Bei ya mahindi yaanza kushuka kwa kasi, yatoka 110,000 kwa gunia hadi 55,000 mkoani Rukwa

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
Bei ya mahindi mkoani Rukwa imeshuka kutoka Shilingi laki moja na elfu kumi hadi kufikia shilingi Elfu hamsini na tano kwa gunia kutokana wanunuzi wa zao hilo kutoka mikoa mingine kupungua kwa kasi.

mahindi.JPG


Chanzo: ITV
 
Bei ya mahindi mkoani Rukwa imeshuka kutoka Shilingi laki moja na elfu kumi hadi kufikia shilingi Elfu hamsini na tano kwa gunia kutokana wanunuzi wa zao hilo kutoka mikoa mingine kupungua kwa kasi.

View attachment 517146

Chanzo: ITV
Ni muda wa kwenda kupata mzigo wa kuweka store aisee.

Maana muda utafika tu wa watu kulia.
 
1. Ni wakati huu wa mavuno. Kipindi kma hiki mwaka jana ilikuwa 30000
2. Mavuno si haba, ila wengi wao walikopeshwa pembejeo.
3. Tusubiri Disemba
 
Katikahili kuna baadhi ya watu litawaudhi kwakua bei ya Mahindi imeshuka.
Hatuawezi kutuudhi maan bwana yule alitujibu vibaya kwamba serikali haina shamba, lakini kwa kudra za muumba akasikia kilio chetu na sasa chakula kinakuja..
 
Amini nakwambia ungesema bei imepanda hadi 200,000/- kwa gunia hii thread sasa hivi ingekuwa na kurasa 200!
Ha ha haaa, kweli kabisa mkuu na ndio maana thread imekosa mwamko. Watu wengi mitandaoni wanapenda habari zenye mrengo hasi kuliko chanya na zile za udaku za nani kafanya nini au amekumbwa na nini.
 
kama mtu ana pesa anunua mahindi sasa muda si mrefu bei itapaa tena kwa kasi ya ajabu
 
Back
Top Bottom