Bayport acheni utapeli

Bayport acheni utapeli

chendelela

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2015
Posts
1,145
Reaction score
1,010
Kile nilichokuwa naambiwa na watu kuhusu hii kampuni nimeamini ni kweli ni matapeli wakubwa hawa.

Walikuwa wananidai deni lao kama milioni 2, nimeangalia salary slip nimekuta wameongeza deni limefika milioni 5. Huu sio utapeli kweli?

Mimi siwezi kubali kutapeliwa kizembe naomba msaada jinsi ya kuwaadabisha hawa nyumbu.
 
Nini kilikutokea mkuu had ukaamua kwenda kwa hao jamaa
Kile nilichokuwa naambiwa na watu kuhusu hii kampuni nmeamini n kweli n matapeli wakubwa hawa.
Walikuwa wananidai deni lao kama milion 2 nimeangalia salary slip nmekuta wameongeza deni limefika milion 5 huu sio utapeli kweli?
Mm siwezi kubali kutapeliwa kizembe naomba msaada jinsi ya kuwaadabisha hawa nyumbu
 

Head Office​


Bayport House
3rd Floor, Al Dua Towers
Plot 3/12, Regent Estate
New Bagamoyo Road, Kinondoni
P.O. Box 71767
Dar es Salaam, Tanzania
Tel: +255 22 277 1420/1/2/3
Customer care: 0800 782 700
Asante mkuu
 
Hawa wapumbavu wanashirikiana na maafisa utumishi wasio waaminifu.
Kama ubaya na iwe ubaya tu kuna mtu lazima atawajibishwa
Mimi jamaa yangu ashakutana na kesi kama hiyo. Ukienda ofisin kwao wanakwambia tuliza boli kesi kama zako zipo nyingi sana. Weka barua yako hapo zamu yako ikifika tutaona shida iko wapi. Hapo inaweza pita hata mwaka huku wanaendelea kukata.
 
Inategemea mkataba ulioingia wa mkopo wa iyo 2 million mlikubaliana utalipa baada ya muda gani. Kama mlikubaliana utailipa ndani ya miaka 5-7....ukijumuisha riba itafika huko tu.. sioni namna unaenda kuwashinda endapo mkopp wako ni wa muda mrefu.

Huwa taasisi zinakushawishi ulipe kwa muda mrefu kwani makato ya mwezi yanakuwa madogo zaidi, ila ukija kwenye riba ndo inakuwa style hii....
 
Ndio wale wanataka uwe na gari namba D, nasikia kuna kampuni wakishakupa mkopo wao chini kwa chini wananza kutangaza kuna gari namba D inauzwa🐒
Labda wamekupimia wameona hauwezi kulipa kwahiyo wanajaribu kukupunguzia mzigo utakapoamua kuuza
 
Inategemea mkataba ulioingia wa mkopo wa iyo 2 million mlikubaliana utalipa baada ya muda gani. Kama mlikubaliana utailipa ndani ya miaka 5-7....ukijumuisha riba itafika huko tu.. sioni namna unaenda kuwashinda endapo mkopp wako ni wa muda mrefu.

Huwa taasisi zinakushawishi ulipe kwa muda mrefu kwani makato ya mwezi yanakuwa madogo zaidi, ila ukija kwenye riba ndo inakuwa style hii....
Deni lao lilikuwa limebaki 2 m nmecheki salary slip ya mwez uliopita deni badala ya kupungua limeongezeka 3 m mbele
 
Back
Top Bottom