Bashe umekosea kwenye Food Security!

Hivi kwa nini waTanzania kadhaa hua mnapenda kuandika kiswanglish katika nchi ya wasiyojua kingereza kwa wingi?mkulima asiyejua kingereza lakini alidownload Jf kwenue simu yake kisha akasoma ulichoandika hapa hata kama kina maana kwake na haelewi utakua umemsaidia nini? Si swala la kujisikia vibaya kwa nilichosema lakini jaribuni kuheshimu KISWAHILI lugha mama,kama maneno ya KISWAHILI hayafanani na ya kingereza "yaani unakosa KISWAHILI chake" ni afadhari kunyamaza
 
Wewe umeelewa lakini?
 
Naibu Waziri ana maamuzi gani kwenye Baraza?
Mimi nimefurahi kapewa hiyo nafasi baada ya kuwa mstari wa mbele katika kuukosoa utawala wa Magufuli.

Nina shauku kubwa ya kuona atachokifanya sasa baada ya kuchonga sana [ingawa kusema ukweli sitarajii lolote lile lililo jipya au lililo tofauti].
 
Asijifanye mtaalam, awatumie wataalam. Wizara ya Kilimo ina changamoto na unaweza kutegwa na kuangukia pua.

Bashe yuko vizuri sana na analeta mawazo mbadala ambayo ninyi wataalamu wa Kilimo hamnayo. Laiti mungekuwa na mawazo ya kimaendeleo basi sekta ya Kilimo Tanzania ingekuwa inachangia mpaka 75% ya pato la Taifa. Jiulizeni miaka yote mpo hapo wizarani mnafanya nini kama siyo kutoa ushauri wa kinadharia kwa wana siasa.

Huyu Bashe aliyekuja sasa ndiyo sahihi kabisa kuja kupindua meza za wakiritimba wa Wizara ya Kilimo. Uzoefu wake si wa kutilia mashaka.
 
Hawa ndo wasomi wetu wanasubiri useme ndo waanze kutoa critisims Bashe ametoa tafsiri yake ya food secutry yeye kakopi toka kwenye mia mbili naona hakuna jema utakalofanya mbele ya wasomi wetu ...
 
Hao wataala wataalamu wea wizara ya kilimo kz yao kubwa ni kutega mawaziri ili waangukie pua Okey furaha yao ni kuona wakulima wanabaki maskini miaka yote
 
Bashe yuko sahihi na ningemuomba aendelee kutoa mawazo yake hata kama kuna watu hawafurahishwi na uwepo wake kwenye nafasi hiyo. Bado naendelea kusubiri kuona mchango wa mawazo ya kujenga kutoka kwa mtoa mada ambaye bila shaka anajua zaidi ili tukichangia humu tupate namna bora ya kufanya maboresho kwenye sekta ya kilimo.
 
Food security ni moja ya somo katika course ya development studies(DS) kwa waliofika vyuoni(vyuo vikuu), hivyo Bashe alipaswa kujua hili unless hakusoma hii somo chuoni au kasahau.
 
Food security ni moja ya somo katika course ya development studies(DS) kwa waliofika vyuoni(vyuo vikuu), hivyo Bashe alipaswa kujua hili unless hakusoma hii somo chuoni au kasahau.
Hilo somo limemsaidia nini mkulima wa Tanzania hadi Leo Hii? Si mmemlundikia umaskini wa kutupwa kwa zaidi ya miaka 58 toka tupate Uhuru?

Mwacheni bashe afanye jambo jipya.huo usomi feki umelitia hasara taifa.Eti mkulima asiuze nje!? Mbona wenye viwanda wanauza nje! Mbona kuna wanafunzi wanaenda kusoma nje,kwanini msiseme wasome hapahapa kwakua walimu tunao na wengine hawana kazi?

Siku misomi ya kibongo itakapojua kujua kilimo ni biashara,huo utakuwa mwanzo wa ukombozi kwa wakulima ambao ni kama 70% ya watanzania
 

Ni wivu tu ndiyo unakuzuzua mtoa mada. Huwezi ukamponda Hussein Bashe kwa sababu zako za kukariri concept ya Food Security. Kwa taarifa yako Bashe ana uhakika na anachokifanya.

Kikubwa alichoongea ni kuanzishwa kwa agricultural stabilization fund ambayo itakuwa ni buffer wakati wa fluctuation ya supply and demand. Na hilo ndiyo jukumu la Serikali yoyote duniani inayowajibika kwa wanamchi wake.
 
Mfanyabiashara hapangi Bei, Bali atanunua kwa Bei ile ambayo itampa faida akifikisha mzigo sokoni(hivyo huwa anaweza kukataa kununua kwa Bei ambayo itamkata/haimlipi). pia mkulima alikuwa anatakiwa awe anafuata same path asiuze mazao yake kwa Bei ambayo haito mlipa gharama na faida......
Elimu,Elimu elimu kwa wakulima...
 
Bashe nimemwelewa sana kunakipindi nilikuwa na gunia 100 zenye debe 10 kila gunia ikauza na kupata milion 2.kama hujalima huwezi ukachukulia kwauzito kauli ya bashe.Mnaolalamika sana mpo mjini hamna hata shamba
 
Wadanganyika sijui mna tabu gani unapoteza muda wako kwa mtu ambae hashiriki hata kwenye vikao vya Baraza la mawaziri yeye anaishia kumshauri tu Boss wake na Kama unavyojuwa bosi wako akiona unaakili yakuonekana yeye ni Bogus hatayafikisha mawazo yako!
 
Tatizo la wanaccm wengi, akishakuwa waziri anajiona kuwa anajua kila kitu hata hawataki kutumia/kusikiliza wataalam
 
Moja ya changomoto kubwa tunayoipata Kama taifa kwenye kilimo, nikuwa kwenye 78% ya watanzania ambayo wanajishughurisha na kilimo zaida ya 90% Ni wakulima wadogo(subsistence farmers) wanalima kwa ajili ya kujilisha na ziada kidogo ndo wauze.....

Hivyo takwimu zinaonyesha kuwa vijiji umasikini umetalaki kuliko mijini na pia umasikini wa chakula Ni mkubwa zaidi vijinini (kwa Hawa wakulima) kuliko mijini....

Jibu: ni kuto kuzalisha mavuno ya kutosha kwa ajili ya chakula mwaka mzima, na ziada ya kutosha kuuza ili kupata fedha ya kukidhi uhitaji vitu vingine elimu,afya na gharama vingine za maisha(maji, energy/mafuta/Sola/umeme) na n.k kwa mwaka mzima

Sababu:
*FARM SIZE/FIELD, Ukubwa wa mashamba, wengi wanalima mashamba madogo chini ya hekari 30 kwa mwaka

* LOW YIELD PER UNIT AREA, mavuno kidogo kulinganisha na ukubwa wa mashamba.

*INADEQUATE USE OF MACHINES AND TECHNOLOGY, uwezilima heka 100 kwa trekta alafu upambane kuzipalilia kwa jembe la mkono, na kuvuna kwa mkono, ukawa na ufanisi wa kuzalisha zaidi.

*FEW WORK DAYS per year, wakulima wadogo tz wanafanya kazi si zaidi za miezi 7 kwa mwaka, yaaaani kidindi ya kuaandaa Shamba,palizi,kusimia shamba,kuvuna na kuifadhi, baada ya hapo hakuna kikubwa wanachofanya kuingiza kipato Hadi msimu wa kilimo Tena uanze...

*POOR FINANCIAL MANAGEMENT, wakulima wadogo wakisha vuna waingiwa na tamaa na kuuza ziada ndani ya muda mfupi na hela haikai

Na n.k sababu Ni nyingi.......
PAUL MAYALA
Eliphaz the Temanite Paul Alex BOOS
 
What a hell is this rubbish?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…