CCM wana matatizo sana, ila tatizo moja kuu ni kwamba "Wanachama wao sio wakweli na wawazi", hasa wabunge. Pili hawana mtazamo wa mbali (Miaka 20 au 30 ijayo, japo wanahisi wanao mtazamo huo ila si kweli).
Wangekua ni wakweli na wawazi toka moyoni, kila mmoja angepaza sauti kutokana na mtazamo wake kuhusiana na viongozi wao na chama kinapoelekea. Na wasingepitia hizi AMBUSH WANAZOPATA kutoka kwa VYAMA PINZANI (Japo wanajidanganya hayatakua na madhara baadae, ila ndio yatakipasua zaidi chama kwa kuondoa umoja baina yao).
Mfano mzuri,
Chama cha Rais Jacob Zuma, aliekua rais wa South Africa 2009 - 14th February 2018, ANC (African National Congress) hawa jamaa wanamsimamo wa dhati, na wanaona/wana malengo ya mbali sana, si dhani kama kuna "CHAMA CHA SIASA" Africa nzima au Marekani kinafikia hata ROBO ya demokrasia au mtazamo walionayo.
Wawakilishi wao wote bungeni ni wawazi, na hawaendekezi unafiki. Pindi walipokua wakiona WAZIRI/KIONGOZI FULANI anakichafua chama kwa maamuzi ya ajabu, walikua wanamwambia RAIS amtengue haraka sana uwaziri na ateue mtu mwingine. Na Rais alitii maombi ya kamati kuu ya chama ANC (Kuna mawaziri walimwagwa kadhaa).
CCM wabunge hawana sauti hii. Tumeshuhudia mawaziri/ma DC kadhaa, wakitoa TWEETS/MAAGIZO za kebehi kwa raia (wapiga kura wao) ila hakuna maamuzi yoyote yaliofanyika.
Pili, ANC walipoona kashfa (zenye ushahidi na mashiko) zimemuelemea Rais (Ambaye wao ndio walimchagua kuwania kiti hicho cha Urais na kumsaidia kufanya campaign mpaka akashinda) walikaa kamati na kujadiliana swala hilo.
Maafikiano waliofikia, ni wampe siku Rais Jacob Zuma aandike barua ya kujiuzulu urais au wakambwage bungeni wao wenyewe kama atagoma kujiuzulu.
Nini mantiki ya maamuzi haya ya chama ANC,
Walitambua kua itawadia ugumu kumsafisha kwa wapiga kura, na itakuja kuwasababishia kupoteza wapiga kura wao waliowachagua (CREDIBILITY OF POLITICAL PARTY).
1) Ingewezekana wamuache aendelee mpaka amalize mhula wake wa uongozi, ila walikua hawapo tayari amalize muda kisha waanze kumsafisha kwa wapiga kura kwenye kampeni. Muda ungekua umeshakwenda.
Kitendo cha kumbadilisha kabla ya kumaliza kwake muda wa uongozi, imekua ni "kampeni" tosha kwa wapiga kura, wapinzani wamejikuta hawana sehem ya kuwajeruhi (Tactical Pyschological Campaign:- kampeni ya kisaikolojia kwa raia wa South Africa, kabla ya kampeni rasmi ya uchaguzi mkuu).
2) Wamedhihirisha wana demokrasia madhubuti, sambamba na mifano kama ya nchi BRAZIL & INDIA.
3) Chama cha ANC kimepata nguvu zaidi, badala ya fikra za "watu wasiokua na uelewa" kufikiria kwamba ni AIBU na CHAMA KITATETEREKA. Raia wameongeza IMANI kwenye chama ya kwamba kina msimamo na si chama cha watu wachache (Baada ya kuonesha UWAJIBISHWAJI wa viongozi wa juu).
4) ANC walikua wana uwezo wa kuingia MKATABA na Rais Jacob Zuma, sambamba na vyama vya upinzani, kua "Mh Rais akijiuzulu KINGA yake na FAMILIA yake ""ISISHTAKIWE MAHAKAMANI"" (Kama ilivyokua kwa Mh Rais Robert Mugabe).
***Kwanini hawakuweka makubaliano hayo? Na baada tu ya kuachia ngazi ya Urais Jacob Zuma akafunguliwa CASE YA MATUMIZI MABAYA YA MADARAKA & RUSHWA?
***Pamoja na mwanaye wa kiume (Kipenzi Chake) Duduzane Jacob Zuma, alipofika Airport tu alikamatwa kisha kufunguliwa case ya Uhujumu Uchumi, Matumizi mabaya ya madaraka, na Rushwa???
Majibu yanarudi pale pale "TACTICAL PYSCHOLOGICAL CAMPAING FOR A LONG TERM RUN".
5) Walifanya hivi kuepusha "MACHAFUKO" kwenye uchaguzi ujao, kuhofia Raia wasije wakawafanyia fujo na kuvunjika kwa amani ya nchi yao (kama tulivyoahuhudia baadhi ya raia wasio na ajira kuvunja maduka ya watu S.A kipindi cha nyuma).
Nawasilisha imani yangu,
Povu ruksa, ukitaka hata kunitukana poa tu.