Barua ya wazi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

GAZETI

JF-Expert Member
Feb 24, 2011
5,277
6,673
Mheshimiwa Rais, sisi wakulima wa zao la korosho ni miongoni mwa watu tusiosikilizwa na tunaopigwa danadana kwenye mambo mengi sana, Bila msaada wako hatuwezi kunusurika.

Kwa nia safi Kabisa serikali imeamua kugawa Viuatilifu kwa wakulima lakini jambo la kushangaza ni kuwa havigaiwi kwa wakati licha ya kuwa viko kwenye maghala ya vyama vya msingi vya ushirika. Ni miezi miwili na zaidi sasa toka awamu ya kwanza ya ugawaji ipite, Kwa mikorosho ni hatari kwani unavyokaa muda mrefu bila kupiga dawa inapelekea kuua maua na hivyo kusababisha uzalishaji kupungua.

Rais Samia, kinachosikitisha ni kuwa hizi pembejeo zipo kwenye maghala lakini zinashindwa kufanikiwa kutokana na kukosekana kwa vitu vinavyoitwa Vibandiko, Sasa serikali inawezeje kusafirisha mzigo mkubwa wa viuatilifu halafu ishindwe vibandiko ambavyo ni vikaratasi vidogo sana visivyo na uzito wowote Jambo la kushangaza ni kuwa tatizo hili limekuwa likijirudia kila awamu.

Muheshimiwa Rais, sisi wakulima wa korosho ni wanachi wako kama walivyo wananchi wengine, kwanini tunanyanyasika kiasi hiki? Tunaamini wewe kama kiongozi wa nchi unaweza kutatua hili ili kuokoa zao la korosho na wakulima wake na si hivyo tu bali pia korosho zinachangia pato la Taifa.

Ahsante
 
Mheshimiwa Rais, sisi wakulima wa zao la korosho ni miongoni mwa watu tusiosikilizwa na tunaopigwa danadana kwenye mambo mengi sana, Bila msaada wako hatuwezi kunusurika.

Kwa nia safi Kabisa serikali imeamua kugawa Viuatilifu kwa wakulima lakini jambo la kushangaza ni kuwa havigaiwi kwa wakati licha ya kuwa viko kwenye maghala ya vyama vya msingi vya ushirika. Ni miezi miwili na zaidi sasa toka awamu ya kwanza ya ugawaji ipite, Kwa mikorosho ni hatari kwani unavyokaa muda mrefu bila kupiga dawa inapelekea kuua maua na hivyo kusababisha uzalishaji kupungua.

Rais Samia, kinachosikitisha ni kuwa hizi pembejeo zipo kwenye maghala lakini zinashindwa kufanikiwa kutokana na kukosekana kwa vitu vinavyoitwa Vibandiko, Sasa serikali inawezeje kusafirisha mzigo mkubwa wa viuatilifu halafu ishindwe vibandiko ambavyo ni vikaratasi vidogo sana visivyo na uzito wowote Jambo la kushangaza ni kuwa tatizo hili limekuwa likijirudia kila awamu.

Muheshimiwa Rais, sisi wakulima wa korosho ni wanachi wako kama walivyo wananchi wengine, kwanini tunanyanyasika kiasi hiki?? Tunaamini wewe kama kiongozi wa nchi unaweza kutatua hili ili kuokoa zao la korosho na wakulima wake na si hivyo tu bali pia korosho zinachangia pato la Taifa.

Ahsante
Mkoa gani na Wilaya gani penye tatizo hilo la ugawaji wa Viuatilifu
 
Sio kwenye viuatilifu tu ambapo Serikali ilishindwa kusimamia ugawaji wake.

Nimeona tatizo hilo pia kwenye ugawaji wa mbolea ya ruzuku pamoja na viatilifu kwenye zao Tumbaku.

Nadhani Waziri wa Kilimo Bwana Bashe, hajaweza kusolve hili tatizo.

Nashauri angeanzisha kikosi kazi kushughulikia hili.
 
Bajeti ya kilimo SHS milion 2🤣tunategemea nini katika dunia hii yenye ushindani
 
Mheshimiwa Rais, sisi wakulima wa zao la korosho ni miongoni mwa watu tusiosikilizwa na tunaopigwa danadana kwenye mambo mengi sana, Bila msaada wako hatuwezi kunusurika.

Kwa nia safi Kabisa serikali imeamua kugawa Viuatilifu kwa wakulima lakini jambo la kushangaza ni kuwa havigaiwi kwa wakati licha ya kuwa viko kwenye maghala ya vyama vya msingi vya ushirika. Ni miezi miwili na zaidi sasa toka awamu ya kwanza ya ugawaji ipite, Kwa mikorosho ni hatari kwani unavyokaa muda mrefu bila kupiga dawa inapelekea kuua maua na hivyo kusababisha uzalishaji kupungua.

Rais Samia, kinachosikitisha ni kuwa hizi pembejeo zipo kwenye maghala lakini zinashindwa kufanikiwa kutokana na kukosekana kwa vitu vinavyoitwa Vibandiko, Sasa serikali inawezeje kusafirisha mzigo mkubwa wa viuatilifu halafu ishindwe vibandiko ambavyo ni vikaratasi vidogo sana visivyo na uzito wowote Jambo la kushangaza ni kuwa tatizo hili limekuwa likijirudia kila awamu.

Muheshimiwa Rais, sisi wakulima wa korosho ni wanachi wako kama walivyo wananchi wengine, kwanini tunanyanyasika kiasi hiki?? Tunaamini wewe kama kiongozi wa nchi unaweza kutatua hili ili kuokoa zao la korosho na wakulima wake na si hivyo tu bali pia korosho zinachangia pato la Taifa.

Ahsante
Wakulima wa pamba huko kanda ya ziwa ni vilio tupu. Bei imeporomoka hatari ukilinganisha na mwaka Jana
 
Mheshimiwa Bashe fatilia huko kwenye Korosho kuna mambo bado inaonekana hayajakaa sawa,vitu vingine mi naona huwa ni vidogo sana mpaka kufikia kwa Raisi au Waziri,ndio maana huwa wakati mwingine kuna haja watu watumbuliwe ili mambo yaende,haya mambo ya kuoneana aibu ni shida sana kwa kweli...
 
Back
Top Bottom