themagnificient
JF-Expert Member
- Dec 13, 2016
- 988
- 3,318
Jamani eeh napenda kuwaashauri tu ukiona mkeo, mmeo, mchumba unaeenda kuoa au kuolewa nae ambae kwenu wanamfahamu basi siku akikupiga tukio jitahidi kuwa na kifua cha kutunza siri ikiwezekana usiwashirikishe ndugu zako achana nae kimya kimya kama kapiga tukio kubwa na kama linavumilika basi malizana nae chini kwa chini pasipo ndugu yako kujua.
Ukiwa na tabia ya kufikisha makosa mazito ya mwenza wako kwa ndugu zako hata pale ambapo haitakiwi Basi jua Ndugu huwa wanatengeneza chuki ya moja kwa moja ambayo baadae itakuja kuleta shida. Mkeo au mmeo anaweza akakupiga tukio la aina lolote na hasira zikiwaisha mkasameheana ila ndugu zako hawatokaa wasamehe.
Muwe na vifua ndani ya Ndoa au mahusiano sio kila jambo muwe mnashtaki kwa ndugu zenu. Mnaweza nyie mkasameheana ila ndugu huwa hawalijui hilo. Ukiwafikishia jambo huwa ndio ntolee.
Ukiwa na tabia ya kufikisha makosa mazito ya mwenza wako kwa ndugu zako hata pale ambapo haitakiwi Basi jua Ndugu huwa wanatengeneza chuki ya moja kwa moja ambayo baadae itakuja kuleta shida. Mkeo au mmeo anaweza akakupiga tukio la aina lolote na hasira zikiwaisha mkasameheana ila ndugu zako hawatokaa wasamehe.
Muwe na vifua ndani ya Ndoa au mahusiano sio kila jambo muwe mnashtaki kwa ndugu zenu. Mnaweza nyie mkasameheana ila ndugu huwa hawalijui hilo. Ukiwafikishia jambo huwa ndio ntolee.