Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 40,949
- 74,431
Baraza la sanaa la Taifa (BASATA) ambalo lipo kisheria, majuzi lilimhukumu msanii Shilole asijihusishe na masuala ya sanaa kwa mwaka mmoja kutokana na kukiuka taratibu zilizowekwa na kuvunja maadili. Hivi tunapozungumza msanii huyo yuko kwenye adhabu hiyo.
Lakini jambo la ajabu ni kuwa CCM pamoja na kufahamu adhabu hiyo wao wameidharau na kumchukua Shilole ili aambatane na mgombea wao wa Urais na kupanda majukwaani kushiriki shughuli za muziki kinyume na adhabu yake. Jee hiyo sio dharau kwa mamlaka iliyotoa adhabu?
BASATA nao kama jambo hilo lingefanywa na wengine wangekaa kimya kama walivyo sasa?
Nadhani sasa wasanii na watu wengine waelewe kuwa adhabu zinazotolewa na mabaraza haya ni za magazetini tuu hivyo hakuna haja ya kuziheshimu wao waendelee na mambo yao tuu.
Hiyo ni Songea kwenye Mkutano. Pia Njombe alikuwa jukwaani..
Lakini jambo la ajabu ni kuwa CCM pamoja na kufahamu adhabu hiyo wao wameidharau na kumchukua Shilole ili aambatane na mgombea wao wa Urais na kupanda majukwaani kushiriki shughuli za muziki kinyume na adhabu yake. Jee hiyo sio dharau kwa mamlaka iliyotoa adhabu?
BASATA nao kama jambo hilo lingefanywa na wengine wangekaa kimya kama walivyo sasa?
Nadhani sasa wasanii na watu wengine waelewe kuwa adhabu zinazotolewa na mabaraza haya ni za magazetini tuu hivyo hakuna haja ya kuziheshimu wao waendelee na mambo yao tuu.
Hiyo ni Songea kwenye Mkutano. Pia Njombe alikuwa jukwaani..