BAVICHA watoa tamko kuhusu maandamano

BAVICHA watoa tamko kuhusu maandamano

otorokoko

JF-Expert Member
Joined
Feb 2, 2012
Posts
2,437
Reaction score
154
Mwenyekiti wa baraza la vijana BAVICHA bw PATROBAS KATAMBI akizungumza na wanahabari muda huu hapa katika mkutano wa chadema unaoendelea
-Kufwatia jeshi la polisi Tanzania jana kupiga marufuku maandamano yaliyotangazwa kufanyika na chama cha democrasia na maendeleo CHADEMA,umoja wa vijana wa chama hicho BAVICHA umeibuka na kusema kamwe hawatishiki na kauli ya jeshi hilo na wapo tayari kwa lolote.
---------
Akizungumza na wanahabari muda huu nje ya mkutano wa kamati kuu ya chama hicho mwenyekiti wa vijana taifa PATROBAS KATAMBI amesema kuwa kauli iliyotolewa na mwenyekiti wao sio kauli yake kwani ni kauli ya chama na wanachama wote hivyo polisi wasihangaike kumkamata mwenyekiti wao na badala yake wajiandae kulinda amani wakati wa maandamano- hayo.
---
“tumezoea kusikia kauli za vitisho vya jeshi la polisi wakati chadema inapotaka kufanya kitu cha kuwatetea wananchi wao,ila siku ccm ikitangaza kufanya maandamano ya amani huwezi kusikia kauli kama hizo,sasa tumechoka na mambo hayo na tupo tayari kwa lolote lile”amesema mwenyekiti wa BAVICHA TAIFA
------
Aidha amesema kuwa ofisi yake imeitisha kikao cha dharura kwa ajili ya kupanga mikakati imara ya kuanza maandamano hayo ambapo amesema kuwa yatafanyika nchi nzima bila kikomohuku akisema -yataanza muda wowote kuanzia sasa.
 
Kumekucha kabisa sasa za .........Chagonja anajitafutia umaarufu kama ilivyo kawaida yake .......Tangu Mwangosi na Mabomu ya Soweto Arusha , ndio kujitokeza hadharani huyu Chamgonjwa ........
 
Katika Maisha ukikosa hoja ya kushawishi unakuwa kioja!
 
Huyu kijana PK yuko fit kuliko wengi wanavyodhani, namkumbuka wakati tuko chuo jamaa ana stand hujapata kuona.Keep it up Kamanda PK.We do appreciate you!
 
Katika Maisha ukikosa hoja ya kushawishi unakuwa kioja!

Kuna watu wako kwenye giza hawawezi kuona ukweli wala uongo lazima waonyeshwe njia. Hawajui kuna kitu kinachoendelea duniani, !!! Lenin alisema peasants are like sack of potatoes they have to be treated potatoes in the liberation struggle! To me, Ukiwa na watu kama hao, ushawishi ni mgumu!
 
Kazi ya jeshi la polisi ni kulinda raia na mali zao na wala si jeshi la kupigana na raia. Polisi wanatakiwa watumie weredi tu. Maandamano na migomo ni haki ya kikatiba ya wananchi katika kuwasilisha sauti zao pale ambapo lugha za midomoni na kalamuni zimedunda. Polisi kuapigana na raia wema kwa maslahi yao binafisi ni kuvunja sheria. Wanatakiwa wawe walinzi wa amani ambao kazi yao ni kuhakikisha maandamano hayo yanafanyika kwa amani na usalama wa waandanaji na waandamaniwaji.

Nguvu ile ambayo wanapanga kuitumia kuua raia kwa sababu tu wanaandamana kwa amani, waitumie kuzuia uharifu wowote ambao intellingencia yao itawaambia. Hiyo ndiyo kazi yao. Vinginevyo, hawataweza kuuzima moto watakao uwasha kwa unyanyasaji na mwendelezo wa umwagaji damu za raia wema.

Wakumbuke kwamba wanaishi na kufanyia kazi kati kati ya raia. Wakumbuke kwamba wana ndugu zao wa damu ambao wanaishi uraiani na kwa vile ni maandamano ya nchi nzima, yamkini hao ndugu zao pia watakuwa miongoni mwa watakao uawa na polisi kwa vile hawatakuwa na nembo kama red cross kwamba hawa ni ndugu wa polisi.

Sioni askari yeyote atafurahia kulinda ccm huku akipoteza ndugu zake wote kwa mkono wa ccm hiyo hiyo. Sioni furaha yoyote wataipata Chagonja na mumiani wowote pale jeshi la polisi likiasi seriakali mikononi mwao. Wfahamu jeshi la leo siyo la zamani la utii kwanza akili baadaye.

Askari wa sasa wana reason na ni wasomi wanaoelewa. Na watakapochoka, ndipo uvamizi wa vituo na wizi wa sialaha magharani utashika kasi huku askari wengi waki resign ili kuepuka amri dharimu za kina chagonja ambazo zitawalazimisha kuua ndugu zao.

Chagonja, muda wa ubabe ukwisha. Tumia akili hata kama huna, azima kwa wasaidizi wako ambao wana akili na weledi kuliko wewe.
 
Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa Patrobas Katambi amelionya vikali jeshi la polisi dhidi ya mbinu za kuhujumu maandamano ya chama hicho yanayotarajiwa kuanza muda wowote kutoka sasa.

Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti huyo akiyeshinda kwa kishindo nafasi hiyo hivi karibuni amesema tamko la kuandamana lililotolewa na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe siyo kauli yake bali ni kauli ya chama.

Pastrobas amelitaka jeshi hilo kuacha kutumiwa na CCM na badala yake wajiandae kulinda maandamano hayo ili kudumisha amani.Pia amewataka kuacha kuhangaika kumkamata Mwenyekiti wao Mbowe kwani wanapoteza muda wao bure.

Patrobas ameitisha kikao cha dharura cha Baraza lake ili kupanga mikakati ya kuratibu maandamano hayo nchi nzima.

Maandamano hayo yanafanyika kulaani uhuni,ubabe na ufisadi wa pesa za wananchi unaofanywa na Bunge Maalum la Katiba na kutaka lisitishwe mara moja.
 
Kumbe tuna jembe!
Hapa magamba lazima mlie kilio cha mb*wa.
Pipoooooz
 
BAVICHA Inabidi waanze kuandika polisi taarifa za kuanza maandamano nchi nzima ......
 
Hakika kazi sasa imeanza rasmi, Mwenyekiti kamanda Patrobas tupp pamoja.

Nakuhakikishia tutawaonyesha maana ya nguvu ya umma chagonja, na polisi kwa ujumla ili waache kutumika.

Wananchi tujitoleze kwa wingi
 
Hakika Bavicha imempata mpambanaji mzuri,, polis wa nchi hii hata hawaelewi wajibu wao,, huyu Chagonja ni tatizo la Taifa amebaki kulamba miguu ya wakubwa zake tu na anafanya kazi kwa maelekezo maalum ya Interahamwe...... STUPID
 
Magamba si mlisema Patrobas mtu wenu haya sasa,msaidieni kuhamasisha maandamano ya kudai haki za raia,katiba yao ndiyo hivyo wanaitaka.
 
Back
Top Bottom