Mwananchi wa chini
JF-Expert Member
- Jul 23, 2013
- 227
- 599
ALIYEKUWA msaidizi wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe, Benard Mwakyembe amejitoza wiki chache baada ya kukihama chama hicho na kueleza mambo 10 yaliyomfanya kuhama kubwa likiwa la serikali ya awamu ya tano kufanyia kazi ajenda za chama hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mwakyembe ambaye pia alikuwa Diwani wa Kata ya Mtoni jimbo la Temeke, amesema ameamua kuzungumza na umma baada ya kuwepo upotoshaji kwamba amenunuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) huku wengine wakidai alilazimishwa kupanda jukwaa la chama hicho Septemba 15 mwaka huu wakati wa kampeni za uchaguzi wa mbunge wa Ukonga .
Mwakyembe amekanusha vikali tuhuma hizo na kusema, “mimi sikununuliwa kwa gharama yeyote na wala sikuwa na sababu ya kununuliwa kwani kipato change kinanitosheleza mimi na familia yangu…hakuna anayetoka Chadema wala chama chochote kwenda CCM akanunuliwa, labda kama wao wanafanya hizo tabia za kununua watu.”
Amesema kila mtanzania ana haki ya kuwa katika chama anachokipenda na anaweza kuhamia chama chochote huku akitolea mfano wa Mawaziri Wakuu wastaafu Edward Lowassa na Fedrick Sumaye ambao walihamia Chadema kipindi yeye akiwa katika chama hicho na kwamba waulizwe kama wao walinunuliwa kuhamia chama hicho.
“Chadema na vyama vingine vyote, acheni kupoteza umma na kuwadanganya watanzania kwamba watu wananunuliwa, wanatekwa. Hizo ni propanganda za kitoto na hazina mashiko yoyote,” amesisitiza Mwakyembe.
Akitaja sababu mbalimbali za kuhama Chadema amesema ajenda kuu katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 na 2015 endapo chama hicho (Chadema) kingeingia madarakani ilikuwa ni kupambana na ufisadi, elimu bure, ujenzi wa miundombinu, kuboresha usafiri wa anga, kuboresha huduma za afya na kuimarisha uchumi na kwamba zimefanyiwa kazi na Serikali ndani ya kipindi cha miaka mitatu tu.
“Leo Rais John Magufuli anafanya haya, tunaona ujenzi wa barabara nchi nzima unaweza kuzunguka kwa gari ukafika kwa wakati. Kama hilo halitoshi, ujenzi wa flyover ya Tazara (Mfugale Flyover) na ujenzi wa Interchange ya Ubungo, kupanua barabara ya Ubungo-Chalinze na kila wilaya zinajengwa barabara mfano Temeke imetengewa Sh bilioni 246 chini ya mradi wa DMDP, ” amesema Mwakyembe.
Amesema pia serikali chini ya Rais Magufuli imeanza ujenzi wa bwawa kubwa na kufua umeme la Stigler’s Gorge katika mto rufiji lenye uwezo wa kuzalisha MW 2100 ili kuondoa kabisa upungufu wa nishati ya umeme na kushusha gharama za nishati hiyo nchini.
Ameongeza kuwa licha ya Chadema kuahidi kuboresha usafiri wa reli, Rais Magufuli ameenda mbali zaidi na kuamua kujenga reli mpya ya kisasa (SGR) itakayosaidia kusafirisha abiria na mizigo kwa haraka zaidi.
Amesema mwaka 2015 kwenye kampeni, Chadema walikuwa wanaimba suala la kutoa elimu bure na kwamba suala hilo limefanyiwa kazi na Rais Magufuli mara tu alivyoingia madarakani kama alivyoahidi na kwamba serikali inatenga zaidi ya bilioni 20 kila mwezi kwaajili ya kuhakikisha hakuna mwananchi anayelipia elimu kuanzia darasa la awamli hadi kidato cha nne.
Aidha kuhusu ajenda ya ufisadi, Mwakyembe amesema ulikuwa ni ajenda kuu ya chama hicho na kwamba tayari imefanyiwa kazi na serikali kwa kukamatwa na kufunguliwa mashtaka watu walioisababishia Taifa hasara kwa namna yeyote.
Ameeleza sababu zingine za kumfanya ahamie CCM ni kuona namna serikali ilivyoondoa watumishi hewa waliokuwa wakiisababishia serikali hasara kwa kulipamishara hewa, ununuzi wa ndege mpya na kufufua shirika la ndege, kupunguza matumizi ya serikali na kuboresha huduma za afya kwa kujenga vituo vya afya, zahanati na hospitali kubwa akitolea mfano Hospitali ya Rufaa ya Mloganzila.
“Kutokana na mambo hayo yote niliyoyataja sijaona tena sababu ya kuendelea kupinga maendeleo yanayofanywa na Rais Magufuli na serikali yake, bali nipo tayari kupambana na kila anayepinaga maendeleo ya nchi yetu ambayo kwa muda mrefu sana ilikuwa inachezewa na wajanja, ” amesema Mwakyembe.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mwakyembe ambaye pia alikuwa Diwani wa Kata ya Mtoni jimbo la Temeke, amesema ameamua kuzungumza na umma baada ya kuwepo upotoshaji kwamba amenunuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) huku wengine wakidai alilazimishwa kupanda jukwaa la chama hicho Septemba 15 mwaka huu wakati wa kampeni za uchaguzi wa mbunge wa Ukonga .
Mwakyembe amekanusha vikali tuhuma hizo na kusema, “mimi sikununuliwa kwa gharama yeyote na wala sikuwa na sababu ya kununuliwa kwani kipato change kinanitosheleza mimi na familia yangu…hakuna anayetoka Chadema wala chama chochote kwenda CCM akanunuliwa, labda kama wao wanafanya hizo tabia za kununua watu.”
Amesema kila mtanzania ana haki ya kuwa katika chama anachokipenda na anaweza kuhamia chama chochote huku akitolea mfano wa Mawaziri Wakuu wastaafu Edward Lowassa na Fedrick Sumaye ambao walihamia Chadema kipindi yeye akiwa katika chama hicho na kwamba waulizwe kama wao walinunuliwa kuhamia chama hicho.
“Chadema na vyama vingine vyote, acheni kupoteza umma na kuwadanganya watanzania kwamba watu wananunuliwa, wanatekwa. Hizo ni propanganda za kitoto na hazina mashiko yoyote,” amesisitiza Mwakyembe.
Akitaja sababu mbalimbali za kuhama Chadema amesema ajenda kuu katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 na 2015 endapo chama hicho (Chadema) kingeingia madarakani ilikuwa ni kupambana na ufisadi, elimu bure, ujenzi wa miundombinu, kuboresha usafiri wa anga, kuboresha huduma za afya na kuimarisha uchumi na kwamba zimefanyiwa kazi na Serikali ndani ya kipindi cha miaka mitatu tu.
“Leo Rais John Magufuli anafanya haya, tunaona ujenzi wa barabara nchi nzima unaweza kuzunguka kwa gari ukafika kwa wakati. Kama hilo halitoshi, ujenzi wa flyover ya Tazara (Mfugale Flyover) na ujenzi wa Interchange ya Ubungo, kupanua barabara ya Ubungo-Chalinze na kila wilaya zinajengwa barabara mfano Temeke imetengewa Sh bilioni 246 chini ya mradi wa DMDP, ” amesema Mwakyembe.
Amesema pia serikali chini ya Rais Magufuli imeanza ujenzi wa bwawa kubwa na kufua umeme la Stigler’s Gorge katika mto rufiji lenye uwezo wa kuzalisha MW 2100 ili kuondoa kabisa upungufu wa nishati ya umeme na kushusha gharama za nishati hiyo nchini.
Ameongeza kuwa licha ya Chadema kuahidi kuboresha usafiri wa reli, Rais Magufuli ameenda mbali zaidi na kuamua kujenga reli mpya ya kisasa (SGR) itakayosaidia kusafirisha abiria na mizigo kwa haraka zaidi.
Amesema mwaka 2015 kwenye kampeni, Chadema walikuwa wanaimba suala la kutoa elimu bure na kwamba suala hilo limefanyiwa kazi na Rais Magufuli mara tu alivyoingia madarakani kama alivyoahidi na kwamba serikali inatenga zaidi ya bilioni 20 kila mwezi kwaajili ya kuhakikisha hakuna mwananchi anayelipia elimu kuanzia darasa la awamli hadi kidato cha nne.
Aidha kuhusu ajenda ya ufisadi, Mwakyembe amesema ulikuwa ni ajenda kuu ya chama hicho na kwamba tayari imefanyiwa kazi na serikali kwa kukamatwa na kufunguliwa mashtaka watu walioisababishia Taifa hasara kwa namna yeyote.
Ameeleza sababu zingine za kumfanya ahamie CCM ni kuona namna serikali ilivyoondoa watumishi hewa waliokuwa wakiisababishia serikali hasara kwa kulipamishara hewa, ununuzi wa ndege mpya na kufufua shirika la ndege, kupunguza matumizi ya serikali na kuboresha huduma za afya kwa kujenga vituo vya afya, zahanati na hospitali kubwa akitolea mfano Hospitali ya Rufaa ya Mloganzila.
“Kutokana na mambo hayo yote niliyoyataja sijaona tena sababu ya kuendelea kupinga maendeleo yanayofanywa na Rais Magufuli na serikali yake, bali nipo tayari kupambana na kila anayepinaga maendeleo ya nchi yetu ambayo kwa muda mrefu sana ilikuwa inachezewa na wajanja, ” amesema Mwakyembe.