Bonson
Senior Member
- Apr 20, 2013
- 183
- 147
Ndugu Mheshimiwa,
Kwa muda mrefu umejijengea sifa ya kuwa kiongozi shupavu na usie na hofu kwa yale unayoyaamini. Katika kipindi chako cha Uspika Wa Bunge ulijinadi na kuthibitisha kwamba wewe ni MTU WA SPEED NA VIWANGO. Bila kuonyesha upendeleo wala woga uliwashugulikia mafisadi wanaoliibia Taifa letu. Kwa sababu tusizo zijua, uliondolewa ktk nafasi ya uspika. Hii ilikuumiza na iliwaumiza wengi.
Mheshimiwa, wakati wa sakata la ugonjwa wa ajabu wa Dr. Mwakyembe, ulitoa kauli nyingi kwamba kuna mkono wa mtu (mafisadi). Wengi walishutumu msimamo wako lakini hukujali. Hii yote ilikua inadhihirisha wewe ni MTU JASIRI Na unaeweza aminiwa kwa nafasi ya juu ya uongozi.
Mheshimiwa, Jina lako limekua likitajwa tajwa kwamba utawania URAIS wa nchi yetu. Kwangu binafsi, ni jambo zuri. Lakini nimepata hofu kubwa sana kuhusu kauli yako uliyoitoa bila hofu ukiwa kama MWENYEKITI WA BUNGE MAALUM LA KATIBA. Kauli yako ya kupinga UHURU WA HABARI NA UHURU WA KUJIELEZA umeleta mkanganyiko mkubwa kwa wananchi wengi hasa wale walokua wakikuona kama Rais ajae.
Mheshimiwa, JE, WAWEZA TOA KAULI KUHUSU ULILOLISEMA KUHUSU UHURU WA HABARI?? Je, huo ndio msimamo wako au ni "ULIMI ULITELEZA??"
Kwa mtazamo wangu, kauli hii uliyoitoa inaweza fanyika KABURI la kuzika ndoto zako zote. Tafadhali toa msimamo wako rasmi kuhusu uhuru wa habari na vyombo vya habari.
Asante kwa kua msikivu.
Mungu Ibariki Tanzania.
Kwa muda mrefu umejijengea sifa ya kuwa kiongozi shupavu na usie na hofu kwa yale unayoyaamini. Katika kipindi chako cha Uspika Wa Bunge ulijinadi na kuthibitisha kwamba wewe ni MTU WA SPEED NA VIWANGO. Bila kuonyesha upendeleo wala woga uliwashugulikia mafisadi wanaoliibia Taifa letu. Kwa sababu tusizo zijua, uliondolewa ktk nafasi ya uspika. Hii ilikuumiza na iliwaumiza wengi.
Mheshimiwa, wakati wa sakata la ugonjwa wa ajabu wa Dr. Mwakyembe, ulitoa kauli nyingi kwamba kuna mkono wa mtu (mafisadi). Wengi walishutumu msimamo wako lakini hukujali. Hii yote ilikua inadhihirisha wewe ni MTU JASIRI Na unaeweza aminiwa kwa nafasi ya juu ya uongozi.
Mheshimiwa, Jina lako limekua likitajwa tajwa kwamba utawania URAIS wa nchi yetu. Kwangu binafsi, ni jambo zuri. Lakini nimepata hofu kubwa sana kuhusu kauli yako uliyoitoa bila hofu ukiwa kama MWENYEKITI WA BUNGE MAALUM LA KATIBA. Kauli yako ya kupinga UHURU WA HABARI NA UHURU WA KUJIELEZA umeleta mkanganyiko mkubwa kwa wananchi wengi hasa wale walokua wakikuona kama Rais ajae.
Mheshimiwa, JE, WAWEZA TOA KAULI KUHUSU ULILOLISEMA KUHUSU UHURU WA HABARI?? Je, huo ndio msimamo wako au ni "ULIMI ULITELEZA??"
Kwa mtazamo wangu, kauli hii uliyoitoa inaweza fanyika KABURI la kuzika ndoto zako zote. Tafadhali toa msimamo wako rasmi kuhusu uhuru wa habari na vyombo vya habari.
Asante kwa kua msikivu.
Mungu Ibariki Tanzania.