni jukumu la awamu inayofata kufata mazuri na kupuuza ya hovyo,tabia ya wanajf na wanahabari kuendelea kumshutumu mzee Mkapa jamani tunakosa utu,!nadiriki kusema hakuna kama mkapa mbali na baba wa taifa,nakuhakikishia kama katba ingekuwa inaruhusu ANGESHINDA KWA KISHINDO,
 
uwezo wako wa kumchambua Mkapa ndio umeishia hapo? au ulitaka kuanzisha thread tu

Hapa panatosha sana. The fact is there. Aliliibia taifa. Hujui kisomo changu,usinibeze na uchambuzi. ujumbe umefika angalia wanavyochangia wanaojua udhalimu wa Mkapa. We ulinufaika na ufisadi wake inaelekea!!!
 
Mkapa ndiyo zaidi ya wote mpende msipende na bila yeye uchumi wenu ungekuwa mbuzi

tusidanganyane sana, jamaa kajitahidi sehemu moja muhimu-Kupunguza mfumuko wa bei. Mambo mengine ni dhahama kwa Taifa. Ubabe wake umeligharimu taifa. Madini na baadhi ya maliasili ni non-renewable, kabinafisisha kwa bei ya kifisadi yakiisha ataviambia nini vizazi vijavyo? Angalau bei ingekuwa fair pesa ingeendeleza sekta nyingine ambazo zingeenelea kuhudumia vizazi hivo na effect ya kutokuwepo madini ingepungua-Leo hii utafikiri sisi ndo wawekezaji na wawekezaji ndo wenye Nchi! Hakika Mungu hamfichi MNAFIKI. huyo BWM kaiua NCHI. Mwalimu aliyoyafanya huwezi kuyalinganisha na rais yeyote aliyetokea katika nchi hii.
Mnaopiga kelele na kumlaumu kama hamjanufaika nae direct mnanufaika kupitia wazazi au ndg zenu waliosemeshwa bure, na sasa watoto wa maskini wanapewa portion ya udhamini wakati watoto wa wenye nazo wanapewa 100%.
Aca unafiki toa comment ki haki na si kupendelea. Marais wenu siku hizi wanapendelea hata maeneo waliyotoka au ukweni kwao, Mwalimu hakufanya hayo, aliona nchi ni moja na popote ni kwake ni lazima apaendeleze.
Haya wanayoyafanya Watawala yanaleta utengano, na kuna siku Mikoa itafikia wakati iseme ijitenge! BWM ana shitaka la kujibu kwa vizazi vyote nyuma yake!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
chuakachara usomi wako una walakini,coz mada yenyewe ulivyoileta ni majungu,umbeaumbea,kinafiki,kwl kama we msomi unaweza kuleta hoja namna hii?we ni mweupe na mtupu sana kichwani,mwacheni mzee wa watu apumzike,TUMEWACHOKA NA CHUKI ZENU
 
chuakachara usomi wako una walakini,coz mada yenyewe ulivyoileta ni majungu,umbeaumbea,kinafiki,kwl kama we msomi unaweza kuleta hoja namna hii?we ni mweupe na mtupu sana kichwani,mwacheni mzee wa watu apumzike,TUMEWACHOKA NA CHUKI ZENU

Apumzike sawa, lakini ametuibia!!!! Kiwila iko wapi, umbea hapo uko wapi. We unanitukana mi sitakutukana, lakini nakupa facts-Kiwila iko wapi? NBC kwa bei ya kutupa etc. Nasema kwa data. Nyumba za serikali ziko wapi? kwa bei ya kutupa. Umbea hapa uko wapi, majungu yako wapi? Angeliacha wengine wakafanya sio yeye tuliyemwamini mpaka Nyerere akaona jahazi linazama akaenda kumpigia kampeni akiamini nchi ameiacha kwa mzalendo wa kweli, kumbe looooooooooo!!!!!
 
Sasa nimeamini JF imeingiliwa na makanjanja wa siasa na taaluma.Kuna umuhimu wa mtu kubainisha yafuatayo kabla hujaamua kumchambua mtu humu
1. Matendo yake versus hali ilivyokuwa
2. Ungekuwa ni wewe kwenye viatu vyake ungefanyaje(just to be fair)?
3. Je maada unayoanzisha iko fair na balanced au inalenga kumchafua tu mtu tena kwa mtindo wa majungu?
4. Je maada unayoanzisha ina mafunzo yoyote kwa jamii au inaelezea namna ya kumchukia mtu?
5. Umechambua vya kutosha Taifa lilitaka nini kipindi hicho versus mazingira na hali ya siasa ilivyokuwa?
Ni vyema kuanzisha uzi ulio fair and balanced ili kuruhusu watu kupata elimu na kuchambua baya na zuri kuhusu mtu au matendo yake mtu.
 

Wewe ndio unaonekana kutokuwa na ABC za uchumi, uchumi wa nchi hii haujawahi kuwa Imara zaidi ya Kipindi cha Nyerere. Maana ya Uchumi Imara ni ule ambao wananchi wanajua nini kitatokea kesho na kesho kutwa, nini kinaendelea na serikali inasimamia nini kwa faida ya wananchi kwa ujumla.

Hakuna mtu alikuwa anauhakika wa nini hasa serikali inasimamia katika kipindi cha mkapa, ubinafsishaji uliofanyika kipindi cha mkapa haukuwa na faida zozote kwa taifa letu, sababu kwanza wananchi hawakushirikishwa kwa maana ya kupewa fursa za kumiliki uchumi wao, na pili ubinafsishaji huo ulikuwa haujengi misingi ya uchumi imara siku za mbele kama hizi tulizomo sasa.

Toka mbele utuambie ni nini tunajivunia sasa ambacho msingi wake umejengwa kipindi cha Mkapa, Ohoo aliacha serikali ikiwa na hifadhi kubwa sana ya fedha za kigeni for what? Fedha za kigeni ndio zinatumika masasi, ndio zinatumika Kirumi au chato au manelemango.

Mfumo mzima wa utawala wa nchi yetu chini ya chama cha mapinduzi umetufunga watanzania kwenye Mwamba wa Umasikini. we can not get out of this mess with these guys on the driving wheel.
 

Mkuu inabidi uwe na utaalamu wa kuelewa financial ststement ili uweze kujua value ya kampuni inayouzwa. Balance sheet inasehemu ya assets na sehemu na liabilities. Kama una madeni ujue thamani ya kampuni yako itakuwa chini. Nends kawsuulize CHC Ltd uambiwe NBC ikiuwa inadsiwa kiasi gani
 

Ukiimarisha uchumi ndio unaruhusiwa kufanya uhujumu uchumi? ndio sheria za nchi hii na katiba inavyosema. Come on Mkapa kafanya mambo mia moja kidogo mabaya kwa taifa hili na Nyerere huko aliko atakuwa anasikitika kama si kumlaani. Alianzia NBC, akaenda Tanesco, achilia mbali migodi, then Kiwira na mengi mengi mabaya kabisa, alitajwa kwenye list of shame ya watu 11 maadui wa nchi hii mbona hakukanusha kwa hoja zaidi ya matusi tu kama mipasho? Mkapa is worst of all
 


Na nyie msiwe mnapenda kuwachanganya wananchi akili. Msipende kutoa takwimu zisizokuwa na maelunzoezo. Wewe unadai NBC ya sasa inalipa kodi well and good. Mbona hutuambii ili walipe kodi ni kwa gross au net? Nijuavayo kodi inalipwa baada ya kutoa matumizi yote-hapa ndio kuna matumuzi ya likizo uchwara ambapo mtu anapewa masurufu ya yasiyohesabika, matumizi ya warsha, promotions, mafunzo, assets na vitu vingi kama hivi. Unakuta kiasi kidogo kinachobaki ndicho wanalipa kodi serikalini. Je kiasi gani wametuibia hapo?

Pili Tanzania sio Dar es Salaam. Huo mkopo unaosema unatoka siku tano naona ni kwa Dar kuliko na matawi kibao na mkoa ni mdogo kwa kuweza kuutemebelea siku nzima na kuumaliza. Vipi maeneo ambayo ni makubwa na miundo mbinu hafifu na banki iko makao makuu ya wilaya au mkoa. Wana faida gani na benki hiyo. Na mkopo wa siku tano unaply online, wadhamini wanatambuliwa online? hakuna collateral security? interest ikoje? Ushasema asset ya morgage unawaongelea watanzania wangapi hata ni wa mjini wakati much of their assets ni informal?Too sweet to be true.

Na ili uboreshe benki natakiwa kuiuza. He had an opportunity to do reforms na kuwandaa Watanzania wawekeze kwenye benki yao sio kuigawa sawa na bure. Mbona CRDB haikupigiwa kelele? Ni kwa sababau wananchi walipewa ownership on transparent manner. Lakini kwa NBC kupelekwa kwa speed ya radi ndio maana watu wanatia shaka.
 

Yote sawa, lakini kutenda hayo ndio kibali cha kujiuzia Kiwila na kufanya biashara akiwa ikulu?
 
Huwa inashangaza kuona hata Ibilisi naye ana watetezi wake duniani.
 
Reactions: Ame
We wasema!! Mkapa yupo kwenye list of SHAME!!! Uchumi sawa uliimarika but at the expense of kuuza nchi kwa wageni!! Wapi benki zetu, NBC ilikuwa na tatizo gani etc. Wapi Kiwira, wapi nyumba za serikali etc. We wasema!!!!!!!!!!!!!

Unataka kuniambia utendaji wa NBC wa miaka ile na sasa ni sawa???
 

Hapo kwenye No. 2 TO BE FAIR and FRANK ningekuwa mimi kwenye viatu vya Mkapa nisingejiuzia mgodi wa KIWIRA kwa bei ya kutupwa na Pia nisingefanya biashara wakati nikiwa IKULU. And thi is from THE BOTTOM OF MY HEART.
 

NBC haijauzwa, serikali imeuza hisa na inamiliki kama 40% kama sikosei.

Na kila mwisho wa mwaka serikali inapata mgao wake wa faida.
 
We wasema!! Mkapa yupo kwenye list of SHAME!!! Uchumi sawa uliimarika but at the expense of kuuza nchi kwa wageni!! Wapi benki zetu, NBC ilikuwa na tatizo gani etc. Wapi Kiwira, wapi nyumba za serikali etc. We wasema!!!!!!!!!!!!!

Zaidi ya haya yeye ndiye aliye erode tax base ya Tanzania kwakuua njia kuu za uchumi zilizokuwa zimemilikiwa na raia wa nchi hii na kuwakabidhi wageni ambao wanaonekana wanalipa kodi kubwa lakini kiukweli in aggregate walipa kodi walipokuwa wengi kodi ilikusanywa kwa wingi zaidi ( proportionaly) kuliko ilivyo sasa hasa tukizingatia strength ya currency yetu. Mkapa ndiyo sababu ya uchumi wetu kufa kwa kasi wakati huu kwani yeye ndiye founder (kwaku implement structural adjustment policies kwa manufaa ya watu wachache (yeye included) bila kuangalia impact yake kwa tax base na ajira kwa raia wa nchi hii) wa hii model anayoitumia mrithi wake.

Rais wa sasa naye amebanwa na mafisadi (waliozalishwa na mfumo wa Mkapa huku yeye (Rais) na chama chake wakilaumiwa kuwa sehemu ya huo ufisadi) ama kwakuogopa akiwashugulikia kwani pamoja na kuwa na nguvu kiuchumi pia kisiasa wakiwa na ushawishi mkubwa na hasa kutokana na hali ngumu ya raia kuhongeka kirahisi na hivyo kujikuta wakiwasaidia mafisadi kuendeleza ufisadi wao bila huruma wala uwoga. Hali hii kwa kiasi kikubwa ndiyo sababu ya sisi kuingia kwenye shida ambayo bila sisi raia wazalendo kukubali tunawajibu wa kuikwamua nchi tutaendelea kuogelea kwenye umasikini kwa majority huku mabepari wakiendelea kukita mirija yao na kuiimarisha zaidi.
 

Hakuimarisha uchumi wowote alisaidia kupoka wananchi njia kuu za uchumi na kuzikabidhi kwa mabepari na kuhakikisha hao waliopewa nguvu za kiuchumi pia wanakuwa na nguvu kisiasa ili kulinda maslahi yao dhidi ya wengi ambao watatumiwa kutokana na shida zao kuendeleza ubeberu wa hao mabepari weusi wanaotumia majina ya weupe na ngao ya sera za IMF na worldbank ambazo zikiwa contextualized wala si mbaya kiasi ya watu wanavyotaka tuamini.
 

kumbe una maslahi kwa mkwa*pa, ndo maana ulitoa pumba kwenye thread ya VINCENT NYERERE
 

na migodi aliyokataa baba wa taifa vipi? Hebu litetee hilo liuaji lako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…