Eeh kweli kabisa buda, hii bato imekuwa iki-lazimishwa mno kwenye social media. Watu wanajitengenezea vita ya kiuchumi ambayo hata haipo maana kila mkoa una uchumi wake, wachaga wana biashara zao wasukuma wana mifugo na kilimo, kila mtu anachangia taifa kwa njia yake. Mimi na rafiki yangu msukuma tunataniana tu kwa utani kila siku, hakuna hata siku moja tukagombana kwa sababu ya hizo bato za kijinga. Ukweli ni kwamba sisi wote ni watanzania na utani wetu ni wa kujenga si wa kuharibu. Hivi watu wanaopiga hizo story wanafikiria wanaleta maendeleo gani? Wacha tuachane na mambo ya kugawa watu, tuheshimiane kama ndugu.