Bei ya mshikaki coco beach

Ikitokea harusi ya ndugu then nikapata zali la kuja dar ntawaomba mnipeleke huko mnakokuita u-coco wa beach, na milimani center sijui shopping nini nako pia, na kwenye hilo taifa la mpira pia na wapi wapi? Nkikumbuka ntasemaa
 

ukiamua unaagiza mtura
 
Bei halali ni 500 kwa nini uuziwe 1500/=
 
Ikitokea harusi ya ndugu then nikapata zali la kuja dar ntawaomba mnipeleke huko mnakokuita u-coco wa beach, na milimani center sijui shopping nini nako pia, na kwenye hilo taifa la mpira pia na wapi wapi? Nkikumbuka ntasemaa

mie nimejitolea kukupeleka sehem zote hizo ila uwe na ela ya mishkak ya paka tu.
 
kuna sehemu masaki kuna mishikaki mitamu sana, ya hapo coco chenga tu.
masaki ipi hiyo?na mimi ni mpenzi sana wa mishkaki.ya coco beach pilipili yake nzuri,ingawa utamu wa ile mishkaki naona kidogo umepungua
 
Nikifika pale sinaga mpango na mishkaki, mpango ni mdudu aka mbuzi katoriki tu!!!
 
Tatizo hapa watu wanazungumzia coco ya mihogo na ile ya Mr Mbuzi...Coco ya mihogo mishkaki ni jero tu japokua naona kuna watu wanaiita ya paka..lakini utamu wake hauna mfano.
 
Pale coco kweli kuna wahudumu aibu hawana. Kwa style yao ya utapeli mimi na wadau ilikuwa tupigwe panga la 12000 Tshs kama tusingeshtuka kwenda kuhakiki bei jikoni na counter
 
Kama hela inasumbua tandika mishkaki ya mia mia uswazi mpaka hamu ikuishe, afu ukienda huko mwendo wa laga tu.
 
Sio Coco tu mahali pengi Dar wahudumu wezi sana na nadhani wanaambiwa kufanya hivyo na mabosi wao. Rose Garden ndio balaa.
 
Nina amu na kirimoto kwa mbaaali!
 
Last edited by a moderator:
masaki ipi hiyo?na mimi ni mpenzi sana wa mishkaki.ya coco beach pilipili yake nzuri,ingawa utamu wa ile mishkaki naona kidogo umepungua

ipo chole road, mishikaki ya jeshini imehamia hapa, ha ha ha yani kisukari ukionja iyo ya coco utaisahau!
 
mpango mzima mishikaki ya mia wana pilipili tamu hyo1500 yako huku mishikaki 15 bado nyongeza kisha waenda shushia na chunky bardiii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…