mrangi
JF-Expert Member
- Feb 19, 2014
- 80,794
- 105,903
Sogeeni muonewanajifariji tu hao
Mwambie lipumbaz wenu atie pua hapo
Ova
Sent using Jamii Forums mobile app
Sogeeni muonewanajifariji tu hao
Bendera za ACT zapepea Makao Makuu CUF Z’bar
Siku moja baada ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kutangaza rasmi kujiunga na Chama cha ACT- Wazalendo, iliyokuwa makao makuu ya CUF Mtendeni mjini Unguja visiwani Zanzibar imeanza kupepea bendera ya ACT- Wazalendo.
BY Muhammed Khamis, Mwananchi mkhamis@mwananchi.co.tz
IN SUMMARY
Iililokua jengo la makao makuu ya Chama cha Wananchi (CUF) Mtendeni mjini Unguja visiwani Zanzibar asubuhi ya leo Jumanne limeanza kupepea rasmi bendera mpya ya chama cha ACT- Wazalendo
Uwepo wa hali hii umeibua maswali kwa baadhi ya wananchi na kujiuliza iwapo jengo hili lilikua mali ya chama au ya mtu binafsi.
Unguja. Siku moja baada ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kutangaza rasmi kujiunga na Chama cha ACT- Wazalendo, iliyokuwa makao makuu ya CUF Mtendeni mjini Unguja visiwani Zanzibar imeanza kupepea bendera ya ACT- Wazalendo.
Baadhi ya wanachama wa CUF kisiwani hapa wakizungumza na Mwananchi walisema hawafahamu kuhusu jengo hilo.
Majda Awadhi amesema anachokifahamu yeye hapo ni makao makuu ya chama na walikua wakiingia na kutoka tu.
“Inawezekana ilikuwa mali ya chama au pia inawezekana walikuwa wanakodi pia, yote ni sawa tu” amesema.
Soma zaidi: Maalim Seif: Shusha tanga, pandisha tanga safari ianze
Naye Said Hassan amesema kinachoonekana sasa ni matukio mazuri zaidi kwao kuliko kubaki kwenye mgogoro aliodai hauna tija kwao.
Amesema anaamini hali hiyo viongozi wanaifahamu na watakua wamejipanga vyema kutetea iliyokuwa makao makuu ya chama hicho iwapo upande wa Profesa Ibrahim Lipumba utadai ni sehemu ya mali ya chama.
Alipoulizwa na Mwananchi aliyekua Mkurugenzi wa habari wa chama cha CUF, Salim Bimani upande wa Maalim Seif, amesema kwa sasa si suala la kujadili na muda ukifika kila kitu kitajulikana ukweli wake.
Amesema kwa sasa wananchi wafahamu kuwa iliyokua jengo la makao makuu ya CUF imegeuka rasmi kuwa ofisi ya ACT- Wazalendo Zanzibar.
Soma zaidi: CUF Pemba wataka bendera za ACT
Usisahau kuimarika kwa ACT ni tangazo la kifo kwa Chadema yako.Kuna mtu pale magogoni KAFURA karibu kupasuka tusishangae majengo yote ya CUF Zenj usiku huu kuvamiwa na JWTZ na kuwekwa chini ya ulinzi mkali sana kwa muda usiojulikana.
Beautiful wife and handsome husband, Lipumba sura mbaya hata familia hana
Yaani miaka mitano inzi wa kijani wanapambana na upinzani kuwauwa na kuwabambikia kesi,hatma yake upinzani umepanda chati.
Anae mke ni KhalifaBeautiful wife and handsome husband, Lipumba sura mbaya hata familia hana
Sent using Jamii Forums mobile app
Mtaishia kuwa wezi wa kura na kupora ushindi kwa msaada wa tiss, jwtz, police na NEC,.zaidi.ya hapo hamna mnaweza.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hii sasa imeshakuwa break 'shoes'!Harakati za ubadilishwaji wa bendera katika matawi mbalimbali ya Chama cha Wananchi (CUF) kisiwani Pemba zinaendelea asubuhi hii na kupandishwa za ACT- Wazalendo huku wakitaka bendera hizo haraka kisiwani humo.
Katika wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba matawi mbalimbali yanaendelea kubadilishwa bendera hizo na wananchi walio wengi wanaonekana ni wenye kufurahia hatua hiyo.
Shughuli hiyo ya ubadilishwaji wa bendera inaongozwa na Mwenyekiti wa CUF wilaya ya Micheweni, Rashid Khalid Salim akiwa pamoja na waliokua viongozi wa chama chao awali.
Kwa mujibu wa Salim wanachokifanya sasa ni kubadili bendera maeneo yote na kufungua matawi mengine mapya ya ACT- Wazalendo kwenye wilaya yao.
Amesema kwa sababu jambo hili limetokea kwa kipindi kifupi na baadhi ya walio wengi hawakuwa wamejipanga kufanya hivyo ndio maana maeneo mengine kuna ukosefu wa vifaa zikiwemo bendera na rangi.
Kutokana na hali hiyo Salim aliwataka viongozi wakuu wa chama hicho kuhakikisha wanawapatia bendera za ACT-Wazalendo haraka.
Kwa upande wake aliyekua mwakilishi wa CUF Jimbo la Micheweni, Thubeit Khamis Faki amesema hawana muda wa kupoteza na kujadiliana kuhusu kumuunga mkono Profesa Ibrahim Lipumba kwa sasa wanachokiangalia ni kusonga mbele.
Alipoulizwa kuhusu majengo ya ofisi za CUF wanaamuaje kufanya mabadiliko amesema majengo mengi ya ofisi za chama ni ya wananchi wenyewe waliojitolea hivyo si miongoni mwa mali za chama hicho.
Bendera za ACT zapepea Makao Makuu CUF Z’bar
Hii propaganda hata beki tatu haikubali.Cuf inawanachama laki sita
Zanzibar wapo Laki moja
Katika hao laki moja 60,000 ni wapemba na ndio waliohama 40,000 bado awana upande wowote unasemaje chama kimekufa
Alafu hizo kelele zote ni za wapemba na wapemba wanamfanya seif kama nabii wao
Ndio maana hata ccm haina wafuasi wa kipemba
Cuf bara hakuna hata tawi moja lililokwenda Act unasemaje chama kimekufa..
Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe ndiye unajifariji, kanywe maji upoze machungu, Halafu mwangalie inzi miguu ya mbale na nyuma pokea ujumbewanajifariji tu hao
Cuf inawanachama laki sita
Zanzibar wapo Laki moja
Katika hao laki moja 60,000 ni wapemba na ndio waliohama 40,000 bado awana upande wowote unasemaje chama kimekufa
Alafu hizo kelele zote ni za wapemba na wapemba wanamfanya seif kama nabii wao
Ndio maana hata ccm haina wafuasi wa kipemba
Cuf bara hakuna hata tawi moja lililokwenda Act unasemaje chama kimekufa..
Sent using Jamii Forums mobile app
Lipumba na ccm akili zao wanazijua wenyewe .walijisahaulisha kabisa kuwa chama ni watu na sio cuf jina la chamaAlidhani anamkomesha maalimu self na mahakama za jiwe kumbe ni mafuriko ya watu toka cut kwenda act wazalendo