Bei ya sembe yapaa zaidi. Kiroba cha 25kg ni shilingi 48500 - 52500. Serikali iingilie kati

gimmy's

JF-Expert Member
Sep 22, 2011
3,283
3,274
Katika mambo ambayo hayahitaji siasa basi ni chakula.Kimsingi hali ya chakula nchini inatishia uhai wa mtanzania masikini kwani bei za nafaka zimekua zikipanda mno.

Leo ni takribani kama wiki hivi bei ya 1kg ya mahindi sokoni Tandale imefika 1350 record ambayo haijawahi kufikiwa tangu biashara hii ilipoanza kufanyika katika soko hili.

Kutokana ba mlipuko huu wa bei za mahindi ndipo bei za unga nazo zimepanda maradufu kutoka tsh37000/25kg hadi tsh48000/25kg mabadiliko ya bei ndani ya wiki moja.Kwakua bei inayouziwa Tandale ni bei ya jumla(viwandani) hivyo mtaani kiroba kimefika tsh50,000 kwa 25kg.

Ukweli ni kwamba chanzo cha tatizo hili ni serikali kufungua mipaka mwaka jana mahindi yakawa yanauzwa nje ya nchi wakati hali ya mavuno kwa mwaka jana haikua nzuri.

Kwaajili yakuweka record sawa niwakumbushe tu mwaka juzi kipindi kama hiki unga kwa 25kg uliuzwa tsh20,000 tu.Mwaka jana nao bei ya juu ilikuwa tsh 25000.

Naishauri serikali kupitia waziri wa kilimo dr Charles Tizeba wasije wakarudia kosa hili tena mwaka huu kwani mahindi sio zao la biashara kama ilivyo korosho hili ni zao la chakula mifumuko ya bei ya kiasi hiki ni hatari kwa usalama wa amani ya nchi yetu.
 
Hoja mzuri, ila wakulima walishaambiwa wauze bei wanayotaka, tena wapandishe...

Atayekufa njaa njaa, itakuwa uzembe wake kutolima...

Kwa jambo hilo, Sitegemei waziri kusema chochote kile, au ajiande kutafuta kazi nyingine kwanza kabla ya kusema...
 
Katika mambo ambayo hayahitaji siasa basi ni chakula.Kimsingi hali ya chakula nchini inatishia uhai wa mtanzania masikini kwani bei za nafaka zimekua zikipanda mno.

Leo ni takribani kama wiki hivi bei ya 1kg ya mahindi sokoni Tandale imefika 1350 record ambayo haijawahi kufikiwa tangu biashara hii ilipoanza kufanyika katika soko hili.

Kutokana ba mlipuko huu wa bei za mahindi ndipo bei za unga nazo zimepanda maradufu kutoka tsh37000/25kg hadi tsh48000/25kg mabadiliko ya bei ndani ya wiki moja.Kwakua bei inayouziwa Tandale ni bei ya jumla(viwandani) hivyo mtaani kiroba kimefika tsh50,000 kwa 25kg.

Ukweli ni kwamba chanzo cha tatizo hili ni serikali kufungua mipaka mwaka jana mahindi yakawa yanauzwa nje ya nchi wakati hali ya mavuno kwa mwaka jana haikua nzuri.

Kwaajili yakuweka record sawa niwakumbushe tu mwaka juzi kipindi kama hiki unga kwa 25kg uliuzwa tsh20,000 tu.Mwaka jana nao bei ya juu ilikuwa tsh 25000.

Naishauri serikali kupitia waziri wa kilimo dr Charles Tizeba wasije wakarudia kosa hili tena mwaka huu kwani mahindi sio zao la biashara kama ilivyo korosho hili ni zao la chakula mifumuko ya bei ya kiasi hiki ni hatari kwa usalama wa amani ya nchi yetu.
Rais alisema kuwa kama mnaona bidhaa za mazao zinalipa mkalime...

Mawazo ya viongozi wetu ni Mungu tu anayajua.
 
Acha tuisome namba. Mpaka kitakapofika, 60 elfu kiwandani ndo serikali itaingilia Kati kuwalazimisha washushe mpaka 50 kwa week 2 then wapandishe mpaka 70. Bei elekezi (isiyo na meno,)..... Loading........
 
Serikali ilisha sema haina shamba, na wakulima waliambiwa wauze mazao yao ghali na wasiingiliwe, unataka serikali ipi mkuu ijiingize kwenye hilo ambalo mkuu aliruhusu bei huria, wakati lile la sukari ALIO PANGA BEI NA KUIKOMALIA, limekiukwa na yupo kimya?! Hakujiandaa kuwa rais lakini alikwenda kuchukua form mwenyewe na kujiingiza ikulu mwenyewe...vi wonder..
 
Sasa hivi kipaumbele kwa kila wizara ni "Tanzania ya Viwanda". Shughuli za msingi zimesimama, kila mteule anaangalia ni namna gani akitoa tamko aunganishe na Tanzania ya viwanda ili kumfurahish mtu yule. Nilichogundua politics za awamu hii ni za kipekee kabisa, na hazijawahi kuonekana katika nchi yetu. Maamuzi yanafanywa kwa kuzingatia mahitaji ya wakati huo. Hawaoni mbali. Wataalam nao saivi huko mawizarani wamebakia kucheza ngoma zinazopigwa na wanasiasa badala ya kusaidia Taifa. Tuliowapa dhamana ya uongozi hawatafuti suluhisho la maana kwa matatizo yetu kwa sababu hawaelewi nini chanzo cha matatizo hayo (labda hawaoni matatizo yaliyopo). Mifumo ya uchumi na kijamii na ya kidiplomasia ya kimataifa haieleweki. Tutaangamia hivi karibuni.
 
Acha tuisome namba. Mpaka kitakapofika, 60 elfu kiwandani ndo serikali itaingilia Kati kuwalazimisha washushe mpaka 50 kwa week 2 then wapandishe mpaka 70. Bei elekezi (isiyo na meno,)..... Loading........
Iliingilia suala la sukari... kwani ilishuka au ndo inazidi kupanda? Mwafaaa
 
Serikali ilisha sema haina shamba, na wakulima waliambiwa wauze mazao yao ghali na wasiingiliwe, unataka serikali ipi mkuu ijiingize kwenye hilo ambalo mkuu aliruhusu bei huria, wakati lile la sukari ALILO PANGA BEI NA KUIKOMALIA, limekiukwa na yupo kimya?! Hakujiandaa kuwa rais lakini alikwenda kuchukua form mwenyewe na kujiingiza ikulu mwenyewe...vi wonder..
Mkuu wakulima wengi mwaka jana kutokana na matatizo ya hali ya hewa walikosa chakula,waliobahatika nao wengi waliuza na kwakuwa mipaka ilikua wazi chakula kingi kiliendelea kutoka nje hasa Kenya.Leo hao wakulima ndio wahanga no moja.
Hii kitu haihitaji siasa mkuu
 
Mkuu wakulima wengi mwaka jana kutokana na matatizo ya hali ya hewa walikosa chakula,waliobahatika nao wengi waliuza na kwakuwa mipaka ilikua wazi chakula kingi kiliendelea kutoka nje hasa Kenya.Leo hao wakulima ndio wahanga no moja.
Hii kitu haihitaji siasa mkuu
Siasa kwenye uhalisia ni jambo baya ila nimenukuu kauli za mkuu, amejisahau kwa kuwa yeye analishwa na hela za walipa kodi kasahau hata walio karibu yake, hajali wapiga kura anajiona yeye ndio yeye, tuililie serikali gani sasa? Tulie na Mungu wetu tu ndio muamuzi mkubwa.
 
Nchi hii uongo na Udicteta umezidi kila kitu watawala wanasema uongo wao wanakula chakula cha bure huko na hawakumbuki watu wanavyopata taabu huku uswahilini, Hakika hatutarudia makosa 2020!! Tumenyooshwa vya kutosha.
 
Acha tuisome namba. Mpaka kitakapofika, 60 elfu kiwandani ndo serikali itaingilia Kati kuwalazimisha washushe mpaka 50 kwa week 2 then wapandishe mpaka 70. Bei elekezi (isiyo na meno,)..... Loading........
bado kuna kijana hataki kulima! anatafuta kiki kwa kutukana wakubwa, hii bongosiasa hovyo sana.
 
Ila kusema kwamba eti mahindi si zao la biashara nikuwatukana wakulima, hivi mnajua mkulima anavyohangaika huku serikali ikimtupa kwa bei za pembejeo kuwa juu?? tunakumbuka bajeti ya ruzuku ilivyoporomoka mwaka Jana? cha msingi serikali iweke mazingira fair kwa pande zote mbili hasa hasa kumwezesha mkulima ili kumpunguzia makali ya gharama za uzalishaji
 
Wee jamaaa 25kg 48000
Nafkir umekosea n 50kg

25kg kama imefka hyo bei
Hii nchi imeuzwa
 
Kwa nini serikali isiwekeze kwenye kilimo cha mazao ya chakula? Bila ya wananchi kuwa na mlo wa uhakika,hakuna kutakachofanyika.
 
Back
Top Bottom