Behind the curtain: September 11

Lazma The bold alikutosa sio bure wenye akili n wazungu tu toka lini mtu mwenye ngozi kama matairi ya bridgestone akawa na akili,hapa hakuna mvulana labda wewe mana nyie watoto wa kubemendwa hua mnapenda kuteleza pakavu na ndo kilichokuathiri,Kaa subiri epsode ingine ya stori ya 11 sept. Leo wacha kelele za Turbo na spidi huna punguza povu la adblue the bold hatumii oil ya SAE 40 kufilishia Diff
jamii..jpg
 
BEHIND THE CURTAIN: SEPTEMBER 11





SEHEMU YA 10






ABLE DANGER PROGRAM



Mwaka 1999 kupitia Idara ya Defense Intelligence Agency Marekani ilianzisha progfamu maalumi ya Ujasusi iliyoitwa Able Danger Program.


Lengo kuu la programu hii ilikuwa ni kung'amua mienendo ya magaidi kimataifa na kushauri vyombo vya Usalama vya Marekani juu ya hatua stahiki za kuchukua kabla hatari haijawa kubwa zaidi.


Programu hii ilikuwa inaendeshwa kidigitali zaidi.
Walikuwa wanatumia mbinu za "data mining" ili kufanya shughuli hii ya utambuzi.




(Data mining ni namna ambavyo unaweza kuchukua kiwango kikubwa cha taarifa za kielektroniki (data set) na kuzibadilisha katika mfumo ambao unakuwa rahisi na wenye kueleweka kwa ajili ya matumizi maalumu. Ili kufanikisha hili zinatumia mbinu kama artificial Intelligence, machine learning, statistics na database systems.
Kwa lugha nyingine tunaweza kusema kwamba 'data mining' ni hatua ya awali ya uchambuzi katika masuala ya "Knowledge Discovery in Database)





Kwahiyo, katika programu hii ya Able Danger, walikuwa wanatumia mbinu hiyo ta 'data mining' kuhusianisha taarifa zinazipatikana katika mifumo huru ya kompyuta (open source information) na kuzihusianisha na taarifa za siri za kijasusi (classified information) ili kuweza kufuatilia mienendo ya watu wanaotiliwa shaka kimataifa, na hatimaye wawezo kutafsiri dhamira/mipango waliyo nayo ili hatimaye waweze kuvuruga mipangk hiyo, au kuwakamata au kuwa'nuetralize' kabla hawajaleta madhara.




Nimeanza kwa kueleza hili (Able Danger Program na walichokuwa wanakifanya) kwa makusudi ili kuweka msingi wa hoja ninayotaka kuijadili.





Mwaka 2005, Mwezi June tarehe 27 mwakilishi wa Pennsylvania katika Bunge la Congress, Bw. Curt Weldon alitoa hotuba ambayo ilikuwa ni mwanzo wa watu kuanza kuhoji juu ya tukio la 9/11.


Nanukuu kipande kifupi cha Hotuba yake:


"..Mhe. Spika, nimesimama kwa sababu kuna taarifa za uhakika nimezipata katika kipindi cha miezi kadhaa iliyopita, taarifa zinazoogofya sana. Nimefahamu kuwa, kwa uhakika, moja ya vyombo vyetu vya usalama, kwa hakika, walikuwa wameng'amua mienendo ya Atta na kijiwe chake cha New York (New York Cell), yaani walimng'amua Atta na wenzake watatu na kuwatilia shaka………… lilipotolewa pendekezo kuwa FBI wawakamate, wanasheria wa Serikali wa kipindi hicho wakaeleza vyombo vya ulinzi kuwa Mohamed Atta yuko Marekani kwa Green Card na inaweza kuleta utata kwenye jamii…. Kwahiyo wakatumia vigezo vya kisheria kuizuia FBi kufanya chochote.."





Turudi nyuma miaka minne kabla… 2001.





PRESIDENT'S DAILY BRIEF



Rais wa Marekani, kila siku kabla hajaanza shughuli zake za kiofisi huwa anapatiwa nyaraka ya siri (top secret document) kutoka kwa Mkurugenzi wa Taifa wa Intelijensia (Director of National Intelligence).


Mkurugenzi huyu wa Intelijensia, huwa ana-summarise ripoti kutoka CIA, NSA, FBI na Defense Intelligence Agency na kuziweka kwenye nyaraka hii na kuiwasilisha kwa rais kila siku saa 07:45 AM, kabla Rais hajaanza shughuli yoyote.


Lengo la nyaraka hii ni kumpa update Rais kuhusu hali ya usalama wa Taifa, matishio yanayoikabili nchi na mienendo ya maadui wa Marekani.



Siku ya Tarehe 6, mwezi August 2001 (siku 36 kabla ya 9/11) nyaraka hii iliwasilishwa kwa Rais George W. Bush ikiwa na kichwa cha habari "BIN LADEN DETERMINED TO STRIKE IN US"



b956e3495ab5f21548cd49b4393a76d2.jpg

PDB iliyopelekwa kwa Rais Bush tarehe 6 August 2001.



Nyaraka hii inaeleza kinaga ubaga kuhusu tishio hilo na ikifanya reference mashambulizi ya ubalozi jijini Dar es Salaam na Nairobi.


Pia inaeleza kuhusu taarifa juu ya tishio la shambulio linalopangwa kufanya ndani ya Marekani na pia licha ya CIA pia hata Idara ya Ujasusi ya Misri inathibitisha juu ya Tishio hilo ndani ya Marekani (Neno "Egyptian Intelligence" limefutwa).



Swali la kujiuliza, je kwanini taarifa hii ifike mezani kwa Rais Bush na ishindwe kufanyiwa kazi kuepusha tukio la 9/11.

Ili kufahamu hili, tufukunyue tena kuanzia miaka kadhaa iliyopita kabla ya 2001.






Genesis..

Ili kuelewa kwa ufasaha zaidi utata wa tukio la 9/11 inapasa kuanza kuangalia suala hili kuanzia miaka mingi iliyopita, kwenye mzizi wake kabisa.


Mwaka 1984 katika ofisi ndogo ya CIA nchini Misri, kuna kijana alifika ofisini hapo ili kufanya mazungumzo na Maafisa wa CIA ili 'kumrecruit'.
Kinana huyu alikuwa anaitwa Ali Abdul Soud Mohammed.
Baada ya mazungumzo ya kina licha ya CIA kudai kuwa hawakuwa wanamuamini 100% lakini alipewa fursa ya kufanya kazi na CIA kama "junior officer".


Katika kipindi hiki ambapo Ali Mohammed alikuwa anajiunga na CIA alikuwa anatokea kwenye jeshi la Misri ambako alikuwa ni Meja katika kitengo cha Intelijensi ya kijeshi (Egyptian Army Intelligence Officer).


Baada ya kuingia CIA, Ali Mohammed alipangiwa kituo cha kufanya kazi nchini Ujerumani, jijini Hamburg.
Akiwa huko alipangiwa kuzi ya 'ku-infilitrate' kikundi cha Hezbollah ambao walikuwa na 'tawi' hapo Hamburg katika msikiti mmoja maarufu.


Kwa mujibu wa CIA wanadai kuwa, badala ya Ali Mohammed kuwachunguza waumini wanaohudhuria Ibada msikitini hapo, yeye akafanye kinyume akaenda kuongea na Imamu na watu wa Hezbollah na kujitambulisha kwao kuwa yeye ni mtu wa CIA na wamempandikiza ili awachunguze.
CAI wanadai kwamba, Ali Mohammed akashawishiwa na kugeuzwa ili aanze kuichunguza CIA na kupeleka taarifa kwa watu hao msikitini.


Sasa hapa ndipo ambapo kunaanza utata na dalili ya kwamba CIA wanasema uongo na kuna jambo zito wanalificha.!!



Katika mazingira ya kawaida lazima CIA wangeacha kushirikiana na Ali Mohammed au kumpoteza kabisa ili asiendelee kutoa siri za CIA kwa Hezbollah.
Lakini badala yake likatokea jambo la ajabu zaidi.. Tarehe 6, mwezi September 1985 Ali Mohammed aliwasili nchini Marekani.
Miezi michache baadae akumuoa mwanamama kutoka Santa Clara anayeitwa Linda Lopez na akafanikiwa kupata Uraia wa Marekani.!!


Yaani, msaliti wa CIA… kwanza anaachwa aemdelee kuishi, pili anaingia Marekani na si hivyo tu mwishowe anapeqa Uraia.!! Hili linawezekanaje?? Alipataje ruhusa ya kuingia Marekani???


Tukifukunyua nyaraka za kumbukumbu za Uhamiaji, tunakuta kwamba Ali Mohammed aliingia Marekani kwa ufadatibu maalumu wa "Visa-Waiver Program".


Chini ya utaratibu huu, mtu anapewa ruhusa maalumu ya kuingia nchini Marekani pasipo kufuata taratibu za kawaida za uhamiaji ikiwemo kuomba viza na kadhalika.


Sasa swali, ni watu wa aina gani wanapewa huu 'upendeleo' au Idara gani inasimamia hii program ni suala ambalo haliko wazi. Programu hii kwa kiwango kikubwa bado haijawekwa wazi namna ambavyo inafanya kazi na nani anayeisimamia au Idara ipi.



Lakini tukitafakari na kutafuta ushahidi zaidi, utagundua kwamba CIA pengine ndio Idara pekee (ukimuondoa Rais) yenye uwezo wa kusimamia programu ya dizaini hii.


Ukipitia Sheria ya Kuanzishwa kwa C.I.A ya mwaka 1949 kipengele 403h (Central Intelligence Agency Act 1949, (codified) 50 U.S.C 403h) inasema hivi;

Nanukuu;

"..the admission of a particular alien into the United States for a permanent residence is in the interest of national security or essential to the furtherance of the national mission, such alien and his immediate family shall be admitted to the Unites States for permanent residence without regard to their inadmissibility under immigration or any other laws and regulations.."




Tafsiri isiyo rasmi;




"..kama ruhusa ya raia wa Taifa lingine kupata makazi ya kudumu ndani ya Marekani kunaleta faida katika usalama wa Taifa au kuchochea kufikiwa kwa malengo ya taifa, basi mtu huyo na familia yake watapewa ruhusa ya ya kuingia Marekani na kupata makazi ya kudumu hata kama ikidhihirika kuwa wasingeweza kupata ruhusa hiyo kwa mujibu wa taratibu za uhamiaji na sheria nyingine.."




Mwisho wa kunukuu.



Hivyo basi, japokuwa kuna usiri kuhusu usimamizi wa "Visa-Waiver Program" lakini CIA ndiyo Idara pekee yenye uwezo wa kisheria kuisimamia, ndio kusema kwa maneno mengine kwamba Ali Mohammed aliingia Marekani kwa ruhusa ya CIA.



Mwenendo huu wa kushangaza haukuishia hapo tu, mwaka 1986 Ali Mohammed aliomba nafasi ya kujiunga na jeshi na kukubaliwa.
Akapangiwa Fort Bragg ambapo kuna "Special Oparations Command" (hapa ndipo ambapo 'Special Forces' wanakuwa trained).


Baada ya kuhitimu kama mwanajeshi mwenye weledi wa juu (US Special Force) wakubwa wake wakamuomba akasomee shahada ya Uzamivu kuhusu Tamaduni za Mashariki ya kati na Uislamu.


Baada ya kuhitimu PhD yake, Ali Mohammed akaingiza katika programu maalumu ya kufundisha wanajeshi wa Marekani kupanua ufahamu wao juu ya Tamaduni za Mashariki ya kati na Uislamu.


(Tazama hapo chini nimeweka video adhimu iliyopatikana hivi karibuni ikimuonyesha Ali Mohammed akitoa dar'sa kwa viongozi wa ngazi za juu kwenye jeshi kuhusu mahusiano kati ya Uislamu na siasa/dola… moja kati ya sentesi muhimu anazozisema ni kwamba "..in order for Islam to survive it needs political domination.. That's why there is a need to establish an Islamic State")





Mwaka 1993, kulitokea shambulio la kwanza katika majengo ya World Trade Center. (Shambulio hili halikuwa kubwa au madhara kama lile la 9/11).


Baadae watuhumiwa wa tukio hilo Mohammed Abouhadima, Mohamed Salameh na Siddig Siddig Ali walikamatwa.


Uchunguzi zaidi ulipofanyika ukabaini kuwa watu hawa wote kwa nyakati tofauti tofauti walikuwa na mawasiliano na Ali Mohammed na kulikuwa na kila dalili kuwa yeye ndiye aliyewafundisha kutengeneza mabomu.


Kesi ikafunguliwa dhidi ya watuhumiwa hao wote watatu lakini jambo la ajabu ni kwamba Ali Mohammed alipelekwa mahakamani kama Shahidi wa serikali na sio mtuhumiwa.

Mwishoni mwa kesi wenzake wote watatu walitiwa hatiani lakini yeye aliachiliwa huru.



Miaka kadhaa baadae, 1998 kulitokea mashambulizi kwenye ubalozi wa Marekani nchini Kenya na Tanzania.

Baada ya uchunguzi, ikabainika kuwa Ali Mohammed aliwahi kusafiri mpaka Yemen na Somalia katika harakati za kuratibu matukio hayo.
Lakini pia alipopekuliwa nyumbani kwake alikutwa na nyaraka kadhaa ambazo zinamlengo wa mafungamano na Al-Qaida.


Kwahiyo February, 2001 akaunganishwa kwenye kesi na watuhumiwa wengine katika kesi ya kuhusika kwenye mashambulio hayo ya balozi nchini Kenya na Tanzania.

Kesi ikaunguruma kuanzia mwezi huo February mpaka mwezi July ambapo Ali Mohammed ambapo alikiri kuhusika na tukio hilo.
Hivyo ilikuwa wazi kwamba Ali Mohammed atahukumiwa kifungo cha maisha jela bila uwezekano wa kupata Parole. Lakini ajabu ni kwamba hukumu haikusomwa na kesi ikahairishwa.


Mwezi octoba 2001, takribani mwezi mzima baada ya tukio la 9/11 kesi ya Ali Mohammed ikaendelea tena kwa ajili ha kusomwa hukumu. Lakini kumbu kumbu za mahakama zinaonyesha kuwa Ali Mohammed na Serikali ya Marekani waka-struck a deal maalumu ya na hivyo hukumu ikaharishwa kwa muda usiojulikana mpaka leo hii.


Ali Mohammed mwenyewe hajulikani amewekwa wapi na serikali ya Marekani, maana hakuna records zake kwenye gereza lolote la Marekani.


Hili suala la kuiweka hukumu 'pending' mpaka leo hii inaonekana kama ni mbinu ya kufanya nyaraka za mahakama kuhusu kesi hiyo kuendelea kuwa 'sealed' ili kulinda usiri wa 'deal' ya Ali Mohammed na Serikali.


Mara kadhaa kwa miaka yote hii 16 mwanasheria wake amekataa kuongelea chochote kuhusu "deal" ya mteja wake na serikali kwa sababu moja kuu, "hukumu bado haijatolewa" hivyo hawezi kuvunja sheria kwa kuingilia Uhuru wa mahakama.


Mkewe pia amekataa kuongelea chochote kuhusu deal hiyo, kwasababu hiyo hiyo kwamba wanasubiri hukumu, lakini wote wanathibitisha kuwa yuko hai japokuwa hawajui amewekwa wapi na serikali. (Ali Mohammed alizaliwa June 3, 1952 kwahiyo mpaka sasa atakuwa na miaka 65).




Sasa basi,


Swali: kwanini nimemuongelea Ali Mohammed kwa mapana hivi??



Turudi tena nyuma kidogo,




Mwaka 1988 Ali Mohammed akiwa mwanajeshi (Special Forces) kituo cha J.F. Kennedy aliomba ruhusa ya kusafiri kwenda nchini Afghanistan.
Akiwa huko alishiriki katika vita ya Mujahedeen dhidi ya vikosi vya Urusi akipigana upande wa vikundi vya Mujahedeen.



(Nilieleza mwanzaoni wa Makala hizi namna Serikali ya Marekani kupitia CIA walivyokuwa wanafadhili na kuunga mkono vikundi vya Mujahedeen).


Akiwa huko, Ali Mohammed alishiriki pia kutoa mafunzo kwa vijana wapya waliokuwa wanajiunga na Mujahedeen.


Mojawapo ya vijana ambao aliwapatia mafunzo hayo alikuwa ni Osama bin Laden, na Ayman al-Zawahiri (kiongozi wa sasa wa Al-Qaida).


Ndio kusema kwamba, Ali Mohammed ndiye 'kungwi' wa kwanza kumfunda Bin Laden katika masuala ya kijeshi. (First trainer)


Baadae mwaka huo huo 1988 akarejea Marekani.


Mwaka 1989 Ali Mohammed akaomba tena ruhusa ya kwenda tena Afghanistan (kumbuka ni kipindi hiki hiki ambapo Osama, al-Zawahiri na Azzam walikuwa wanaanzisha Al-Qaida).


Akiwa huko taarifa zabujasusi zenye uhakika zinaonyesha kuwa alishiriki kuwapatia mafunzo "first batch" ya wapiganaji wa Al-Qaida.


Pia alitumia ujuzi wake na weledi wa 'Special Forces' kuandaa "msahafu" wa Al-Qaida (Al-Qaida Playbook). Ambapo ulihusu masuala mbali mbali adhimu ya kijeshi kama vile Covert Operations, Kutengeneza mabomu, kuunda vijiwe (cells), ushushushu na kadhalika.



Ali Mohammed aliendelea kuwa na mawasiliano ya karibu na Osama kwa miaka mingi iliyofuata (nitaeleza huko mbeleni).



Sasa, kwanini mtu ambaye japokuwa CIA wanaficha na kumficha lakini imethibitika pasina shaka yoyote kuwa ni "asset" ya CIA awe na mafungamano kiasi hiki na Bin Laden?? Je Bin Laden alikuwa ni mshirika pia wa CIA/Marekani??





Usikose sehemu ya 11... Jumatano
 
SEHEMU YA 10, POST # 952


Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu @charmie DON SINYORI mij adden
bwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome
 
Mmmmmh! Kweli huu ni uhondo, mapemaa tu nami nimeuotea leo.
Kubali san kaz zako the Bold, kuna kitu kinazid kufunguka kchwani humu.....sio mchezo, kuna siri kubwa hapa....

Kazi njema mkuu, nasubiria j'tano.
 
SEHEMU YA 10, POST # 952


Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu @charmie DON SINYORI mij adden
bwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome
The say sijaiona mkuu, Fanya hivyo Basi maana package nimeipata kwa taab sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom