Mashine ya Kusaga ama kukoboa ina sehemu mbili. INJINI na KINU.
INJINI / MOTA zinapatikana kwa ukubwa tofauti yaan Horse Power mbalimbali. Eg. HP 12, 15, 20 na kuendelea. Injini nzuri kwa kupiga mzigo na Ulaji mzuri wa Mafuta ni HP 20 bei yake ni 950,000 aina ya Jiang Dong JD, ama DF ama AMEC zote za mchina. Usinunue Lister Peter.
Ukisha nunua Injini unanunua kinu cha Kusaga na kukoboa vinapatikana Sido ama kwa mafundi wa kuchomelea kwa bei ya 500,000-700,000 kutegemea na makubaliano.
Baada ya hapo utasimika mashine yako eneo ulilochagua. Note.... Injini moja inaweza kuvuta vinu viwili katika jengo lako kinachotakiwa ni kutafuta fundi mtaalamu. Ukiwa Dsm Injini zinapatikana Mtaa wa India duka la Jumla la Injini hizo linaitwa KILIMO BORA, AU AGRO METRO. Ukiwa Mwanza duka la Injini lipo Mtaa wa Rwagasore linaitwa SHYMOND.
Endapo utasimika mashine yako kwa usahihi kabisa Kila dumu la Lita ishirini la Diesel faida yake ni Tshs. 60,000 - 80,000 kulingana na bei ya Kusagiaa.
Karibu kwenye biashara isiyo na stress Mkuu.