Relief Mirzska
JF-Expert Member
- Jun 13, 2017
- 13,988
- 22,379
Mkuu,
Pole kwa majukumu na changamoto za uongozi.
Kwanza naomba ku-declare interest: Mimi ni kijana wa kiislam ambae Nina uelewa kiasi juu ya Uislam.
Hivi karibuni ulidhamiria kufanya kampeni ya kulisafisha jiji la Dar as salaam kuhusu suala zima la watu wanaojihusisha/wanaofanya mapenzi ya jinsia moja (mashoga). Napenda nikuhakikishie kuwa, ndani ya mioyo ya Watanzania wenye busara na akili na wenye kuitakia mema nchi yao ulipata uungwaji mkono wa hali ya juu. Mimi binafsi nilikaa nikawa nakuombea kwa Mungu akupe ujasiri wa kulifanikisha suala lile.
Mkuu, nataka nikuhakikishie na kukufariji kwamba wapo watu wakubwa na wenye busara zao ambao wanajua kwamba ulikuwa sahihi kuanzisha kampeni ile, sitaki kuwazungumzia maana mimi sio msemaji wao rasmi lakini amini usiamini kwamba kuanzia Mheshimiwa Mchungaji Peter Msigwa, Mheshimiwa Said Kubenea, Mheshimiwa Zitto Kabwe, Dk Bashir Ally, Baraza la wawakilishi la Zanzibar na kama sisi hohehahe tulikuwa pamoja na wewe.
Mkuu, suala hili lilikuwa na sura mbili na ni bahati mbaya sana kwamba umma wa wanasiasa wakalifanya ni suala la kisiasa. Wanasiasa hao walikuwa wakikuunga mkono ndani ya mioyo yao lakini kwa sababu hawakutaka kuwakasirisha ma-boss wao wakajitoa akili zao, wakajifanya hamnazo, wakakupinga au wakafurahia pale ulipopingwa hadharani.
Mkuu, katika suala hili la ushoga ujasiri wako hautosahaulika kamwe na Mimi binafsi mungu akinipa umri nitakuja kuhadithia ujasiri huu wajukuu zangu. Vile vile hatutakaa tuusahau ukasuku na unafiki wa wale waliokupinga katika hili, hatuna vya kuwafanya tunawatazama tu ila kiukweli thamani yao kwetu imeshuka.
Mkuu, kwa vile msingi mkubwa wa barua hii ni suala hili la ushoga, naomba tuishie katika suala hili japo zipo kampeni zako nyengine nyingi tu ambazo binafsi nilizikubali sana ila sikukubali njia ulizotumia kwenye kampeni hizo. Kampeni ya madawa ya kulevya, kampeni ya kutetea wanawake/ watoto waliotelekezwa na nyenginezo zilikuwa ni kampeni zenye nia njema lakini njia zilizotumika kufanya kampeni hizo nadhani hazikuwa sahihi. Kama hivyo ndivyo, basi nadhani ipo haja ukaangalia upya timu ya washauri wako.
Najua watatokea watakaonipinga, kunikebehi na kunitukana lakini Mwenyezi Mungu mtukufu kwenye kitabu chake cha qur an anasema " wala msichanganye haki na batili, mkaificha haki na hali mnajua (Qur an 2:42)" na Mimi nimeamua kukukumbusha na kukupongeza juu ya msimamo wako uliouchukua juu ya suala hili.
Mkuu, hata kama nchi hii haina dini, na msingi wa taratibu na kanuni za maisha ya Watanzania ni katiba zao, basi sihitaji kukukumbusha kuwa hiyo katiba ambayo wale waliokupinga "WALIAPA" kuilinda na kuitetea basi inakataa mambo ya ushoga ndani ya nchi hii ambayo mmoja wa waasisi wake alitangazwa kuwa "MTAKATIFU".
Kuna mengi ya kusema lakini kwa Leo naomba niishie hapa ili nikaribishe matusi na kejeli za wale wote wanaotetea ushoga.
Relief Mirzska.
Pole kwa majukumu na changamoto za uongozi.
Kwanza naomba ku-declare interest: Mimi ni kijana wa kiislam ambae Nina uelewa kiasi juu ya Uislam.
Hivi karibuni ulidhamiria kufanya kampeni ya kulisafisha jiji la Dar as salaam kuhusu suala zima la watu wanaojihusisha/wanaofanya mapenzi ya jinsia moja (mashoga). Napenda nikuhakikishie kuwa, ndani ya mioyo ya Watanzania wenye busara na akili na wenye kuitakia mema nchi yao ulipata uungwaji mkono wa hali ya juu. Mimi binafsi nilikaa nikawa nakuombea kwa Mungu akupe ujasiri wa kulifanikisha suala lile.
Mkuu, nataka nikuhakikishie na kukufariji kwamba wapo watu wakubwa na wenye busara zao ambao wanajua kwamba ulikuwa sahihi kuanzisha kampeni ile, sitaki kuwazungumzia maana mimi sio msemaji wao rasmi lakini amini usiamini kwamba kuanzia Mheshimiwa Mchungaji Peter Msigwa, Mheshimiwa Said Kubenea, Mheshimiwa Zitto Kabwe, Dk Bashir Ally, Baraza la wawakilishi la Zanzibar na kama sisi hohehahe tulikuwa pamoja na wewe.
Mkuu, suala hili lilikuwa na sura mbili na ni bahati mbaya sana kwamba umma wa wanasiasa wakalifanya ni suala la kisiasa. Wanasiasa hao walikuwa wakikuunga mkono ndani ya mioyo yao lakini kwa sababu hawakutaka kuwakasirisha ma-boss wao wakajitoa akili zao, wakajifanya hamnazo, wakakupinga au wakafurahia pale ulipopingwa hadharani.
Mkuu, katika suala hili la ushoga ujasiri wako hautosahaulika kamwe na Mimi binafsi mungu akinipa umri nitakuja kuhadithia ujasiri huu wajukuu zangu. Vile vile hatutakaa tuusahau ukasuku na unafiki wa wale waliokupinga katika hili, hatuna vya kuwafanya tunawatazama tu ila kiukweli thamani yao kwetu imeshuka.
Mkuu, kwa vile msingi mkubwa wa barua hii ni suala hili la ushoga, naomba tuishie katika suala hili japo zipo kampeni zako nyengine nyingi tu ambazo binafsi nilizikubali sana ila sikukubali njia ulizotumia kwenye kampeni hizo. Kampeni ya madawa ya kulevya, kampeni ya kutetea wanawake/ watoto waliotelekezwa na nyenginezo zilikuwa ni kampeni zenye nia njema lakini njia zilizotumika kufanya kampeni hizo nadhani hazikuwa sahihi. Kama hivyo ndivyo, basi nadhani ipo haja ukaangalia upya timu ya washauri wako.
Najua watatokea watakaonipinga, kunikebehi na kunitukana lakini Mwenyezi Mungu mtukufu kwenye kitabu chake cha qur an anasema " wala msichanganye haki na batili, mkaificha haki na hali mnajua (Qur an 2:42)" na Mimi nimeamua kukukumbusha na kukupongeza juu ya msimamo wako uliouchukua juu ya suala hili.
Mkuu, hata kama nchi hii haina dini, na msingi wa taratibu na kanuni za maisha ya Watanzania ni katiba zao, basi sihitaji kukukumbusha kuwa hiyo katiba ambayo wale waliokupinga "WALIAPA" kuilinda na kuitetea basi inakataa mambo ya ushoga ndani ya nchi hii ambayo mmoja wa waasisi wake alitangazwa kuwa "MTAKATIFU".
Kuna mengi ya kusema lakini kwa Leo naomba niishie hapa ili nikaribishe matusi na kejeli za wale wote wanaotetea ushoga.
Relief Mirzska.