Ndugu, Mhe. Rais wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. SAMIA SULUHU HASSAN
Nakusalimu kwa jina la JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.
Mhe. Rais, Mimi ni kijana Mtanzania (Mzalendo), umri wangu ni miaka 40, na nina Postgraduate Diploma in Accountancy.
Ninaomba kuonana na wewe Mhe. Rais, ili niweze kusikia busara zako, Utashi wako na Mwongozo wako kabla sijafanya uamuzi wa kuivunja KATIBA ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria, Kanuni na Taratibu zake kwa kujitoa uhai wangu.
Nasikitika kila kukicha kuona Karama, Kipaji, kipawa na Talanta, nilivyopewa na Mungu wangu havitumiki katika kulisukuma gurudumu la Taifa. Najiona sina maana ya kuendelea kuishi hapa duniani.
Msongo wa mawazo unanitesa sana. Natamani kujinyonga au kufanya tukio kubwa nipelekwe gerezani nikafie huko, au niende hata msituni nikaliwe na wanyama wakali.
Tafadhali Mhe. Rais, ninaomba msaada wako ili niweze kutoka katika kipindi hiki cha mateso makali. Nina watoto wawili ambao sipo nao, mke alishanikimbia muda mrefu sana.
Nina amini, nikipata kitu cha kufanya chenye uhakika, hata kama ni kuosha magari ya Serikali, Kazi yeyote ile (permanent) ya kuniingizia kipato, nitapata utulivu wa akili na wa Moyo.
Natanguliza shukurani za dhati.
Wako Mtiifu na Mnyenyekevu,
Nakusalimu kwa jina la JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.
Mhe. Rais, Mimi ni kijana Mtanzania (Mzalendo), umri wangu ni miaka 40, na nina Postgraduate Diploma in Accountancy.
Ninaomba kuonana na wewe Mhe. Rais, ili niweze kusikia busara zako, Utashi wako na Mwongozo wako kabla sijafanya uamuzi wa kuivunja KATIBA ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria, Kanuni na Taratibu zake kwa kujitoa uhai wangu.
Nasikitika kila kukicha kuona Karama, Kipaji, kipawa na Talanta, nilivyopewa na Mungu wangu havitumiki katika kulisukuma gurudumu la Taifa. Najiona sina maana ya kuendelea kuishi hapa duniani.
Msongo wa mawazo unanitesa sana. Natamani kujinyonga au kufanya tukio kubwa nipelekwe gerezani nikafie huko, au niende hata msituni nikaliwe na wanyama wakali.
Tafadhali Mhe. Rais, ninaomba msaada wako ili niweze kutoka katika kipindi hiki cha mateso makali. Nina watoto wawili ambao sipo nao, mke alishanikimbia muda mrefu sana.
Nina amini, nikipata kitu cha kufanya chenye uhakika, hata kama ni kuosha magari ya Serikali, Kazi yeyote ile (permanent) ya kuniingizia kipato, nitapata utulivu wa akili na wa Moyo.
Natanguliza shukurani za dhati.
Wako Mtiifu na Mnyenyekevu,