Bei yabasi dogo aina ya coster.

Bei yabasi dogo aina ya coster.

Mnyaluhala.

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2012
Posts
1,430
Reaction score
1,789
Habari members! naomba kufahamishwa gharama za zote ( gharama kamili) za kuagiza gari aina ya coster ama aina nyingine inayofanana na hiyo kutoka nje ya nchi hadi inanifikia mimi kama mmiliki kwa ajili ya biashara. Natanguliza shukrani kwa wachangiaji!
 
angalizo: kumbuka kuna mradi wa mabasi yaendayo kasi ambao utaua biashara zote za minibuses mjini labda ulipeleke kibaha au kisarawe hilo basi lako ingawa nako kutakuwa na ushindani kwani mabasi yote yatakayoachishwa kupisha mradi wa mabasi yaendayo kasi. Kuhusu bei google kwenye used car kisha hapa wadau watakusaidia mambo ya kodi

wabeja sana
 
Nakushauri kanunue viwanja 4 vya tsh10m kila kimoja!
 
hqadi unalimiliki mkononi kama ni la mwaka 2003 kuja juu maximum 55 milion ambapo ukienda show room linakuwa hadi 60milion. Likiwa la mwaka 2000 kushuka chini inaweza fika 65 kwasababu ya kodi ya dumpimg fee.
 
Habari members! naomba kufahamishwa gharama za zote ( gharama kamili) za kuagiza gari aina ya coster ama aina nyingine inayofanana na hiyo kutoka nje ya nchi hadi inanifikia mimi kama mmiliki kwa ajili ya biashara. Natanguliza shukrani kwa wachangiaji!
coaster.jpg

2004 Toyota Coaster
Lete 46.8M nikuletee Mpaka mlangoni kwao Mkuu.
 
Lete tu huo mradi hauwezi Kuwa njia zote,mji unapanuka sana Kila siku kuna njia mpya zinaanzishwa,wapo watu wanaonunua ya petroli ambayo ni automatic ni kweli yana bei ndogo sana lakini si mazuri kwa biashara,yaliyo mazuri kwa biashara ni manual ambayo ni disel bei yake pia ipo juu la Mwaka 2000 wawezapata kwa $21000 (C.I.F).Kwa maelezo ya TRA magari haya yanayotoa huduma kwa jamii yana ushuru wa chini kidogo.Mwaka juzi niliingiza Toyota hiace super roof ushuru ulikuwa 6ml,ushuru wa coaster sina uhakika sana lakini Kama nilivyosema uwa upo chini kidogo mfano import duty ni 15% na sio 25% Kama luxury vehicles,pia ile 25% excise duty haipo ila vat ipo Kama kawaida
 
Back
Top Bottom