Basi la MWANZA COACH latumbukia mtoni

Basi la MWANZA COACH latumbukia mtoni

Taarifa za kufunguliwa leseni yake mbona hazijawekwa wazi ila nashangaa haya mabasi kuanza safari tena. Hii nchi kazi kweli kweli. Poleni mliokumbwa na masaibu.

Gharama ya rushwa ni kubwa sana na haiishii kwenye grand corruption pekee kama Escrow hapana from bottom to up. Rushwa inanuka kila sehemu unatarajia nini kitatendeka kwa haki nchi hii? Ni ngumu sana. Ndio maana mwalimu alikuwa mkali sana kwenye rushwa kwenye levels zote.
 
attachment.php

Kama ndo hivi ajali zitatumaliza maana mwanza Coach ilifungiwa pamoja na @J4 baada ya ajali mbaya iliyotokea kiabakari halafu leo tena ajali. Serikali haiko makini upande wa magari imebaki kukimbizana na bodaboda barabarani wakati magari yanamaliza watu. Tunaenda wapi? Je, tutafika tuendako?
 
Last edited by a moderator:
achen ushabik...kuna wafanyakaz kibao mwz coach...ikitokea UDA imepata ajal ndo wafungie zote?
 
Serikali inabaka raia wake kila siku kwa amri zisizo na mashiko!


Tanzania ni kama nchi ya mazuzu tu,

Tunaishi kwa matukio!
 
Mimi bado nashangaa sana maana hii hali ya ajali za barabarani zinanichanganya kabisa akili. Sijaelewa kinachowashinda madereva kuwa na mwendo wa kawaida maana kila ajali ikitokea ati mwendo kasi. Je, huu mwendo kasi hauwezi kuzuiliwa?
 
Lilifungiwa tu kwa muda but zilifunguliwa na zilishaanza kazi tena ya kusafirisha abiri

Hili ndio lile lililoua watu zaidi ya 60 katika ajali iliyohusisha na basi jingine la J4, na likafutiwa liseni au?
 



.. ZAIDI ya abiria 60 waliokuwa wakisafiri na basi la kampuni ya Mwanza Coach, kwenda Musoma mjini wamenusurika kufa baadabasi hilo kutumbukia mtoni.

"hii habari nimeipata NIPASHEonline" ni Ajali nyingine au ndiyo hii ya zamani?
 
Back
Top Bottom